Serikali wekeni dini mbali na mambo yenu ya Kiserikali ili nyote muwe huru

Serikali wekeni dini mbali na mambo yenu ya Kiserikali ili nyote muwe huru

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Wiki hii watu wametokwa na povu sana kutokana na matukio mbalimbali yalioashiria mwanzo wa kuanza kutomaswa tomaswa kwa dini zao ambazo zilikuwa zimepewa hadhi maalum ya kuwa zisizogusika au 'untouchables' kwa muda mrefu.

Mzee wa Upako ni mmojawapo wa watu waliotokuwa na povu hilo hadi kufikia hatua ya kutoa vitisho mbalimbali kwa utawala ambao muda mrefu amekuwa swahiba wake wa karibu sana. Wapo waliotokwa na povu na kamata kamata zinazofanywa makinasani

Ni wakati sasa wa Serikali kujifunza na kuisogeza dini mbali kabisa na mambo yake.
Hakuna haja kila jambo la kiserikali linapofanyika likaunganishwa na mambo ya kidini. Hakuna haja ya kuwa na mabaraza ya kidini yenye muelekeo wa ushawishi wa kiserikali.Hakuna haja ya kubebana na viongozi wa kidini katika kila tukio la kiserikali.

Mambo ya kidini yakiwekwa mbali na serikali. Itakuwa na faida kubwa kwa serikali, viongozi wa dini na waumini wa dini kwa sababu wote watakuwa na uhuru mkubwa wa kutenda na kusimamia yale wanayoamini ni sahihi na yenye maslahi kwao.
 
Huyu mama asipoangalia hatotoboa maana ameanza kugusa sehemu hatari
 
Sasa hivi video youtube za wenye zama yao zimejaa wanatimiza ubabe wao bila woga.
 
Nasisi tusichanganye siasa na dini,haikua na ulazima wa kuvaa gwanda za chama na kuingia kanisani kwa kisingizio cha maombi.
Tusome alama za nyakati
Uko sahihi kanisani si sahihi kuingia na nguo ya chama iwe CCM au CHADEMA ni sawa na kufanya mkutano wa siasa ndani ya kanisa

viongozi wa dini kwa hili wakemee

vikao vyao vya siasa wafanyie nje ya kanisa sio ndani ya kanisa kwa kisingizio cha tumekuja kufanya maombi kuombea Mbowe au yeyote

mavazi ya vyama yawe nje ya kanisa na viongozi wa dini kwa hili wawe makini nalo
 
Nasisi tusichanganye siasa na dini,haikua na ulazima wa kuvaa gwanda za chama na kuingia kanisani kwa kisingizio cha maombi.
Tusome alama za nyakati
Hoja yako haina mashiko. Tangu lini serikali ilianza kuwapangia watu nguo za kuvaa? Mbona mara nyingi tu unakuta akina mama na wabibi wamevaa kanga, vitenge na vilemba vya ccm kwenye ibada makanisani! Lakini hakuna aliye lalamikia?

Nongwa wakivaa chadema! Halafu Makanisa yalitoa malalamiko yoyote yale serikalini? Au ni kiherehere tu cha policcm kutaka kuonekana kwa mabosi wao wa ccm!
 
Hoja yako haina mashiko. Tangu lini serikali ilianza kuwapangia watu nguo za kuvaa? Mbona mara nyingi tu unakuta akina mama na wabibi wamevaa kanga, vitenge na vilemba vya ccm kwenye ibada makanisani! Lakini hakuna aliye lalamikia?

Nongwa wakivaa chadema! Halafu Makanisa yalitoa malalamiko yoyote yale serikalini? Au ni kiherehere tu cha policcm kutaka kuonekana kwa mabosi wao wa ccm!

Kanisani ni neutral ground siasa za vyama huko nje ya kanisa si sahihi hata kama linafanywa na CCM

Hata majeneza iwe ni marufuku kufunikwa bendera ya chama chochote linapoingizwa kanisani walazimishwe kutoa tambala lao nje ya mlango wa kanisa

kanisani sio ofisi ya chama chochote cha siasa
 
  • Thanks
Reactions: len
Nani kasema kuvaa mavasi ya chama kanisani ni kosa? Kama kweli kila mtu ana uhuru wa kuabudu na uhuru wa kufuata na kushiriki siasa, kupitia chama chochote basi utaona si kosa. Kila mtu amind mambo yake. Hii inaonekana inshu kwa sababu ya wanasiasa wanaingia dini na dini zinaingilia wanasiasa.

Nakubaliana na mto mada kwamba, kama wanasiasa hawatatumia viongozi wa dini na viongozi wa dini wakakaataa kutumika na wanasiasa mambo yatakuwa shwari
 
kanisani ni neutral ground siasa za vyama huko nje ya kanisa si sahihi hata kama linafanywa na CCM

Hata majeneza iwe ni marufuku kufunikwa bendera ya chama chochote linapoingizwa kanisani walazimishwe kutoa tambala lao nje ya mlango wa kanisa

kanisani sio ofisi ya chama chochote cha siasa
Kubali polisi wetu wanakosa weredi kwenye masuala madogo madogo! Na pia wanapenda sana kufanya vitu vya kitoto wakati fulani, ili tu kujionesha wapo kwa lengo la kuilinda serikali ya ccm.

