Serikali: Mafanikio makubwa ya Royal Tour ni kufanikiwa kumshawishi baba yake Rihanna kuja kuishi Tanzania

Hahahahah [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Anaupiga mwingi
 
Kwani huyu baba akija atatusaidia nini watanzania? Ataongeza kiasi gani kwenye GDP yetu? Huyu msigwa vipi!!!!
 
Na wewe unaweza kupata mwenza ukaacha kutangatanga
 
Hizi sarcastic thread zinawapa kujiliwaza kwa muda tu. Lakini kibaya ni kwamba hata akili mnaziweka katika mtindo wa kuendekeza udaku na masikhara siku zote. Wale wenye kutazama content nzima ya kitu ndio wanaokuwa wanafanikiwa siku zote.

Akina sisi tunakuwa ni walalamikaji kila kukicha kwa sababu akili zetu ndio kila kitu, unachokiwaza na kukiweka akilini muda mwingi maishani mwako ndicho kinakuja kuwa uhalisia wako siku zote.
 
Acha uwongo we sukuma gang, kasema wamefaniukiwa kuvuta wawekezaji wengi kuja nchini, pia kutakuwa na direct flights za Tanzania hadi USA
Hilo la baba wa Rihanna ni kama extra tu na sio mafanikio makubwa zaidi kama unavyotaka kuliweka wewe
Hahahahaha kwisha habari ni mwendo wa kurukaruka kama maharage yakiwa jikoni hakuna mnacho kijua
 
Acha uwongo we sukuma gang, kasema wamefaniukiwa kuvuta wawekezaji wengi kuja nchini, pia kutakuwa na direct flights za Tanzania hadi USA
Hilo la baba wa Rihanna ni kama extra tu na sio mafanikio makubwa zaidi kama unavyotaka kuliweka wewe
Hahahahaha kwisha habari ni mwendo wa kurukaruka kama maharage yakiwa jikoni hakuna mnacho kijua
 
Tukumbushane tu kilichomzuia Michael Jackson kutembelea Sinza na Ngorongoro
 
Nilichosikia hapo ni kuwa wamepata ahadi nyingi.

Ahadi mtu anaweza timiza au asitimize hivyo hakuna manufaa ya moja kwa moja ya hiyo filamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…