Tatizo sio kurudishiwa fedha za viingilio tu, kuna gharama nyingine kubwa ambazo zinatakiwa kuangaliwa kwa kina, mfano kuna wapenzi wa soka waliokodisha magari kutoka mikoa mbalimbali kuja Dar es Salaam, vipi kuhusu yule shabiki aliyetembea kwa miguu toka Kigoma hadi Dar es Salaam, huyu nae wanamfikiriaje?
Kurudisha fedha za viingilio tu haitoshi, ila warudishe gharama nyingine kwa mashabiki watakaoweza kuthibitisha gharama walizoingia siku hiyo, kwa watu waliokodi gari kutoka mikoani, kuwarudishia viingilio tu hiyo naona si sawa.
Pia waliosababisha sintofahamu hii wachukuliwe hatua, ni bahati tu madhara makubwa hayakutokea, lakini suala hili likifumbiwa macho hatuwezi kujua nini kinaweza kutokea siku za usoni, hivyo hatua kali zichukuliwe na wahusika wenyewe wajiulize kama wanastahili nafasi hizo, wasisubiri kuambiwa wala tamko.