Serikali ya Tanzania yatoa msaada Uturuki

Serikali ya Tanzania yatoa msaada Uturuki

Nasemaje Tanzania inarudi katika medani za siasa za kimataifa,mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.Ahsanteni KWA comment zenu
 
Nimefarijika Kuona na sisi tumetoa msaada uturuki, angalau na sisi tunajua kutoa, angalau!
 
Wanabodi habari zenu!!

Moja KWA moja niende kwenye mjadala, kuna habari za uhakika kuwa sasa Tanzania imerejea rasmi katika nafasi yake kwenye uwanja wa kimataifa.

Na hii inachagizwa baada ya Rais SAMIA SULUHU Hassan kuridhia Msaada wa Kifedha kuwasaidia wananchi wa UTURUKI kutokana na tetemeko la ardhi lililowakumba.

Katika diplomasia,daima kuna mahusiano ya nchi na nchi katika ushirikiano kwenye nyanja mbalimbali.

Moja ya nyanja hizo ni katika maafa na vita on reciprocal basis.Uturuki imepata maafa na serikali imeamua kutoa Msaada.

Pamoja na kwamba inazo changamoto nyingi za ndani ikiwemo mfumuko wa bei ya bidhaa bado serikali imeona vyema kushirikiana na wenzetu katika nyakati ngumu.

Msaada wa zaidi ya bil 2 za kitanzania ni sehemu tu ya moyo wa upendo wa nchi yetu KWA waturuki.

Msemaji wa serikali ya Tanzania Gerson Msigwa amebainisha hayo.Jambo hili ni jema mbele za Tanzania,UTURUKI na mbele za Mungu.

Kwa hapo acha tuseme Rais wetu Dr SAMIA SULUHU Hassan ameupiga mwingi.

Nasemaje mnyonge mnyonge Iakini haki yake mpeni.

Mungu ibariki Tanzania na Mungu ibariki UTURUKI

Nawasilisha
Nchi ipo na makuta mingi kila goli milioni 5 wacha tuwape msaada tu!
 
Tanzania karibia wote ni maskini.

Ukiangalia orodha ya matajiri wote ni Raia wa nje.

Hakuna mzawa.

Sasa kama spidi ndio hii ya kumwaga tu mahela kila mahali halafu baadae tunakopa kujengea vyoo hiyo sio sawa.
Gori moja m 5, hii ndio tanga na nyika.
 
Hapana.
Hawa wasingejua hali yetu ya umaskini, ila ninayo hakika wanajua hali yetu ya upumbavu wa nchi yenye neema kubwa kabisa kuwa na viongozi wasiojuwa kuwaongoza wananchi wao wautumie utajiri wao mkubwa kuondoa umaskini wa kutupwa.

Wanajuwa vizuri sana, tulivyo na viongozi wanaofuja mali za wananchi.

Kwa hiyo, wao kupewa dola milioni moja haiwastuwi hata kidogo, kwani wanajua vilevile, hata wakiikataa hela hiyo itaishia kwenye kufujwa tu haitafanya kazi yoyote ya maana kuwasaidia wananchi.

Nitakubaliana nawe, kama utashauri wachukue hiyo hela, halafu wao waje watujengee vsima vya maji huko vijijini kwa kuitumia hela hiyo hiyo.
Mimi naona tupeleke petition ubalozi wa uturuki ili wa diverge hiyo pesa kwenye visima na zahanati kule vijijini kwetu.
 
Mimi naona tupeleke petition ubalozi wa uturuki ili wa diverge hiyo pesa kwenye visima na zahanati kule vijijini kwetu.
Mkuu, huu ni mwanzo mzuri wa mchango wa mawazo.

Ingetokea jambo kama hili unalopendekeza hapa, na tukawa na mwendelezo mzuri, hasa na hizo Balozi kubwa kubwa zilizopo hapa nchini, sina shaka patakuwepo na matokei chanya.

Kiongozi yeyote akifuja pesa za misaada wanazotoa hawa wanaoitwa 'partners' wa maendeleo, tukashika bango kwenda kwenye ofisi zao na 'petition' zetu, najuwa patakuwepo na msisimko.

Lakini tatizo kubwa ni moja tu. Nchi yetu hatuna watu wa namna hiyo.

Hao NGOs wenyewe ambao wangekuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi, ndio wafaidika wakuu katika kushiriki maovu haya!

Sasa tutaanzia wapi na 'petition'!
 

Tanzania yatoa msaada wa Dola za Marekani 1,000,000 kwa Uturuki kufuatia madhara ambayo nchi hiyo inepata kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea mwezi Februari mwaka huu.

Hii ni mara ya pili Tanzania kufanya hivyo baada ya majuzi kuwasaidia marafiki zetu wa Malawi [emoji1156] waliokumbwa na Kimbunga kilichosababisha maafa.

Tanzania inarejea enzi za Mwalimu Nyerere ilipokuwa mstari wa mbele kulikomboa Bara la Afrika.
Mama yangu akiwa na pesa utamjua tu huwa hajifichi watoto huwa tunatumwa sana dukani.. ila sikiisha makasiriko bila sababu mtajua hujui..
 
IMG-20241118-WA0010.jpg


2024 hii, sad.
 
Back
Top Bottom