Serikali wekeni dini mbali na mambo yenu ya Kiserikali ili nyote muwe huru

Serikali wekeni dini mbali na mambo yenu ya Kiserikali ili nyote muwe huru

Bas na ww ni sehem ya hili tatzo kwa sababu uliliona na ukalikalia kimya kipindi hicho chote had limefikia hatua mbaya ndio unajidai kulikemea huo ni unafiki
Kama unasubili mm nikuambie subili hivyohivyo na ubavicha wako
 
Sare za Chadema zinaeleweka vizuri ni yale magwanda ya mgambo na zile Tshirt zao zenye rangi za chama chao

Huyo askofu naye aliruhusuje watu waliovaa nguo za chama kugeuza kanisa kikao cha chama waliingiaje kanisani na nguo za vyama vyao? yaani polisi wana ufahamu mkubwa kwenye hilo swala kuliko yeye Askofu .Very sad
Huku kwetu wafuasi wa ccm kila jumapili wanavaa nguo za ccm,mbona sijaona akari yeyote akiwakamata?
 
Huku kwetu wafuasi wa ccm kila jumapili wanavaa nguo za ccm,mbona sijaona akari yeyote akiwakamata?
Si sahihi iwe imefanywa na CCM au Chadema viongozi wa dini wakemee
Nyie Chadema na nyie Acheni kuiga kila kitu CCM

Kama mnapenda kuiga si mjiunge tu na CCM tujue kuwa nyie CCM pia sio Chadema?
 
Si sahihi iwe imefanywa na CCM au Chadema viongozi wa dini wakemee
Nyie Chadema na nyie Acheni kuiga kila kitu CCM

Kama mnapenda kuiga si mjiunge tu na CCM tujue kuwa nyie CCM pia sio Chadema?
Ubaya unapokuja baadhi ya watu wakivaa sare za ccm makanisani siyo kosa ila wakivaa baadhi ya watu sare za chadema kanisani wanahamasisha fujo,jeshi la polisi lisitumike vibaya kwa vile tu IGP ni kada kindaki ndaki wa ccm na si vinginevyo,tuliona alitaka kugombea ubunge kupitia ccm jimboni kwake alikozaliwa,na kama siyo msimamo wa Magufuri basi IGP huyu tulie nae angekuwa mbunge kupitia ccm.
 
Ubaya unapokuja baadhi ya watu wakivaa sare za ccm makanisani siyo kosa ila wakivaa baadhi ya watu sare za chadema kanisani wanahamasisha fujo,jeshi la polisi lisitumike vibaya kwa vile tu IGP ni kada kindaki ndaki wa ccm na si vinginevyo,tuliona alitaka kugombea ubunge kupitia ccm jimboni kwake alikozaliwa,na kama siyo msimamo wa Magufuri basi IGP huyu tulie nae angekuwa mbunge kupitia ccm.
Kifupi wewe Chadema na mapadri na maaskofu wasiojielewa waambie nguo za chama hazitakiwi kanisani ziwe za CCM au Chadema nk
 
Uko sahihi kanisani si sahihi kuingia na nguo ya chama iwe CCM au CHADEMA ni sawa na kufanya mkutano wa siasa ndani ya kanisa

viongozi wa dini kwa hili wakemee

vikao vyao vya siasa wafanyie nje ya kanisa sio ndani ya kanisa kwa kisingizio cha tumekuja kufanya maombi kuombea Mbowe au yeyote

mavazi ya vyama yawe nje ya kanisa na viongozi wa dini kwa hili wawe makini nalo
Binafsi sijajua kabisa ktk eneo hili;
Yaani mtu akihudhuria ibada iwe kanisani au msikitini na nguo yenye maandishi anakuwa ametenda kosa? Ikiwa ni kosa,atakuwa amelikosea kanisa/msikiti husika au serikali?? Au tatizo ni aina ya maandishi yatayosomeka kwenye nguo husika?
Maana km nguo zenye maandishi ni makosa kuhudhuria nazo ibadani,mbona siku zote na hadi hii leo waumini tunavaa nguo zikiwa na maandishi na michoro mbalimbali na hakujawahi kuwa na makosa wala hatukupata kusikia viongozi wa madhehebu wakitoa ilani ya aina hiyo? Mbona km inawafikirisha hata kudhan km mnasaidia kuwapa promo ya bure watu hao mnapowaambush!
 
