Serikali yaelekeza Wanafunzi pia wasomee nyumbani kwa Januari 27 na 28, 2025

Serikali yaelekeza Wanafunzi pia wasomee nyumbani kwa Januari 27 na 28, 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema wanafunzi wa shule na vyuo pia wanatakiwa kusomea nyumbani kesho tarehe 27 na keshokutwa 28, Januari 2025, kutokana na kufungwa kwa barabara nyingi za jiji la Dar es Salaam kupisha Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi Barani Afrika.
IMG_2769.jpeg

Taarifa hiyo ni mwendelezo wa taarifa ya awali iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Moses Kusiluka kuhusu watumishi wa umma wa Mkoa wa Dar es Salaam kufanyia kazi nyumbani kwa siku hizo mbili.

Msigwa pia, amezitaka taasisi za sekta binafsi kufanya vivyo hivyo ili kuepuka usumbufu.
IMG_2768.jpeg
 
Screenshot 2025-01-26 193549.png
UFAFANUZI
Kufuatia taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi kuwa tarehe 27 na 28 Januari, 2025 Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Dar es Salaam wafanyie kazi nyumbani kutokana na barabara nyingi kufungwa ili kupisha Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi Barani Afrika, mnajulishwa kuwa Wanafunzi wa shule na vyuo pia mnapaswa kusomea nyumbani kwa siku hizo mbili.

Taasisi za sekta binafsi mnashauri kufanya vivyo hivyo ili kuepusha usumbufu ambao wafanyakazi na wanafunzi wanaweza kuupata.

Pia soma ~
Baadhi ya watumishi wa umma Dar kufanyia kazi nyumbani Januari 27 na 28, 2025 sababu ya Mkutano wa Nishati Afrika
 
Tusikuze mambo, siku 2 sio nyingi
Inafuatana na kazi unayofanya mkuu.
Siku mbili zinabadilisha mambo mengi sana.
Trump kadeport wahamiaji haramu zaidi ya 500 ndani ya siku mbili.
Mwalimu wa secondary anaweza kumaliza topic ndani ya siku mbili.
Mtihani wa darasa la saba hufanyika kwa siku mbili!
Usichukulie poa.
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema wanafunzi wa shule na vyuo pia wanatakiwa kusomea nyumbani kesho tarehe 27 na keshokutwa 28, Januari 2025, kutokana na kufungwa kwa barabara nyingi za jiji la Dar es Salaam kupisha Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi Barani Afrika.
View attachment 3214908
Taarifa hiyo ni mwendelezo wa taarifa ya awali iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Moses Kusiluka kuhusu watumishi wa umma wa Mkoa wa Dar es Salaam kufanyia kazi nyumbani kwa siku hizo mbili.

Msigwa pia, amezitaka taasisi za sekta binafsi kufanya vivyo hivyo ili kuepuka usumbufu.
View attachment 3214907
 

Attachments

  • IMG-20250126-WA0007.jpg
    IMG-20250126-WA0007.jpg
    39.9 KB · Views: 3
Sisi tuka jua waalimu wanabaki nyumbani wanafunzi wanaenda.

Ila kama hawakuwa wamejiandaa kabisa, huo ni mkutano wa siku mbili tena kwa nchi 20 na kadhaa, vipi huko Amerika kunafanyika mikutano ya dunia nzima? Vipi hapo Ethiopia inapofanyika mikutano ya umoja wa Afrika viongozi wote wa Afrika wanakutana hapo?
 
Sisi tuka jua waalimu wanabaki nyumbani wanafunzi wanaenda.

Ila kama hawakuwa wamejiandaa kabisa, huo ni mkutano wa siku mbili tena kwa nchi 20 na kadhaa, vipi huko Amerika kunafanyika mikutano ya dunia nzima? Vipi hapo Ethiopia inapofanyika mikutano ya umoja wa Afrika viongozi wote wa Afrika wanakutana hapo?
Aliyepeleka nchi Dodoma alikuwa na akili nyingi sana. Tumerudi kule Kule kwenye kudeki barabara
 
Hivi kuna mchambuzi anayeweza kufanya tathmini ya hela kiasi gani itapotea kwa kufunga hizo barabara vs manufaa ya huo ugeni ili viwekwe kwenye mzani au wachambuzo wetu ni Simba na Yanga tu🐼
 
Aliyepeleka nchi Dodoma alikuwa na akili nyingi sana. Tumerudi kule Kule kwenye kudeki barabara
Alikua sahihi sana.
Huu mji wa dar umejaa kwa kweli.

Jana kutoka mwenge kuja tegeta toka saa moja jioni hadi saa nne usiku ndio tunafika, wakati ni kipande cha dakika 30 kwa mwendo wa wastani
 
Back
Top Bottom