Serikali yaagiza Mtoto Charles Mathias arushwe Darasa kutoka Chekechea hadi Primary, Babu Tale aahidi kumlipia ada

Serikali yaagiza Mtoto Charles Mathias arushwe Darasa kutoka Chekechea hadi Primary, Babu Tale aahidi kumlipia ada

Serikali mkoani Morogoro imeagiza mtoto Charles Mathias mwenye umri wa miaka 6 arushwe darasa kutoka Chekechea hadi darasa la kwanza baada ya kuonyesha kipaji kikubwa kwenye somo la Hisabati.

Afisa tawala wa mkoa bwana Kobehelo amesema agizo hilo lianze kutekelezwa mara moja.

Naye mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Hamis Taletale ameahidi kugharamia elimu ya mtoto huyo hapo kijijini.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
Mwanangu ana miaka 6 na yupo darasa la pili
Baasi na yeye namuweka kundi moja na mtoto mwenye kipaji .
This world isn't fair. Nahisi alitakiwa kurushwa labda mpaka la tatu huko
 
Safi sana Mkuu....[emoji23][emoji23][emoji23]
Hapo ajaruka kuruka angetoka chekechea hadi la 2 na kuendelea ikiwa na maana karushwa drs la kwanza sasa kutoka chekechea kwenda la kwanza karuka darasa gani najaribu kuwaza.
 
ada gani tena si tulikubaliana elimu ni bure
Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Babu Tale agharamie nini tena wakati elimu ni bure?
Jaribu kuficha ujinga wako mkuu.
Kama aufuatilii habari kuwa kimyaa.
Babu tale alishasema tangu Awali atamsomesha St mary morogoro au nayo ni Bure?
 
Serikali mkoani Morogoro imeagiza mtoto Charles Mathias mwenye umri wa miaka 6 arushwe darasa kutoka Chekechea hadi darasa la kwanza baada ya kuonyesha kipaji kikubwa kwenye somo la Hisabati.

Afisa tawala wa mkoa bwana Kobehelo amesema agizo hilo lianze kutekelezwa mara moja.

Naye mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Hamis Taletale ameahidi kugharamia elimu ya mtoto huyo hapo kijijini.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
Tale nae aache sifa sasa ada gani kwa shule ile? Yeye akajenge madarasa tu
 
Mwanangu ana miaka 6 na yupo darasa la pili
Baasi na yeye namuweka kundi moja na mtoto mwenye kipaji .
This world isn't fair. Nahisi alitakiwa kurushwa labda mpaka la tatu huko
Hajui kusoma wala kuandika anapelekwa vipi darasa la tatu mkuu?
 
kweli usemavyo lkn ila Ubongo unachemka uyo dogo. Msasa Tu wa nguvu atajua vyote
Akisoma darasa kwanza mpaka mwisho naona ndiyo wataona maendeleo yake hapo wakimrusha itakuwa vizuri
 
Haaaahaaa hata me nawaza
Hapo ajaruka kuruka angetoka chekechea hadi la 2 na kuendelea ikiwa na maana karushwa drs la kwanza sasa kutoka chekechea kwenda la kwanza karuka darasa gani najaribu kuwaza.
 
Mwalimu wake wa darasa alinukuliwa akisema pamoja na dogo kuwa fiti hesabu ila hajui kuandika. Badala ya kumrusha rusha dogo na kumtoa mazingira aliyozoea ingekuwa busara kama hiyo hiyo shule iboreshwe. Anawezwa pelekwa shule nyingine mazingira tofauti akawa wa kawaida sana. Mazingira is everything!
 
Jaribu kuficha ujinga wako mkuu.
Kama aufuatilii habari kuwa kimyaa.
Babu tale alishasema tangu Awali atamsomesha St mary morogoro au nayo ni Bure?
Hapekekwi St Merry sasa...
 
Back
Top Bottom