Serikali msijisahau katika hili la daktari kumtibia mtu wa jinsia tofauti na yeye

Serikali msijisahau katika hili la daktari kumtibia mtu wa jinsia tofauti na yeye

Mbona kuna hospitali flani wamama wanaojifungua wanapendelea manesi wanaume kuliko wanawake. Tena asiwe mwanamke aliyefunga uzazi tiyari, "panuaa unajifanya kuumia kama vile sisi hatujazaa bhana".
 
Kama hufamu kitu unauliza ndugu yangu..
Sheria/miongozo ipo inayotaka ukienda hospt ukahudumiwa na Dkt wa Kiume na wewe ni jinsia ya kike basi inabidi awepo nesi wa kike wakati wote ukiwa chumba cha daktari na huwa hivo hivo hata kwa wagonjwa wa jinsia ya kiume endapo watakutana na Dkt wa Kike. Na hii inatokea ili kuepusha malalamiko hususani ya wagonjwa wa kike kufanyiwa vitendo visivyo vya kiungwana na madaktar wa kiume.
Hivi umeelewa hoja ya mtoa mada?

Mtoa mada analalamika mgonjwa kutibiwa na dk asiye wa jinsia wa jinsia yake wewe unasema sheria zipo zinataka kama mgonjwa ni ke na dr ni me basi awepo na dr/nesi wa kike,sasa huyo nesi wa kike atazuia vp dr wa kiume kumchungulia mgonjwa?

Hio sheria kama ipo basi itasaidia unyanyasaji wakijinsia ila mambo mengine kama kuchungulia hio sheria itasaidia vipi?

Nikuulize swali,hivi endapo ikitokea mama wa dr wa kiume ni mjamzito je huyu dr wa kiume anaweza kumzalisha mama yake chini ya uwepo wa dr/nesi wa kike?

Kwavyovyote dr ataomba ma dr wenzake wamzalishe mama yake kwani kwa utamaduni wakiafrika sio heshima.

Sasa inakiwaje vi dr vidogo vinapata ujasiri wakuchungulia wamama wenye rika sawa na mama zao?
 
Mkuu habari ya tiba ni kitu kingine kabisa, wanawake sio wazuri na kujali sana kwenye huduma,
Mwaka 2013 Temeke hospital mke wangu alienda kujifungulia pale akiwa na mimba ya mapacha, mmoja akatoka vizuri tu mwingine akagoma tena kaenda kujificha juu madr wa4 wa kike waliokua wanamhudumia wakawa wanashauri afanyiwe operesheni lkn kabla hawajafikiwa maamuzi wakaenda kuita madr wawili wa kiume walianza kumpushi yule mtoto wanavyojua wao hadi akajifungua kawaida.
Hapo sio kwamba wameweza kwa sababu ni wanaume ati na wale wameshindwa kwa sababu ni wanawake no no.

Hao wameweza pengine kwa sababu wana ujuzi zaidi na uzoefu kuliko hawa wanawake.

Wanawake wanahitaji wafundishwe vizuri sana kwa utawi wa jamii.

Alafu pia kwa kesi kama yako wapo madaktari wa kike wazuri kwa kuzalisha hao walikuwa labda wamepanick au maarifa madogo,lakini sio kwamba ati walishindwa kwa sababu ati ni wanawake hapana
 
Unapotetea uhai unajali Mambo ya aibu?
Huu NI ujinga kabisa
Mbele ya kifo unasema naona aibu!!!!
Madaktari NI wachache kwanza lazima muelewe
Mkuu kama umekereka tusamehe bure.

Ila hapa tunakubali kuwa madaktari ni wachache na ndio maana haya yote yanatokea.

Ndio maana tukatoa suluhisho kuwa wanawake wasomeshwe ili kusudi sasa hao madaktari wawe wengi,usipanick mkuu haya ni mambo ya kawaida
 
Kama hufahamu kitu unauliza ndugu yangu..

