Serikali ya Kenya imepiga marufuku shule za bweni kwa ngazi ya msingi, sisi ndiyo kwanza tunakumbatia

Mbona zimejaa Tz, watapingana na serikali ya Kenya?
Sio kesi uzuri sasa tuko kwenye Eas African Community ukipiga marufuku bweni wewe nchi zingine zinaenendelea na bweni

Watoto wengi wa Kenya chekechea na Msingi wazazi watawapeleka Uganda ambako huo ujinga haujafanyika

Na hata Tanzania wakiiga huo ujinga wazazi watapeleka watoto kusoma Uganda shule za bweni kuanzia chekechea hadi primary na ada yao nafuu sana kuliko shuke za bweni za Tanzania au Kenya

Na mzazi huwezi mzuia asipeleke mwanae huko baki na mishule yako ya day sio kesi

Mzazi ndie mwenye final decision kuhusu elimu ya mwanae asome day au boarding sio serikali

Mishule ya primary private Kenya itafungwa watoto watahamia Uganda case closed hasara kwa wakenya owners wa hizo shule na hasara kwa Kenya Revenue Authoriy itapoteza mapato

Kuna mambo hayahitaji ubabe kuwa mimi nimesema hasa yahusuyo uwekekezaji uwe wa shule za bweni etc

Useme wewe kama nani ulizaa huyo mtoto ? Kunataka dialogue best ways kuamua sio ohhh serikali imesema

Serikali sio Mungu wanawekwa kwa kura tu
 
Mimi kila siku nashinda nje ya Nchi wife kazini anachelewa kurudi home mtoto alelewe na dada wa kazi si bora kumtafutia shule nzuri kila wiki end mkiwepo mnaenda kumchukua mtoto hizo mambo mnaongea kana kwamba wote tupo nyumbani...
 

Afadhali kuna mtu mwenye busara na hekima katika uzi huu, hongera kwa ufafanuzi kuntu!
 

Kuna mijitu ya kuiponda nchi yetu Tanzania [emoji1241] kwenye kila jambo!
Kazi yao ni kusifia nchi nyingine tu walahi [emoji2959]
Bloody fools [emoji35]
 
Wewe huwa huna hoja, huna akili. Hopeless kabisa. Kwa hiyo unataka mtoto wa miaka mitano-kumi aende bweni? Majukumu yako kama mzazi unamuachia nani?

Watu kama hampo tayari kuzaa ni heri muache.
Watoto wa Uncle yangu wamesoma boarding tangu wakiwa na 8yrs na leo hii wapo vizuri sana both kimaadili na hata kimaisha.Nadhani ni busara kila mtu achague parenting ya watoto wake.Tusifike hatua ya kupangiana parenting ya mtoto.Kila mtu afanye kile anachoona ni bora kwa future ya uzao wake.Unaeona si sawa mtoto kuwa boarding upo sahihi kabisa lakini pia aliyepeleka mtoto wake boarding pia yupo sahihi.
 
Strong point mkuu
 
Mimi nimehamisha mtoto shule sababu ya kulazimishana bweni darasa la nne. Ukikataa unapewa adhabu ya kumpeleka mapema na kumchukua jioni sababu ratiba inapishana na school bus! Hii inafanywa makusudi ili ushindwe ulipe gharama za bweni!!

Huko Bweni malezi mabovu, ufuatiliaji wa maisha ya watoto ni hovyo, kuna watoto wanatoka familia zimeoza kimalezi wanakuharibia mtoto! Bora mtoto akiwa sekondari anakuwa na uwezo wa maamuzi!

Kijana wangu wa kiume niliruhusu akae bweni miezi mitatu nikamtoa nikawaambia walimu mwanangu hata feli darasa la nne sababu hakukaa bweni! Hii ni baada ya kufatilia malezi ya mabovu huko! Mtoto anakusimulia uchafu wa wenzake unajiuliza hawa watoto 7 -9 yrs how wawe na lugha chafu, matendo machafu na matron hajui?

Hapa Tanzania bado hatujaamua kulinda kizazi kijacho kimalezi! Maadili kuanzia shule inapaswa kuwa mjadala wa Taifa.
 
Hiyo sheria ni kwa shule zipi za Serikali au private?
Kama inahusisha private schools ni hopeless decision

Mambo mengine washirikishwe wazazi kuamua kipi kiwe kipi sio kukaa ofisini tu na kuamua bila kushirikisha wazazi
We hidaya ni mpumbavu, kupeleka mtoto bweni ni upumbavu

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
We hidaya ni mpumbavu, kupeleka mtoto bweni ni upumbavu

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Upumbavu kwenu ndio.maana kwenu maskini watupu

Watoto wote wa Dewji akiwemo bilionea Mo Dewji alisoma Bweni Arusha kuanzia chekechea na Primary zote kasoma bweni Baba yake akiwa milionea

Sasa hivi Mo Dewji ni bilionea wewe una nini maskini mkubwa umejaa umaskini hadi kwenye nani hii na wanao

Una nini cha kuonyesha na hizo day school zako ulisoma na kusomesha wanao zaidi ya umaskini uliojaa kunguni kila eneo? Lofa mkubwa wewe
 
Uvivu wa kulea na hii inasababishwa na wanawake wasiojua nafasi zao kwenye malezi. Madanga yaliyobahatisha ndoa
Uvivu kawaida wagunduzi wengi walikuwa wavivu mfano anaona kwa nini nitembee kwa miguu nachoka anagudua baiskeli kwa nini nilime kwa jembe la mkono kuanzia asubuhi hadi jioni anagundua treats

Kama mvivu kulea kwa nini usipeleke mtoto Bweni kwa waliosomea malezi ya watoto wakufanyie kazi hiyo kwa malipo?

