Serikali ya Ujerumani kutoa kiasi cha Shilingi Bilioni 56 za Kitanzania zitakazotumika kwa ajili ya miradi ya mikubwa ya shughuli za Uhifadhi nchi

Je, huu ni msaada au mkopo? Tungekuwa tunapata ufafanuzi kidogo ili sisi walipa kodi tujue, endapo tumeongezewa deni jingine la kulipa au tumepewa bureee
 
Mzee Pascal je unaweza kuamua unapenda kudai nini? Unaanza warudishe walichopora, ila baada hutaji walichopora unjadili mifupa isiyo na thamani yoyote ya kifedha;
(mafuvu hukaa kwenye ghala za makumbusho yao, hakuna anayetaka kuziona; mifupa ya dinosauri inapendeza lakini jinsi ilivyo haileti faida, makumbusho yao yanahitaji pesa kutoka serikali kwa sababu kiingilio hakitoshi kulipa gharama; juzi tu walifanya ukarabati wa kiunzi kwa milioni nyingi...)
 
Cha msingi hizo ela zisije zikaingia kwenye mikono ya wajanja wachache.
 
Mkipewa hizo pesa zote msinyanyue tena mdomo kudai mabaki ya limjusi lenu
 
Enzi za Kayafa fedha kama hizi zingetengwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu ili kulazimisha CCM ishinde.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…