Sheria/miongozo ipo inayotaka ukienda hospt ukahudumiwa na Dkt wa Kiume na wewe ni jinsia ya kike basi inabidi awepo nesi wa kike wakati wote ukiwa chumba cha daktari na huwa hivo hivo hata kwa wagonjwa wa jinsia ya kiume endapo watakutana na Dkt wa Kike. Na hii inatokea ili kuepusha malalamiko hususani ya wagonjwa wa kike kufanyiwa vitendo visivyo vya kiungwana na madaktar wa kiume.
Mkuu ili haya yasiwe madai tuwekee ushahidi hapa wa hayo uliyoyasema ili tupate faida isiwe inaishia kwemye kudai tu mkuu
 
Kinachouma mama mzazi anaenda hospitali anakutana na daktari ambaye ana umri kama wa mimi mwanae alafu madaktari wa kike wapo kabisa.

Kuna mama wa kipemba wakati anajifungua alitaka kuja daktari wa kiume, basi mama mpemba akamuuliza "uko radhi kuchungulia tv ya mamayo wee "?

Daktari akaenda mbio
Ilikuwaje hapo awali ambapo ma Dr wa kike hawakuwepo, mambo siku hizi wamebadilika, unaweza kukuta mama yako kazaa midume tu na uzee umemfika na siku hizi kupata wahudumu au wasaidizi wa kazi ni kazi .
 
Kwanza kabisa nakusihi uache wivu.

Tanzania Kuna madaktari wa kiume wengi kuliko wanawake. Lakini pia Tanzania wanao attend hospital wengi Ni wanawake.

Pia Kuna manesi wengi to wakiume waliosomea kuzalisha pale labour.
Vumilia tu Kaka, kuona si kuchukua Wala kutumia.
Kwa nini polisi katika upekuzi kumpekua mtuhumiwa hutumiwa wanawake,mbona hata polisi mwanaume asitumike kumpekua mhalifu wa kike ?

Unaonaje juu ya polisi wa kiume kumpekua kila sehemu mtuhumiwa wa kike ?
 
Unapotetea uhai unajali Mambo ya aibu?
Mkuu hata polisi anapotetea usalama akitumia hoja hii kwamba usalama kwanza manake polisi wa kiume ana haki ya kumpekua mpaka mtuhumiwa wa kike kwa maslahi mapana ya taifa pengine kaficha mabomu hata sehemu za siri.

.kwa nini polisi wa kiume asitumie hoja ya usalama kumpekua mtuhumiwa wa kike ?
Mbele ya kifo unasema naona aibu!!
Manake tuhalalishe polisi mwanaume akitaka kumpapasa mtuhumiwa mwanamke kwa kumkagua,mtuhumiwa akikataa na kusema hiyo ni udhalilishaji huyu polisi anaweza kumuambia "mbele ya usalama unaona aibu ?".

Hapana swrikali yetu iangalie hili jambo kwa upana wake
 
Ilikuwaje hapo awali ambapo ma Dr wa kike hawakuwepo
Kwa hiyo hata wanawake ambao wangesomeshwa udaktari wakaja kupunguza wimbi hili hawakuwepo hao wanawake ?

Hao madaktari wa kiume kumbuka wamwtengenezwa,basi na hawa wa kike tuwatengeneze pia.
 
Mimi hupenda kuhudumiwa na dr mwanaume hayo ya utu uzima sijali, pia ukiwa na dr wakiume nurse wa kike lazima awepo same applies na kukiwa na Dr wa kike lazima nurse mwanaume awepo, so uoga kwenye kuumwa hauna mashiko
 
Wakuu naomba niipongeze serikali kwa jitihada zake inazofanya katika kuhakikisha ile heshima ya jinsia zote inalindwa.

Tukiangalia katika majeshi hasa jeshi la polisi utakuta kuna askari wa kike ambao kama itatokea muhalifu ni mwanamke basi askari yule hakuajiriwa kwa bahati mbaya bali hiyo itakuwa ni kazi yake kumpekua sehemu za mwili wake.