Leo hii nikikuiliza sare za Chadema ni zipi, sidhani kama utakua na jibu sahihi. Na ndiyo maana hata Askofu aliamua kuwaumbua hao polisi waliokwenda kanisani na kusababisha taharuki! Kwa sababu hawakuwa na sababu ya msingi, zaidi tu ya kujikomba komba kwa watawala wa ccm.
 
Wiki hii watu wametokwa na povu sana kutokana na matukio mbalimbali yalioashiria mwanzo wa kuanza kutomaswa tomaswa kwa dini zao ambazo zilikuwa zimepewa hadhi maalum ya kuwa zisizogusika au 'untouchables' kwa muda mrefu.

Naona umejipa kazi ya kumshauri kenge.

Akikusikia bila damu kumtoka masikioni usiache kutuletea mrejesho.

Serikali 'sikivu' Inaposikia nusu nusu

Nilidhani tuliacha kumshauri tangia tulipoachana kwenye mataa?

Baada ya siku 100: Tunapoachana kwenye Mataa na Rais Samia

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kubali polisi wetu wanakosa weredi kwenye masuala madogo madogo! Na pia wanapenda sana kufanya vitu vya kitoto wakati fulani, ili tu kujionesha wapo kwa lengo la kuilinda serikali ya ccm.

Leo hii nikikuiliza sare za Chadema ni zipi, sidhani kama utakua na jibu sahihi. Na ndiyo maana hata Askofu aliamua kuwaumbua hao polisi waliokwenda kanisani na kusababisha taharuki! Kwa sababu hawakuwa na sababu ya msingi, zaidi tu ya kujikomba komba kwa watawala wa ccm.
Sare za Chadema zinaeleweka vizuri ni yale magwanda ya mgambo na zile Tshirt zao zenye rangi za chama chao

Huyo askofu naye aliruhusuje watu waliovaa nguo za chama kugeuza kanisa kikao cha chama waliingiaje kanisani na nguo za vyama vyao? yaani polisi wana ufahamu mkubwa kwenye hilo swala kuliko yeye Askofu .Very sad
 
Hoja yako haina mashiko. Tangu lini serikali ilianza kuwapangia watu nguo za kuvaa? Mbona mara nyingi tu unakuta akina mama na wabibi wamevaa kanga, vitenge na vilemba vya ccm kwenye ibada makanisani! Lakini hakuna aliye lalamikia?

Nongwa wakivaa chadema! Halafu Makanisa yalitoa malalamiko yoyote yale serikalini? Au ni kiherehere tu cha policcm kutaka kuonekana kwa mabosi wao wa ccm!
Mkiendelea na haya mawazo mtajikuta mmechafuliwa na tope la CCM matokeo yake mfanane nao, wananchi washindwe kuwatofautisha then iwe faida kwa CCM.
 
Sare za Chadema zinaeleweka vizuri ni yale magwanda ya mgambo na zile Tshirt zao zenye rangi za chama chao

Huyo askofu naye aliruhusuje watu waliovaa nguo za chama kugeuza kanisa kikao cha chama waliingiaje kanisani na nguo za vyama vyao? yaani polisi wana ufahamu mkubwa kwenye hilo swala kuliko yeye Askofu .Very sad
Aisee!! Basi sawa. Kwa ushahidi wako huu, iwapo na hao policcm watautumia mahakamani, basi saa mbili tu asubuhi watakuwa wameshindwa kesi.

By the way, namuunga mkono Mhashamu Baba Askofu kwa kuwazodoa hao polisi hadharani. Maana alikuwa sahihi kwa 100%
 
Mkiendelea na haya mawazo mtajikuta mmechafuliwa na tope la CCM matokeo yake mfanane nao, wananchi washindwe kuwatofautisha then iwe faida kwa CCM.
Tukiendelea kivipi sasa! Mimi ni raia mwema tu nisiye na chama. Ila sifurahii baadhi ya madudu yanayofanywa na polisi kwa lengo la kiwafurahisha watawala wa ccm.

Mimi siyo Kiongozi wa Chadema! Najaribu tu kutoa mtazamo wangu.
 
Aisee!! Basi sawa. Kwa ushahidi wako huu, iwapo na hao policcm watautumia mahakamani, basi saa mbili tu asubuhi watakuwa wameshindwa kesi.

By the way, namuunga mkono Mhashamu Baba Askofu kwa kuwazodoa hao polisi hadharani. Maana alikuwa sahihi kwa 100%
Askofu wala hakutakiwa kutoka kwenye press alitakiwa aongee nao kimya kimya aelezwe kipi ni kipi.Naye hana weledi kwenye mambo mazito

Anyway maaskofu wenzie watamnongoneza ataelewa sidhani kama tukio kama hilo atakubali lirudiwe tena la watu kuingia na ma uniform ya vyama vyao kanisani!!!
 
Tukiendelea kivipi sasa! Mimi ni raia mwema tu nisiye na chama. Ila sifurahii baadhi ya madudu yanayofanywa na polisi kwa lengo la kiwafurahisha watawala wa ccm.

Mimi siyo Kiongozi wa Chadema! Najaribu tu kutoa mtazamo wangu.
Ok, ila mtazamo wa aina yako hautakiwi kuwepo, huo utetezi ulioutoa utawapoteza Chadema, watafute mbinu mpya za kufanya siasa zao sio kuwaiga CCM, watadumaa, two wrongs can't make it right.
 
Back
Top Bottom