Serikali ya Tanzania yazuia ndege kutoka shirika la Kenya Airways kutua Dar, Kilimanjaro na Zanzibar

Nakubaliana na wewe...Uhuru lazima aje apige magoti hapa na siyo goti moja...hakuna kupiga simu...tutawatimua wakenya wore...hatua inayofuatia ni kufunga mpaka...nyang'au mpaka aombe suluhu
 
Mimi nafikiri sasa wewe tatizo lako na serikali ya tanzania ni personal zaidi kuliko huu mjadala uliopo.

Sijui kama wanaokujibu wamelielewa hilo au nao hawana kazi ya kufanya!!!!
Nobody is paying me for proposing anything...

Thats not my job....tumeajiri watu kufanya that,and they dont do their job!

In October we will fire them all!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]sawa nimekuelewa wewe mtu wa aina gani.. wakewale.. crying wolf!! Okay brother jifurahishe
 
Mkuu huyo jamaa nahisi ni mkenya ila km ni mbongo nahisi ile tumbua tumbua style ilimkumba mana anapinga kila kitu na leo ndo nimezd kumuona mpuuzi eti anapinga GoT kufanya retaliation lkn hapingi walichofanya Wakenya.

Huwa nachukia sana watu dizain hii wasiokuwa fair kwny argument zao na wengi wao ni hasa washabiki wa siasa wawe ccm au chadema wananiudhi sn watu hawa.
 
Kwamba wao watufungie na wao huku kwetu waendelee kuja tuu!? tena kwetu ndio nchi pekee EA wana safari nyingi kuliko nchi yeyote.

Ulitegemea majawabu ya aina gani!? hatuwezi kuwa walamba makalio kiasi hicho, suala kufungiwa mipaka tulienda kuzungumza nao leo tena wanarejea yaleyale,,

Hii ni Nchi mzee sio Kijiji.
Kila mtu ashinde mechi zake
 
Katika awamu ambayo itawatia adabu wakenya ni awamu hii ya Serikali ya tano.

Msicheze na Magufuli hana utani wala hamung'unyi maneno ukiweka ugoko anaweka jiwe.

Very soon Wakenya mtaufyata ni suala la muda tu
 
Hapo ni pale unakuja kuthibitisha kuwa malipo ni hapahapa duniani.
Hongera kwa serikali sikivu ya Tanzania upole ukizidi sana napo unashikwa masikio kila nyanja.
 
Wewe naomba unijibu hili hapa, na utakaponijibu mimi sitaendelea kujishughulisha na wewe kwa vyovyote utakavyojibu, hao hapo ni wamarekani wenye akili na maarifa mengi
 
Sikiliza, wao kama wsnaogopa Corona, tumewazuia kuja kuchukua Corona, tatizo liko wapi?. na nchi yoyote itakayofanya hivyo tutawasaidia wasipate Corona kwa njia hiyo.
Inashangaza. Kama tatizo ni korona, kwanini ndege zao zije huku kuchota korona!
 
Maduka ni mengi kuanzia ya dawa baridi mpaka ya bidhaa za kawaida, na ukienda mikoa ya kanda ya ziwa na kilimanjaro ndo soko kubwa la bidhaa hizo.
Unaongelea panadol wewe,kafanye tena utafiti utagundua kuwa kwa bidhaa zilizopo Ni zile zisizo na umuhimu zenye umuhimu Kama za maziwa haziji
 
Safi sana walituzoea sana hawa majirani.

Waendelee na Covid yao
 
Na hii Tanzania kuwa open, (though with restrictions) ndio inawaumiza sana hawa wakenya.
 
Hata Kikwete kupitia Samweli Sitta walishapunguza route za Kenya Airways baada ya kusumbua watu wetu wa utalii na hapo ndio wakashika adabu.

Hawa walituzoea sana, kwasasa ni kama system haitaki tena mazoea yaliyokwisha tugharimu sana.
Sema hawa Jirani zetu wapenda kuchukua hatua KiulayaUlaya wakati maisha wanaishi kibongobongo tu.
 
Huu upuuzi wenu ndio hatuutaki, hicho kijumuiya kisipokuwepo shida iko wapi? Nyang'au dawa yake ndio hiyo

Tatizo kubwa la Wakenya walio wengi wana an inflated view of their importance katika ukanda wetu wa Afrika Mashariki, tukitaka kukomesha jeuri zao ni kuiga mfano mzuri wa Mwl. Nyerere wakati akina Charles Njonjo na gege lake walipo vunja EAC na kupora asilimia 80% ya assets za EAC.

Mwl.Nyerere alitumia busara sana kuwakomesha vegeugeu hawa, alisema hivi: "Fungeni mipaka yetu ndio Wakenya watatambua umuhimu wa Tanzania katika maisha yao ya kila siku" na kweli, baada ya miezi michache kupita baada ya kutekeleza amri ya Mwl. Nyerere, Kenyan leadership went down on their knees begging Kambarage afungue mipaka - itakuwa vema tuki-emulate mbinu za Mwalimu lakini safari hii ziwe kali zaidi ili wasiwe wanatuchukulie poa hata kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…