Serikali ya CCM na wahusika wote wanaohusika kuhujumu mradi wa SGR wafikishwe mahakamani

Serikali ya CCM na wahusika wote wanaohusika kuhujumu mradi wa SGR wafikishwe mahakamani

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
GbrxQ7DbwAEFmhS.jpg
GbrxQ7JbgAAcwxT.jpg


July 04, 2022 Rais Samia Suluhu Hassan alisema serikali ya CCM itanunua vichwa na mabehewa vilivyotumika (mtumba) na vyenye hali nzuri watavitengeneza.Mradi mkubwa wa thamani ya Sh16 trilioni kutumia mabehewa na vichwa (used), hii sasa ndiyo hujuma yenyewe. Hata hakuna ambaye anahujumu mradi.

HUJUMA kwa SGR ni kununua madude yaliyotumika wakati wa ‘Escape from Sobibor’ mwaka 1943. Unatia nakshi. Unanunua mabehewa na vichwa used.Kuendesha mradi wenye thamani ya trilioni 16 kwa treni ambayo siyo high performance locomotive na haina Auxiliary Power Unit (APU) hii ndiyo HUJUMA.Dunia sasa inatengeneza sera za viwanda na kuzuia uagizaji wa vifaa vya mitumba (used), serikali ya CCM kupitia waziri wake wa fedha, ipo tofauti na Dunia.Mwigulu Nchemba na bunge la CCM wamepitisha sheria ya manunuzi kuhalalisha ununuzi wa mitumba (chakavu) katika ndege, meli, vichwa vya treni, mabehewa.Kwa mantiki hiyo, mradi wa SGR umehujumiwa na SERIKALI na siyo kama ambavyo tunataka kuaminishwa sasa. Msiwasingize kunguru au nyaya kukatwa.Sheria ya manunuzi ya umma 2011 s.66(2) inaruhusu Serikali kununua mitambo chakavu (used), lakini kwa DHARURA na waziri LAZIMA atengeneze kanuni!Sheria ya Manunuzi ya Umma inataka waziri kuunda kamati maalum ya ushauri kiufundi inayojumuisha watu wenye taaluma, maarifa, uzoefu masuala ya ununuzi. Tufahamishwe kundi lililompa ushauri waziri wa uchukuzi kununua mabehewa na vichwa vya treni vya MTUMBA kwa DHARURA. Hao ndiyo WAHUJUMU.NB; Kila mwaka Serikali ya CCM inatumia Sh558 bilioni kununua magari mapya (VX V8) ‘shangingi’. Vitu vipya kwa watawala, vyuma chakavu kwa walipa kodi?
 
Ni bora kwenda taratibu mkifanya vitu bora na vya uhakika wa kudumu kuliko kufanya vitu vingi kwa harakaharaka vya hovyo na kiwango duni visivyodumu ktk matumizi...!

Utatumia pesa nyingi kujenga miundombinu ya njia ya reli (SGR) halafu halafu unanunua gari chakavu iliyokwisha kutumiwa na wengine kupita ktk reli hiyo..?

Laana ya Nuhu kwa Hamu ndiyo inalisumbua bara la Afrika na Waafrika....

Watu (viongozi wa serikali) wanatumia sheria mbovu walizopitisha kupitia Bunge kuibia na kuifisadi nchi na kuacha wananchi wengi wakiteseka kwa kukosa huduma hizo ambazo fedha yake ilishapatikana na kuibwa na kufanya mradi lakini kwa viwango vya chini na mingi haikamiliki na mingine kutelekezwa....

Sekta ya ujenzi na usafirishaji kwa ujumla hali ni mbaya mno. Ndiyo sekta iliyoathirika zaidi...

Miradi ya barabara nyingi nchini kila sehemu imetelekezwa na kidogo inafanyika, basi inafanyika ktik viwango duni...

Mfano huku kwetu kuna mkandarasi anajenga barabara. Katika eneo (kilometa) alizopita na kuzikamilisha na kuanza kutumika, hata mwezi haujaisha barabara inabomoka na hakuna kiongozi anayejali wala kuwajibika..!

Haya ndiyo madhara ya RUSHWA na UFISADI...
 
Hakuna anaye hujumu SGR,tuna wakuu wa taasisi wasio na sifa na vigezo kuwa katika ofisi za umma.
"60% watumishi waliopo serikalini hawana uwezo"Prof Asad
 
Ni bora kwenda taratibu mkifanya vitu bora na vya uhakika wa kudumu kuliko kufanya vitu vingi kwa harakaharaka vya hovyo na kiwango duni visivyodumu ktk matumizi...!

Utatumia pesa nyingi kujenga miundombinu ya njia ya reli (SGR) halafu halafu unanunua gari chakavu iliyokwisha kutumiwa na wengine kupita ktk reli hiyo..?

