Serikali na CCM walivyo na sikio la kufa lisilosikia dawa, tayari wanataka kuanzisha vita nyingine kubwa na hatari zaidi na Kanisa la Mungu

Serikali na CCM walivyo na sikio la kufa lisilosikia dawa, tayari wanataka kuanzisha vita nyingine kubwa na hatari zaidi na Kanisa la Mungu

Kinachotafutwa hapa ni vita ya udini baada ya kuonekana ya uzanzibari vs utanganyika umeshindikana,, Mungu bado anaipenda Tanzania tuendelee kuiombea,,
Tuzichape tu maana kuheshimiana hakupo tena
 
Ni hatari sana..

Kuna kila dalili kuwa, baada ya tamko la Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC), vita ya skandali la bandari inakwenda kuchukua sura nyingine kati ya kikundi kilichomo ndani ya serikali kilichotengeneza uchafu huu na Kanisa la Mungu.

Na bila shaka TEC imetangulia tu na muda si mrefu The Christian Council of Tanzania (CCT) na The Council of Pentecostal Churches of Tanzania (CPCT) nao wanakuja na matamko yao na misimamo yao na tunafikiri yatakuwa ni matamko ya namna gani?

Obvious ni kuukataa mkataba huu kwani kwa sababu ziwazo zote, hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu na hajahongwa anaweza kukubaliana na ujinga na uchafu huu unaoitwa IGA kati ya Dubai Emirate na Tanzania.

Kama Rais Samia Suluhu Hassan akishindwa kutumia fursa hii kwa serikali yake kurudi kwenye drawing board ili kufikiria namna nyingine ya ubia wa uboreshaji wa bandari zetu badala ya mkataba huu mbovu na Dubai kupitia kampuni yao ya DP World, basi awe tayari kuanza kuitumikia hukumu yake yeye na watu wake wote walio nyuma ya scandal hii.

Ni hukumu yake kwa sababu dalili zinaonesha kuwa hiki kikundi baada ya kumshawishi Rais na Kwa baraka zake kinakwenda kuanzisha vita na kanisa la Mungu.

Hili likitokea, basi itakuwa ni heri ya wapiganiao haki maana hakuna mamlaka ya serikali yoyote ya kidunia imewahi kushindana na Kanisa la Mungu na mamlaka hiyo ikasimama na kushinda. Tunayo mifano mingi ktk historia ya Biblia kama vile Babeli ya kale, dola la Rumi ya kale, Misri ya Farao nk.

Rais Samia Suluhu Hassan, za kuambiwa changanya na za kwako mama. Wewe ni mwanamke, usiingie ktk historia ya wanawake viongozi wa hovyo waliowahi kuongoza nchi zao na kutoka kwa aibu.

Hata wao wanajua fika wameingia cha kike kwenye huu mkataba,shida ni ule mzigo waliokula[emoji28][emoji28] wanarudishaje pesa za mwarabu.
 
Maslahi yakiguswa mahali kuna tonge na unawapokonya basi tegemea kelele za aina zote

Goods exempt from tax zilianza miaka yaani kabla hata ya Uhuru

Ila kuna watu wanaitumia vibaya wanaingiza kila kitu kupitia bandari wakisingizia msamaha wa Kodi.

Humo humo wanatakatisha na hela haramu.

Kila mmoja alipe kodi na tuache wizi na kujiita wapenda nchi na rasilimali zake huku kuna maslahi binafsi

Ukisimamishwa mahakamani ulete ushahidi kwa haya unayoyasema utatoa huo ushahidi au una jisemesha humu na wewe uonekane umesema.
 
Na bila shaka TEC imetangulia tu na muda si mrefu The Christian Council of Tanzania (CCT) na The Council of Pentecostal Churches of Tanzania (CPCT) nao wanakuja na matamko yao na misimamo yao na tunafikiri yatakuwa ni matamko ya namna gani?
Mbona unawabagua Bakwata? 😀 😀 😀 😀 😀 😀
 
Kitachofuata hapo ni vita ya udini. Waislamu uchwara(Muislam anaejitambua hawezi tetea upumbavu huu) wanaofikiria matumbo yao watapewa ubwabwa waanze kutumia misikiti kujibu maaskofu. Kipindi hicho wanaotoa hayo majibu hata hawajui kilichoandikwa kwenye hiyo mikataba.
 
Huu mkataba haufai...Samia FUTA Hili dude tumekataa,, Hata wakija tutawahujumu tuuu
 
Back
Top Bottom