Hata akiwa day mzazi ukiwa na kazi lszima utafute house girl akulelee mtoto kwa malipo

Kwani mama na baba mkiwa wafanyakazi mnakuwa na muda wa kulea huyo mtoto full time zaidi ya kumbwagia house girl? Nyie mnashinda huko kitafuta riziki mwaweza hata rudi mtoto kalala na asubuhi mnatimka mtoto hata hajaamka mbio kazini mnaachia housegirl

Wewe na mkro kama wafanyakazi hata wafanyabiashara mbali na nyumbani mna muda gani wa kulea mtoto?

Si heri mtu yule kakubali kukataa unafiki kuwa sina muda kulea mtoto akampeleka bweni kwa watu wamesomea kulea mtoto wenye qualification za child care na vyeti vya childhood education kuliko huyo house girl.wako unamwachia mtoto ambaye hajayawahi attend hata semina ya siku moja ya kulea mtoto? Au ya childhood education
 
Sasa unaweza shindanisha ISM au St Constantine na hizi boarding zetu?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Serikali ya Kenya imeona mbali sana, hapa Tanzania kuna shule zinaweka hadi watoto wa darasa la pili boarding, sijui wazazi wanakwepa majukumu au wana mambo mengi lakini natamani serikali ya Tanzania ifanye maamuzi juu ya hili kuokoa vizazi vijavyo
 
Sasa unaweza shindanisha ISM au St Constantine na hizi boarding zetu?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Issue Kenya wamepiga marufuku shuke za bweni za chekechea na Primary bila kujali International or whatever ndio maana nasema wajinga .Private waziache

Serikali haina shule za bweni za chekechea na Primary ndio maana namuona Ruto ns serikali yake wajinga tu

Mambo ya private schools chekechea na Primary waachie wazazi waamue

Wazazi kibao Kenya husomesha watoto chekechea na Primary uingereza

Sema Ruto mwenyewe ni mzazi mshamba na bahili anaishi kijinga fulani hivi

Hebu fikiria pamoja na pesa zote alizonazo na mivyeo mikubwa kashika Kenya yenye pesa nyingi ikiwemo u makamu wa Raisi wanae wanasoma shule za Serikali cheap na zenye matatizo kibao Hasomeshi shule za private So stupidly Conservative

Anataka kila mzazi Kenya awe kama yeye mjinga mkubwa. Watoto wasome day kama wake na wadkme shule za Serikali ambazo huwa hazina bweni Ana roho mbaya

Anataka kila mzazi wanawe Kenya wawe kama wanawe
 
Msiwatukane Wakenya kwani mtakuta mnajitukana wenyewe kwa kukosa kuelewa. Swala la bweni kwa shule za msingi za serikali Tanzania ndo ya mwanzo kupiga marufuku kabla ya hao Kenya. Nakumbuka shule niliyosoma tulikuwa na wenzetu wanaishi bweni mpaka miaka ya 2005 au 2004 ndipo mabweni yakavunjwa yote kwa amri ya serikali
 
Serikali ya Kenya imeona mbali sana, hapa Tanzania kuna shule zinaweka hadi watoto wa darasa la pili boarding, sijui wazazi wanakwepa majukumu au wana mambo mengi lakini natamani serikali ya Tanzania ifanye maamuzi juu ya hili kuokoa vizazi vijavyo
Kila mzazi ahangaike na wanawe hangaika na wanao ya watoto wa wazazi wengine waachie wenyewe hasa linapokuja swala la kusoma kuwa wasome bweni au day

Hangaika na wanao wa wengine kwenye hilo waachie wenyewe

Kesha ukihangaika na mwanao ya wazazi wengine huo ni umbeya mtaani.koma
 
Mawazo yako yanafanana kabisa na yangu. Na ndiyo njia sahihi.
 
Mbona hadi sasa shule za private za chekechea na msingi za Bweni mbona zipo kibao

Na zina wanafunzi hadi muda huu tunaandika leo December

Unaongelea vitu hewa Hizo walivunja 2004 na 2005 labda za Serikali. Za Private hadi saa hii zipo

Wewe utakuwa mkenya hujui kilichoko Tanzania
 
Kama unajiona uko bize kiasi kwamba una majukumu mengi, hupaswi kuzaa kuja kumtesa mtoto mdogo kuishi na watu walifikia!! Madhara ya mtoto kulelelewa na watu baki moja wapo ni asilimia kubwa ya watoto hawa hukosa upendo kwa wazazi wao na kujikuta wanawapenda zaidi wale walio walea, nahapo itategemea kama hao wanao mlea ni kweli wanamapenzi ya dhati kwa mtoto!!

Uwezi kulielewa hili sasa hiv kama kijana, ila ukifika umri wa uzee ukiwa mpweke, unahitaji faraja ya watoto wako na mtoto hakuwahi kuwa na bond na wewe toka utotoni kama mzazi, utapiga simu sana akutembelee katu huto muona!! Zaidi atashauri na wewe upelekwe nyumba za wazee umpunguzie kero

Kama mzazi unawajibika moja kwamoja kwa mtoto au watoto wako!! Kama unajiona huna na fasi ya kuspend time na watoto wako usizae subiri siku ukiwa free zaaa!! Kuliko kuwa damp shule eti kisa unamajukumu mengi
 
Kama ni suala la ''Kenya kuwa soko la kimataifa la shule za msingi za boarding'' basi Ruto apongezwe sana sana. Anaonyesha kujali zaidi hatma ya watoto na siyo kuingiza fedha. I mean linapokuja suala la future ya watoto na kizazi kinachokuja, basi hakuna mbadala, hata ziwe ni fedha na mali nyingi kiasi gani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…