serikali gani unayoiambia,hii inchi imejaa vilaza,umeshasikia meneja wa TRA katumbuliwa kwa mambo kama hayo ,hujui kuwa hao unaowasema wanapangiwa kiasi cha kukusanya na hiyo serikali yako,wasipotimiza lengo imekula kwao,NI LAZIMA ATUMIE NGUVU KUKUSANYA MAPATO,NAMPONGEZA SANA ,TENA AZIBURUTE BAJAJI HATA KWA KIFARU ZILIPE KODINimepata bahati ya kuja masasi kula sikukuu ya xmass na nimepata bahati ya kuongea na watu tofauti tofauti hasa wafanyabiashara
Asilimia kubwa ya wafanyabiashara ambao tumekaa na kuongea nao malalamiko yao makubwa ni kutoka kwa Meneja wa TRA Masasi
Huyu jamaa anazorotesha sana biashara kwa kuwafungia watu maduka yao, yani yale mambo ambayo Rais huwa anaagiza kuwa watu wa TRA waongee vizuri na wafanyabiashara ni gumu sana kwa huyu jamaa.
Nilishangaa kusikia mpaka waendesha bajaji na wao wanamchukia sana, anafunga bajaji zao na kuzivuta kwa gari.
Wafanyabiashara wengi wameanza kuondoka Masasi na kwenda mikoa mingine kutokana na usumbufu wa huyu meneja.
Najua Serikali inapita kwenye hili jukwaa basi fanyieni kazi malalamiko ya wafanyabiashara hawa wa Masasi.
Sent from my itel A11 using JamiiForums mobile app