Serikali yabaini ubadhirifu mabilioni ya fedha za malipo ya korosho. Wakulima wasiolipwa watakiwa kujitokeza na CAG kuikagua bodi ya Korosho

Hivi hii Serikali imelaaniwa na nani? Mbona mambo yanaenda shaghala baghala, yaani msobwe msobwe tu.

Inasikitisha sana hii, sasa CAG anaenda kukagua Bodi ya Korosho ambayo Rais aliivunja mwaka jana? CAG anaenda kukagua Bodi ya korosho ambayo yenyewe haijahusika na malipo ya Korosho? waliolipa korosho si ni Bodi ya mazao Mchanganyiko na Benki ya Kilimo?

Ni ajabu sana hii, mnaleta maelezo meeengi na vijisababj kibao ili tu wakulima wa korosho wasilipwe stahiki zao, ni mwaka sasa mmeshindwa kuwalipa na mnakuja na hoja ya Ukaguzi kwa bodi ya Korosho.

Naamini katika miaka hii mitano jambo watajutia watoa maamuzi, ni suala la kuingilia kununua/kukopa korosho, hili litawatafuna sana kama ilivyo sura ya korosho.

Mngeanza kuwakagua wanajeshi ambao walibeba korosho kwanza, wao ndio walikuwa wanabeba gunia 50 wanafika njiani wanauza gunia 6 kwa laki mbili au moja. Korosho imeleta hasara kwa wananchi ambao kimsingi ndio tumenunua hizo korosho kwani tumekula hasara tumeuza chini TZS 2700/=
 
Hii awamu mtaipata tu kama mlizoe kula vya watu kisha mkanyamaziwa safarii hii mtaipata...ilizoeleka kula vya maskini kisha matapotezea kiana safari hii mtalalama sana...mara ufisadi awamu hii ni kuliko awamu zote pamoja na hayo wanaumbuka na kuumbuliwa na awamu hii hii..
 

Figisu ni kuwadhibu bodi kwa kulilia hela zao za mfuko maana wao ndio kimbelembele, mfuko ambao srekali umeupiga na CAG ni shahidi.
 
Kwa kweli nimeshutuka sana baada ya kumsikiliza Waziri wa kilimo ndugu Asunga kuwa malipo ya Korosho yalitofanywa na serikali pesa nyingi zimeibiwa.

Yaani pamoja na kufukuzwa kwa yule aliyekuwa mkurugenzi wa bodi ya korosho proffesa, pamoja na kuundwa kwa Kamati ya uhakiki wa malipo bado watu wamepigwa mabilioni ya pesa?

Nina imani kamati za kuhakiki walipwaji ziliundwa kwa kuingiza baadhi ya watumishi wa vitengo vyetu nyeti hivi imekuaje hayo mabilioni tena kuibiwa?

Nimejiuliza sana dhidi ya uhadilifu wa watumishinwa Bodi ya korosho, watumishi wa wizara ya kilimo idara za ushirika na wengine.

Mimi niliwahi kusema kuwa hizi idara zinastaili kufumuliwa ila kwa sbabu tunasemeaga kupitia jf mpka huwe pascally ndio utaheshimika.

Katika hili ningeomba kuwashirikisha jambo ndugu zangu kuwa kuna uwezekano mkubwa kauli nyingi za Mh Rais ambazo huwa zinaruhusu matumizi fulani ya pesa watu wanazitumia sana kupiga pesa.

Kama maamuzi magumu kama yale watu watu wameiba pesa hatua kali zichukuliwe dhidi ya walio hakiki, Kaimu warajisi wa mikoa, na maafisa ushirika wa eneo uska pasipo kusahau watumishi wa bodi ya korosho.
 
Wanajeshi hata suala la vyeti feki hawakuguswa hata hili itakuwa hivyo hivyo.
 
,hiyo 2017/2018 fedha zilipitia kwenye vyama vya ushirika then zikawekwa kwenye ac za wakulima,2018/2019 magufuli na jeshi lake hawakupitisha hela kwenye vyama vya ushirika,na kuna wakulima wengi hawajalipwa mpaka sasa lakini wanaosumbuliwa ni viongozi wa vyama vya ushirika
Ni mimi sijaukelewa au? Kawahiyo unamaanisha 2017/18 kilikua cha Mwinyi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…