Laana ya Nuhu kwa Hamu ndiyo inalisumbua bara la Afrika na Waafrika....

Watu (viongozi wa serikali) wanatumia sheria mbovu walizopitisha kupitia Bunge kuibia na kuifisadi nchi na kuacha wananchi wengi wakiteseka kwa kukosa huduma hizo ambazo fedha yake ilishapatikana na kuibwa na kufanya mradi lakini kwa viwango vya chini na mingi haikamiliki na mingine kutelekezwa....

Sekta ya ujenzi na usafirishaji kwa ujumla hali ni mbaya mno. Ndiyo sekta iliyoathirika zaidi...

Miradi ya barabara nyingi nchini kila sehemu imetelekezwa na kidogo inafanyika, basi inafanyika ktik viwango duni...

Mfano huku kwetu kuna mkandarasi anajenga barabara. Katika eneo (kilometa) alizopita na kuzikamilisha na kuanza kutumika, hata mwezi haujaisha barabara inabomoka na hakuna kiongozi anayejali wala kuwajibika..!

Haya ndiyo madhara ya RUSHWA na UFISADI...
Inasikitisha sana, Mbaya zaidi wapigaji tutawaona baada ya miaka kadhaa wakitamba na majumba na magari ya kifahari kama kina Lugumi
 
Hakuna anaye hujumu SGR,tuna wakuu wa taasisi wasio na sifa na vigezo kuwa katika ofisi za umma.
"60% watumishi waliopo serikalini hawana uwezo"Prof Asad
Kadogosa anapaswa kuwajibika, Reli kiwango cha SGR alafu mabehewa ubora wa miaka ya 1970's. Aibu mpaka majirani zetu wakenya wanatucheka
 
Kadogosa anapaswa kuwajibika, Reli kiwango cha SGR alafu mabehewa ubora wa miaka ya 1970's. Aibu mpaka majirani zetu wakenya wanatucheka
Shida sio Kadogosa,bali aliye mpa hiyo nafasi ni taswira yake mwenyewe,hivyo hayo ni matawi tu, kwenye shina ndo kwenye tatizo lenyewe.
 
Hii nchi Kwa nini?
Kwa nini? Hajitokezi hata diktet@ mwenye akili atakayetawala kimabavu.
Kwa lengo la kuimarisha nchi.
Dict*ta mzalendo Ambaye atakubali majina mabaya akubali kuitwa nyang'au aisaidie nchi Tajiri tz.
Aidondoshe demokrasia Tusiwe na vyama . Ipandwe Misingi ya Umoja.

Mshika mbili moja Humponyoka.

Kiongozi awaze Maendeleo ya nchi Kiongozi awaze Maendeleo ya chama chake,
Bado na yeye anajipenda.
Bora uje diktet@ uipende nchi
Ubadilishe Mfumo wa uongozi Mfumo wa wazungu udondoke ugenini
Welcome 🙏 diktet@ Welcome 🙏 diktet@ ufanye kazi yako
 
Wachawi wamo humo humo ndani ya CCM - wajikamate wenyewe.
Kwa mfano mimi kapuku hata sehemu ya kukatia huo waya ntaijuaje? afu nikitaka ntapata faida gani?
 
Hii nchi Kwa nini?
Kwa nini? Hajitokezi hata diktet@ mwenye akili atakayetawala kimabavu.
Kwa lengo la kuimarisha nchi.
Dict*ta mzalendo Ambaye atakubali majina mabaya akubali kuitwa nyang'au aisaidie nchi Tajiri tz.
Aidondoshe demokrasia Tusiwe na vyama . Ipandwe Misingi ya Umoja.

Mshika mbili moja Humponyoka.

Kiongozi awaze Maendeleo ya nchi Kiongozi awaze Maendeleo ya chama chake,
Bado na yeye anajipenda.
Bora uje diktet@ uipende nchi
Ubadilishe Mfumo wa uongozi Mfumo wa wazungu udondoke ugenini
Welcome 🙏 diktet@ Welcome 🙏 diktet@ ufanye kazi yako
Benevolent Dictator anahitajika kuinusuru hii nchi, aidha atoke jeshini au aibuke kutoka chamani kama Magufuli au Jeshi lichukue nchi na kufanya safisha kwa miaka mitano.
 
Wahujumu uchumi ni hao walionunua hayo madude used inabidi wawajibishwe
 
Benevolent Dictator anahitajika kuinusuru hii nchi, aidha atoke jeshini au aibuke kutoka chamani kama Magufuli au Jeshi lichukue nchi na kufanya safisha kwa miaka mitano.
Atatokea Naamini ipo siku yaja.
Na Misingi imara ndipo itakapoundwa.
Sauti za wanyonge zitasikika.
Dictat*r Naamini atatoka j*shin
 
Back
Top Bottom