Wiki hii watu wametokwa na povu sana kutokana na matukio mbalimbali yalioashiria mwanzo wa kuanza kutomaswa tomaswa kwa dini zao ambazo zilikuwa zimepewa hadhi maalum ya kuwa zisizogusika au 'untouchables' kwa muda mrefu.

Mzee wa Upako ni mmojawapo wa watu waliotokuwa na povu hilo hadi kufikia hatua ya kutoa vitisho mbalimbali kwa utawala ambao muda mrefu amekuwa swahiba wake wa karibu sana. Wapo waliotokwa na povu na kamata kamata zinazofanywa makinasani

Ni wakati sasa wa Serikali kujifunza na kuisogeza dini mbali kabisa na mambo yake.
Hakuna haja kila jambo la kiserikali linapofanyika likaunganishwa na mambo ya kidini. Hakuna haja ya kuwa na mabaraza ya kidini yenye muelekeo wa ushawishi wa kiserikali.Hakuna haja ya kubebana na viongozi wa kidini katika kila tukio la kiserikali.

Mambo ya kidini yakiwekwa mbali na serikali. Itakuwa na faida kubwa kwa serikali, viongozi wa dini na waumini wa dini kwa sababu wote watakuwa na uhuru mkubwa wa kutenda na kusimamia yale wanayoamini ni sahihi na yenye maslahi kwao.
Dini imekuwa "overrated" sana kiasi kwamba baadhi ya Viongozi wa Dini wamekuwa wakizitumia Dini hizo na madhabahu kufanya Siasa. Hicho ni kitu hatari sana kikiachwa.

Wapo Viongozi wa dini ambao dhahiri wameamua kuwa wanasiasa kwa kuwatumia Waumini.

Naishauri Serikali na Vyombo vyake iendelee kuwakazia tu Viongozi wa dini wa namna hii, sisi waumini halisi wa dini ambao kinachotupeleka Misikitini na Makanisani ni Ibada na maombi tutaelewa mbivu na mbichi.

Masuala ya Siasa yakafanywe huko kwenye maeneo ya Siasa yaliyotengwa, siyo Makanisani au Misikitini.
 
Wiki hii watu wametokwa na povu sana kutokana na matukio mbalimbali yalioashiria mwanzo wa kuanza kutomaswa tomaswa kwa dini zao ambazo zilikuwa zimepewa hadhi maalum ya kuwa zisizogusika au 'untouchables' kwa muda mrefu.

Mzee wa Upako ni mmojawapo wa watu waliotokuwa na povu hilo hadi kufikia hatua ya kutoa vitisho mbalimbali kwa utawala ambao muda mrefu amekuwa swahiba wake wa karibu sana. Wapo waliotokwa na povu na kamata kamata zinazofanywa makinasani

Ni wakati sasa wa Serikali kujifunza na kuisogeza dini mbali kabisa na mambo yake.
Hakuna haja kila jambo la kiserikali linapofanyika likaunganishwa na mambo ya kidini. Hakuna haja ya kuwa na mabaraza ya kidini yenye muelekeo wa ushawishi wa kiserikali.Hakuna haja ya kubebana na viongozi wa kidini katika kila tukio la kiserikali.

Mambo ya kidini yakiwekwa mbali na serikali. Itakuwa na faida kubwa kwa serikali, viongozi wa dini na waumini wa dini kwa sababu wote watakuwa na uhuru mkubwa wa kutenda na kusimamia yale wanayoamini ni sahihi na yenye maslahi kwao.

Wenye macho yanayoona mbali wameona kuwa serikali inafanya uchokozi kama wana masikio na ufahamu wachukue hatua ya kujichunguza.
 
