Serikali pangisheni yaliyokuwa majengo ya Wizara na Taasisi mbalimbali DSM vijana tupate ofisi na ninyi mpate kodi

Serikali pangisheni yaliyokuwa majengo ya Wizara na Taasisi mbalimbali DSM vijana tupate ofisi na ninyi mpate kodi

sajo

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
3,474
Reaction score
6,195
Ni zaidi ya miaka 5 sasa toka Rais JPM alipoagiza Wizara zote za Serikali kuhamia jijini Dodoma yalipo makao makuu ya nchi. Agizo la rais ni sheria, hibyo lilitekelezwa kwa ukamilifu na sasa Wizara karibu zote zimehamia Dodoma ambapo zina majengo katika mji wa serikali Mtumba.

Kwa miaka yote hiyo zaidi ya 5, majengo yaliyokuwa yakitumiwa na wizara hizo jijini Dar es Salaam yamebaki wazi, hayatumiki na yamekuwa kama magofu. Maana nyumba isiyotumika ni lazima ichakae.

Sasa basi ninaona ni muda muafaka, serikali ipangishe majengo haya kwa bei nafuu ili vijana wengi wanaojiajiri wapate ofisi wajiongezee thamani kwa kazi zao na pia wajipatie kipato.

Tunajua kuwa ofisi ni anuani, mteja anakuwa na amani akifanya kazi na mtu ambaye anakua na ofisi. Wekeni viwango hata vya Tshs. 10,000/= kwa skwea mita, mtakua mmetatua tatizo la ajira, mtakua mmeinua vijana na wakati huohuo mtaongeza chanzo cha mapato (kodi).

Kuna majengo kama lile lililokuwa likitumiwa na Wizara ya Katiba na Sheria lenye takribani ghorofa 10 hali yake kwa sasa inasikitisha, vioo vinavunjika, madirisha hayafungi ilhali lilikuwa ni jengo zima kabisa.

Pangisheni lile. Na pale ofisi za Takwimu yalipokua makao makuu ya NIDA kuna jengo limechoka vibaya kwa sasa lakini zamani lilikua vyema kabisa, pangisheni. Hata pale ilipokuwa wizara ya Kazi, jengo limebaki tu. Fanyeni hivyo kwa majengo yote yaliyobaki wazi na yanaendelea kuchakaa.

Tunaomba serikali mlifanyie kazi hili, kama mtakosa nguvu kazi ya kusimamia, niteueni mimi nifanye kazi hiyo, majengo yarudi kwenye ubora na vijana wapate ofisi.

Mhe. Dkt. Gwajima D wizara yako inahusika kabisa kwa upande wa maendeleo ya vijana, naomba ufikishe hili kwenye vikao vya baraza la mawaziri. Ahsante
 

Attachments

  • VID_2023-04-29-14-25-02-000.mp4
    14.1 MB
Unazo pesa za kutosha za kulipa Kodi ya Pango?
Bei ya NHC kwa sasa ni Tshs. 15,000/= kwa skwea mita, wao wafanye sio zaidi ya Tshs. 10,000/= hatutashindwa kulipa kodi ya pango. Hata wakifanye Tshs. 3,000/= kwa skwea mita bado ni bora na faida kwa serikali kuliko kuacha majengo yachakae na kuwa hifadhi za popo.
 
Mbona majengo mengi tu huko Posta yako tupu. Ukitaka kupanga unapata kirahisi sana

Ila tu mengi yanalipiwa kwa USD, na kwa square metre. .
Mkuu hayo ni majengo ya watu binafsi, yanahudumiwa kwa usafi - hayachakai na hoja yangu sio kuwa, Posta kuna uhaba wa majengo ya kupanga. Mimi nazungumzia majengo ya serikali yaliyojengwa kwa kodi za wananchi. Yanavyobaki wazi ni hasara kwa wananchi, ni kama vile kodi yetu inakua imetupwa tu, jengo linachakaa na halizalishi chochote. Ndio natoa mbadala kuwa serikali wayapangishe ili yasaidie wananchi na pia yaokolewe yasiendelee kuchakaa.
 
Lowassa aliwahi kusema tatizo la serikali ya wabongo hamnaga mwenye maamuzi wala vision, nakumbuka walivyoua Embassy hotel kifala tu hadi likawa gofu, na hizo ofisi ndicho kitakachofuata
Kweli kabisa aisee. Yaani unaona kabisa jengo linachakaa na viongozi wanapita hapo kila siku, hawaoni namna ya kuliokoa na wala hawaumii kuona uharibifu unaotokea
 
Kweli kabisa aisee. Yaani unaona kabisa jengo linachakaa na viongozi wanapita hapo kila siku, hawaoni namna ya kuliokoa na wala hawaumii kuona uharibifu unaotokea
Jengo likikaa bila wapangaji na repair ndani ya miaka mitano tu linakua halifai tena kwa matumizi hadi likarabatiwe tena, lakini ndugu zetu haya wanayajua au wanajua na kupuuza tu kwa kuwa ni mali ya umma nani anajali!
 
Back
Top Bottom