Serikali: Mafanikio makubwa ya Royal Tour ni kufanikiwa kumshawishi baba yake Rihanna kuja kuishi Tanzania

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200
Serikali ya Tanzania imefanikiwa kuwashawishi wageni wengi kuifahamu Tanzania na kwalo HADI BABA YAKE RIHANNA AMEKUBALI KUJA KUISHI TANZANIA!

Hayo yamesemwa na Msemaji Mkuu wa Serikali bwana Gerson Msigwa.

Asante mama Samia kwa kufanikiwa kumshawishi BABA Rihanna kuja kuishi Tanzania.

Your browser is not able to display this video.
 
Kwa CCM hii mbovu hayo ni mafanikio makubwa sn
 
Huyu mzee ni mwekezaji kwamba anakuja kuongeza tija au kumaliza tu oxygen, (Akishastaafu)? , Kwamba Vigezo vya uhamiaji amekidhi ?, Au ukiwa mzazi wa Rihana tayari unapewa entry

Kweli ni usanii na kuigiza tu kutoka kwenye Sinema yenyewe mpaka kwenye interview na utendaji....
 
Acha uwongo we sukuma gang, kasema wamefaniukiwa kuvuta wawekezaji wengi kuja nchini, pia kutakuwa na direct flights za Tanzania hadi USA
Hilo la baba wa Rihanna ni kama extra tu na sio mafanikio makubwa zaidi kama unavyotaka kuliweka wewe
 
Kupata vichekesho vingine kama hivyo tunabonyeza ngapi mkuu....??
 
Rihanna ndo yule mwenye pigo za kumwabudu shetani bila kificho, sasa baba yake utamtegemea aweje zaidi ya kutuletea watu wa kuhamasisha ushoga.....
 
Hii nchi imeoza tupu
 
Hii nchi kweli hata hatujui nini tunatakiwa tufanye. Ni imelaaniwa.
 
Nongwa hizi sasa ..

Vipi haya sio mafanikio? 👇





 
Aliongea na waandishi kwa sekunde 44 tu kuwaeleza mafanikio ya kuja kwa baba Rihanna basi. Akaondoka, yaani hakuna jingine lolote aliloliongea.

Dah! Hv mbona mi nakuwa muoga sana katika unafiki huku hali ikiwa tofauti kabisa kwa wenzangu?!!!! Tena wengine wakubwa kunizidi?!!!!
 
Sasa Baba yake Rihanna!!!!?si bora mimi mlipakodi angalau nashiriki kujenga nchi!!!Sasa huyu anawekeza Nini Sasa!!!??USA WAMEAMUA KUTUSANIFU!YAANI BIDEN AJE TZ HALAFU TUWAPE BABA YAKE MOND AKAISHI USA!!!?ASANTE MAMA KWA MAFANIKIO YA AWAMU YA SITA!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…