Hali kadhaalika mwanaume atapekuliwa na askari wa kiume katika kulinda heshima.

Hata mashuleni kuna waalimu wa kike kibao ambao wao watashughulikia masuala mbali mbali ya wanafunzi wa kike.

Mbona sioni suala hili la kuheshimu jinsia na kulinda heshima ya mtu likifanyika na kusisitizwa katika kada ya afya ?

Kwa nini isiwe kosa daktari wa kumtibia mgonjwa wa jinsia tofauti na yeye ikiwa katika hospitali hiyo ama maeneo hayo kuna daktari mwenye jinsia sawa na mgonjwa ?

Kama ambavyo polisi haruhusiwi kumfanyia upekuzi wa mwili mtu wa jinsia isiyekuwa yake wakati wa jinsia yake wakiwa pale hii ni kosa,vipi isiwe kosa katika hii kada ya afya ?

Yani utakuta hospitali kuna madaktari wa jinsia nyingi lskini mwanamke anatibiwa na mwanaume au kinyume chake.

Serikali isomeshe watoto wengi wa kike ili kuja kuepusha hii aibu,ipunguze vigezo vya kusomea udaktari kwa mwanamke hasa kwa mambo ya kawaida haya ambayo hayahitaji kujitoa sana wanawake wasomeshwe waje kuzalisha wanawake wenzao.

Chumba cha kuzalisha kuna madaktari wa kike watano na wa kiume mmoja,huyu wa kiume anatafuta nini,kwa nini isiwe kosa kisheria?
Umeongea ovyo uonekane unalogic kumbe hewa tu kama hujui miongozo ya udaktari uliza ndo uje jukwaani
 
Mkuu kama umekereka tusamehe bure.

Ila hapa tunakubali kuwa madaktari ni wachache na ndio maana haya yote yanatokea.

Ndio maana tukatoa suluhisho kuwa wanawake wasomeshwe ili kusudi sasa hao madaktari wawe wengi,usipanick mkuu haya ni mambo ya kawaida
Kumbuka tu
Mficha uch hazai
Mficha maradhi kilio kitamuumbua
 
Mimi hupenda kuhudumiwa na dr mwanaume hayo ya utu uzima sijali, pia ukiwa na dr wakiume nurse wa kike lazima awepo same applies na kukiwa na Dr wa kike lazima nurse mwanaume awepo, so uoga kwenye kuumwa hauna mashiko
Ulikuwa wap kumuelekeza ndugu yetu mpka anakurupuka ivooo
 
Hili ni ambalo linafanywa hata na wanaume mm wake zangu wanazalishwa na madaktari wa kike na hiki unachokisema hakija tokea,kukosa umakini hakuzingatii jinsia ya dokta.
Ina maana una wake wangapi?
Acha umalaya na wivu unao huku mwenyewe una Kijiji Cha wanawake
 
Mbona kuna hospitali flani wamama wanaojifungua wanapendelea manesi wanaume kuliko wanawake. Tena asiwe mwanamke aliyefunga uzazi tiyari, "panuaa unajifanya kuumia kama vile sisi hatujazaa bhana".
Wanawake tunapenda ma Dr na na nurse wa kiume, ukikutana na mwanamke ni roho mbaya tu hawajui kupet pet
 
mkuu,

unaongelea pumb* zipi? kama ni hizi hizi za kwetu omba zisikuume..maana maumivu yake hatari... hutojali jinsi wala umri wa doctor...
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwa hiyo hata wanawake ambao wangesomeshwa udaktari wakaja kupunguza wimbi hili hawakuwepo hao wanawake ?

Hao madaktari wa kiume kumbuka wamwtengenezwa,basi na hawa wa kike tuwatengeneze pia.
Hii unayo ongelea au kutamani ni option
Kama Dr unayemtaka yupo, la sivyo awe Mwanamke au Kiume utatibiwa naye, uki kata ni juu yako na afya yako
 
Back
Top Bottom