Serikali: Mchakato wa Katiba Mpya na maboresho ya Sheria ya vyama vya Siasa na Uchaguzi, sasa kuanza

Serikali: Mchakato wa Katiba Mpya na maboresho ya Sheria ya vyama vya Siasa na Uchaguzi, sasa kuanza

Sasa mbona hizo Katiba Mpya hazina maana yeyote kwenye maisha yoa? Mbona Zina maisha hovyo kuliko Tanzania..

Mfano Huwa mnazunguka huko mitaani mnawaambia watu eti Katiba Mpya itazuia Serikali Kukopa ,Ghana
,Zambia na Kenya zimefilisika kwa nini Katiba Mpya haikuzuia hayo?

Katiba Mpya is overrated na nasisitiza ni Kwa maslahi ya Wanasiasa na Wala sio Wananchi wa kawaida..

Hivi Kwa mfano maskini hana pesa hiyo Katiba Mpya itamsaidia nini akidhulumiwa Haki Mahakamani?
Kwamba hizo nchi maisha yako hovyo kuliko Tanzania! Unajua unachoongea boss?

Kwamba kuna watu wanasema katiba mpya itazuia nchi kukopa, acha upotoshaji usio na tija, au ni ili hoja yako ionekane ya maana nini?

Ni kweli hiyo katiba mpya ni kwa ajili ya wanasiasa, je hao wananchi wa kawaida wao ni maiti, kwanini hawajitokezi kudai hayo maslahi yao wanasubiri tu wanasiasa wadai maslahi yao?

Katiba hii ya sasa ndio inamruhusu mwananchi masikini kukopa, ila ikija katiba mpya ndio itamzuia kukopa? Hoja yako ni nini hapa, au unaleta ubishani wa jazba?
 
Sina ujinga wa kupoteza mda na Wanasiasa niache kutafuta pesa,mimi.nafahamu kwamba mwanasiasa hawezi kuniletea maisha Bora ila unfortunately Dunia Ina wajinga wenu ndio mtaji wenu.

Sioni kama una jipya zaidi ya jazba za bei rahisi. Ni pesa gani unatafuta boss, hizo hela za mshahara ndio zinakupa kiburi hadi uone katiba mpya haifai?😂😂
 
Kiini macho tu, katiba ya kweli huku Afrika huandikwa baada ya machafuko, au serikali kupinduliwa.
Uhuru wetu tu ulipatikana kwa majadiliano. Haya machafuko unayoyataka sidhani kama utayashuhudia.
 
Sioni kama una jipya zaidi ya jazba za bei rahisi. Ni pesa gani unatafuta boss, hizo hela za mshahara ndio zinakupa kiburi hadi uone katiba mpya haifai?😂😂
Natafuta zote za mshahara na zingine,Sasa Katiba ndio itaniongezea? Wewe si unatafuta za wizi huko kwenye siasa ndio maana umekomaa
 
MCHAKATO WA KATIBA MPYA KUTENGEWA FUNGU KWENYE BAJETI YA 2023/ 2024

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa mchakato wa Katiba Mpya pamoja na maboresho ya sheria ya vyama vya siasa na Uchaguzi unatarajiwa kuanza kufanyiwa kazi baada kupitishwa kwa makadirio ya mapato
Muhimu tu Mama ajitahidi kuwadhibiti Wahafidhina. Enzi za JK, zoezi lilikuwa linaelekea pazuri. Kwa bahati mbaya akaharibu baadaye kwa kuruhusu wanasiasa wabinafsi kuuteka mchakato wote.
 
Sina hakika kama Katiba Mpya itaniongezea chochote Cha maana kwenye maisha yangu hasa nikiangalia kinachoendelea Kenya ,South Africa,Ufaransa..

Hizi mambo nadhani zinawasaidia zaidi Wanasiasa,so ikipatikana sawa isipopatikana sawa.
Hua unasomaga teuzi za rais?
 
Time frame hadi kwenye Referendum, je mchakato utaingiliana na Uchaguzi mkuu ujao au kabla?
 
Bado upo Chato unaomboleza Msiba, hujatua Tanga bado
Huyo jamaa huwa hataki kabisa kusikia habari za jamaa wa Chato yeye ni pro Awamu ya sita ila kitu kimoja hajakijua ni kwamba watu wa Zanzibar ndio wanaoihitaji katiba mpya kupitia Rasimu ya Warioba kuliko hata Wabara wanavyoitaka katiba mpya !! Tusubiri tuone. !!
 
Atleast serikali inaendelea kuonesha nia, ipongezwe; wasiwasi wangu ni kwamba, kwasababu inaonekana Samia ana copy & paste kila kilichofanywa enzi za JK, isije tokea huo mchakato wa Katiba Mpya ukafa kifo kile kilichotokea wakati ule, vyema ajitahidi yeye amalizie alipoishia mwenzake.

Kinyume na hapo, utakuwa ni muendelezo ule ule wa kuchezea pesa za walipakodi, usitokee; pia sitarajii kusikia maneno ya wahafidhina wamegoma kupitisha hiki au kile, hili taifa sio la wahafidhina, ni la watanzania wote, nao kwa umoja wao ndio wanahitaji Katiba Mpya, sasa muhimu maoni yao yafanyiwe kazi kwenye hiyo Katiba itakayopatikana.

Hatuhitaji Katiba Mpya ya watawala kama hii tuliyorithi toka kwa mkoloni, hili taifa limeshakuwa huru ni wakati wa kuonesha hayo kwenye Katiba Mpya, nchi sasa irudi mikononi mwa wananchi.
Ninachofahamu ni kuwa Mh. Rais Samia alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba. Anajua "A" mpaka "Z" ya kilichotokea, hivyo kwa kuwa sasa yeye ndiye raia namba moja mwenye nguvu zaidi, na kwa kuwa kama kweli atakuwa na nia ya dhati ya kutengeneza katiba mpya, sioni chochote wala yeyote wa kumfanya asitimize hili.

Naomba Watanzania wote tunaoitakia mema Tanzania yetu, tumuombee na kumpa ushirikiano ili lengo hili litimie kwa mustakabari mwema wa vizazi vya sasa na vijavyo.

Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki Mh. Rais Samia SS.
Mungu tubariki Watanzania.
 
Back
Top Bottom