CCM wenyewe washagawanyika vipande vitatu kwa sasa....CCM ya kina nape .... CCM ya mwendazake na hii mpya ya huyu maza.


Sasa sijajua ni CCM ipi inaruhusu askari na mabuti yao machafu kuingia makanisani kukanyaga madhabahu ya kikrito (kunajisi ibada) na kukamata waumini eti kisa tu wamevaa tisheti ya katiba mpya.

Ni ka ushamba kengine kapya ka kijinga.
 
Huna akili kumbe kila anesema kitu tofauti na unachokitaka ni bavicha
Wewe popoma mbona ulisema Mimi ccm sija kumaindi,nilijua tu kwakua bichwa yako no mzigo kwa mwili utamaindi
 
Nasisi tusichanganye siasa na dini,haikua na ulazima wa kuvaa gwanda za chama na kuingia kanisani kwa kisingizio cha maombi.
Tusome alama za nyakati
Sare za Chadema zinaeleweka vizuri ni yale magwanda ya mgambo na zile Tshirt zao zenye rangi za chama chao

Huyo askofu naye aliruhusuje watu waliovaa nguo za chama kugeuza kanisa kikao cha chama waliingiaje kanisani na nguo za vyama vyao? yaani polisi wana ufahamu mkubwa kwenye hilo swala kuliko yeye Askofu .Very sad
Nyie wote wawili mmechemka hatari....

Kwani "nguo za chama cha siasa" zikoje na utawezaje kuzitambua?

Zina uhusiano gani na imani ya mtu? Si sawa tu na aliyevaa jezi ya Taifa Stars au Arsenal au Simba SC na kwenda kusali...?

Kama imefikia hatua ya serikali au watawala kuogopa hadi mavazi yanayofanana na sare za chama fulani, basi hiyo ni hatari kwelikweli....!!!
 
Wewe popoma mbona ulisema Mimi ccm sija kumaindi,nilijua tu kwakua bichwa yako no mzigo kwa mwili utamaindi
Ukibishana na mpumbavu utaonekana wote ni wapumbavu. Ngoja nikae kimya tu maana umekoswa hoja
 
Hoja yako haina mashiko. Tangu lini serikali ilianza kuwapangia watu nguo za kuvaa? Mbona mara nyingi tu unakuta akina mama na wabibi wamevaa kanga, vitenge na vilemba vya ccm kwenye ibada makanisani! Lakini hakuna aliye lalamikia?

Nongwa wakivaa chadema! Halafu Makanisa yalitoa malalamiko yoyote yale serikalini? Au ni kiherehere tu cha policcm kutaka kuonekana kwa mabosi wao wa ccm!
Nadhani ni sahihi kuwa kuvaa nguo zenye alama ya chama si hoja, ma bibi zetu kijijini wana vilemba vya sisiem na wazee fulana hizo.
Hoja ni kuvaa na kwenda kuanzisha mambo ya siasa kanisani.
Haya maombi ya FREE MBOWE ni siasa.

Kama lengo ni kuombea watu hatuombi kwa kuwabagua watu, watu wa Mungu huombea mema Wema na Waovu.

Ukiona mtu anaomba mwingine apatwe na mabaya jua hapo HAKUNA DINI.

Kama kuna kikundi kimejipanga kama PRAYER WARRIORS basi watenge tena siku ya FREEE SABAYA

Siku ya BLESS CHADEMA
Siku ya BLESS CUF
Bless SSH
Bless TL
Bless MWIGULU wa TOZO etc

Lingine watu wanaojifanya eti kazi yao ni KUIPATIA WARAKA SERKALI hawajatumwa .
Mpeni Kasisari yaliyo yake

Kama kulikuwa na serkali corrupt ni ya KIRUMI wakati wa YESU lkn hakuanzisha HARAKATI kuiondoa.
Ni ujinga kuwa kiongozi wa dini mwana siasa.
 
Back
Top Bottom