Serikali ya Iran yafunga kiwanda chake cha kutengeneza magari kilichojengwa Syria miaka 20 iliyopita, sababu za kiuchumi na mahusiano mabaya zatajwa

Iran bila kutafuta njia ya kujirudi ili kuachana na vitendo vya kufadhili magenge ya kigaidi kamwe wataendelea kukumbana na vikwazo na watazidi kuumia zaidi ya wanavyoumia sasa.
Nyinyi msio fadhili ugaidi mbona kila kukicha mambo yanazidi kuwa magumu mara 100 ya Iran?
Hivi kwa akili yako ndogo unadhani Iran anafadhili haya makundi kwa ajili ya kujifurahisha tu hana masilahi nayo?
 
Sorry tu kukwambia habadili sera kwa ajili ya watu wachache, kwa ajili ya mfumo wa uchumi wa dunia ulivyo. Brics wanatumia blue print zile zile just at low cost, hakuna tofauti
Cha msingi Iran akipata wateja wa mafuta yake na gesi na akajipanga vizuri kwenye delivery hapo anaweza kupiga hela ndefu na kutajirika, na sasa anao wapo China, Venezuela na North Korea Pakistan. Na bado Mzunguko wa magendo unknown wa IRGC nadhani atavuka tuu kipindi hiki kigumu
 
Kwanini unapinga

Naomba sababu mbili tatu

Toyota mbona kawekeza south Africa?
Toyota ni nchi au mtu ? tumia akil mkuu , ingekuwa ni kiwanda cha muiran ingekuwa sw ila ishu kinamilikiwa na serikali ya iran
 
Na Ujerumani ambapo viwanda vinafungwa na penyewe inafuata sela kama za Iran?
Alafu Iran imefunga baada ya kukosa faida baada ya uchumi wa Siriya kuanguka kwa sababu ya vita.
Hayo mengine ni yako.
hujui kua gharama za uendeshaj viwanda kwa ulaya zipo juu ?
 
Utengenezaji magari sio lelemama ukiwatoa Toyota kwa soko la sehemu nyingi na China aliyetapakaa kila mahali hata Ujerumani sasa hivi ana panic kwa sales kushuka mfululizo..., Muingereza ndio alishafunga viwanda vyote na gari zake zote kuuza....

Na bila kumpiga China tariff za kufa mtu Europe wangefunga viwanda vyote au kumualika mchina ajenge viwanda kwao..... Na kama Iran atajiunga BRICS the future of Europe ni ya kusikitisha sana..... Sababu kuna nchi za NATO lukuki zinapenda kujiunga BRICS
 
Toyota ndio the best seller, is No 1 worldwide for more than 20 years; unafananisha na gari za Iran ambazo hata hatujui ni aina gani?
Mkuu Iran sio watu wa kubahatisha.
Sawa gari zao hazijajulikana kwasababu ya vikwazo vya kiuchumi walivyowekewa.
Ila mind you Iran ingekua imeachiwa huru aisee watu wangepiga sana nduru.
Mfano mdogo tu,umeona hii reli yetu ya SGR?
Mie nina wazee TRC,walinipa fununu kuwa ilikua bado kidogo wajenge Iran,na Iran wako na teknolojia nzuri sana ya reli,ila ubahili wa 10% ukawafanya wakose tenda na kupewa mzabuni Yepi Merkezi.
Iran ni watu ambao huwa wakifanya kitu wanajizatiti na hawabahatishi.
USA na washirika wake kumuwekea vikwazo hawajakurupuka,wanajua uwezo wake mkuu.
Wewe fikiria taifa lina vikwazo takriban miaka 40+ ila ipo uchumi wa kati wa juu,imeendelea kiteknolojia sio tu ya silaha bali hata ya nuclear,madawa(waliunda chanjo yao ya corona),reli n.k n.k.
Jiulize wangekua huru kama Tanzania tu wangelikua wapi!??
Na hizo gari zinakuwa manufactured from scrap to a whole thing.
 
Hamna Saipa humo, hio ni Toyota Allion rebaged. Waache uhuni hao! Kumbe wanafanya mchezo wa kichina nao. Tazama hii gari na hio Saipa zina tofauti gani πŸ˜‚!?

View attachment 3155039
Mkuu kugeza model ni kawaida ila ukija kwenye engine na vifaa vingine wanaunda wenyewe.
Basi hata kama useme wana rebag bado sio kitu chepesi,siku hawa watu wakikaa na wakatulizana basi wataunda vikubwa zaidi ya hiko.
Ukizingatia unaambiwa nchi ina vikwazo vya uchumi tangu mwaka 79 aloooooh!
Unaweza ukajilaani kuzaliwa Tanzania.
Itizame Toyota supra Ile ni BMW Z tupu.
 
Hahahah BMW engine ndio imeharibu kwenye supra bora wangeunda engine mpya yenye power ila iwe yao Toyota
 
Hahahah BMW engine ndio imeharibu kwenye supra bora wangeunda engine mpya yenye power ila iwe yao Toyota
Imeharibu kivipi kaka!?
Kumbe Ile engine ya supra ni ya BMW?

Iran wanajitahidi aisee wana kampuni nyingine inaitwa Bahman,embu tizama chuma hiyo chini mkuu haikushawishi kweli kuinunua!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…