Nchi za ulaya mangaribi zinatumia western liberal model of development
Nchi za asia: south korea, Taiwan, Thailand, Singapore, na Malaysia zinatumia: developmental state model
US wanatumia command and market economic model
Sasa, naomba kuuliza kiungwana tu, Tanzania yetu na hasa serikali hii ya ccm inafuata model ipi kutuletea maendeleo ya kiuchumi?
Uchumi wa Tanzania ni ule wa "Market Economy" ambao wategemea mazao yanotokana na kilimo, madini machafu, gesi asilia, viwanda na utalii.
Hizi sekta hazifuati sera za uchumi bali wenye mitaji na waloshikilia njia kuu za uchumi.
Ni mfumo wa uchumi ulorithi mfumo uloitwa "command economy" ambao ulikuwa ni ule unopangwa na serikali kupitia sera ya ujamaa na kujitegemea ambapo serikali ndio mpangaji mkuu wa sera za uchumi wa nchi.
Lakini baada ya serikali ya awamu ya pili kufungua mianya ya biashara na kuwapa watanzania wenye uwezo nafasi ya kumiliki njia kuu za uchumi, nchi yetu imeenda na kufikia hapa tulipo tukiwa hatujielewi na hatufahamu ni uchuni upi tuufuatao.
Hata ukiulizwa utashindwa kusema ila itabidi useme Tanzania ya sasa ina uchumi mseto yaani "Mixed Economy" ambao ni kujifanya twashiklia sera za ujamaa na kujitegemea lakini ndani yake kuna uharibufu mkubwa ulofanywa dhidi ya uchumi wetu.
Ila uchumi halisi tulo nao ni ule wa soko yaani "Market Economy."
Soko ndilo latawala uchumi huku wenye kushikilia njia hizo kuu za uchumi wakidhibiti ama serikali au baaadhi ya viongozi.
Mfano ni kampuni ya satelite ya kimarekani ambayo imeshindwa kuanzisha huduma za mitandao nchini Tanzania kwa kisingizio cha kudaiwa iwe na ofisi Tanzania.
Lakini kiukweli ni kwamba kampuni za simu ambqzo ndozo zimeshikilia na kuhodhi soko la watumiaji wa simu za mikononi na mitandao hazitakubali kampuni ingine ije Tanzania jambo ambalo kwao ni tishio (threat) kwa wao kuendeleza biashara zao.
Mfano mwingine ni serikali kutokuwa na neno katika upangaji wa bei za bidhaa za biashara kama Kahawa, Korosho , Mbaazi na zingine na kuwaachia wafanyabiashara wawabinye wakulima kwa kulipa bei ndogo sana lakini huko nje kupata faida kubwa.