Serikali yafuta vijiji na vitongoji vyote vya wamasai wa Ngorongoro kupitia Amri ya tangazo la Serikali namba 673

Serikali yafuta vijiji na vitongoji vyote vya wamasai wa Ngorongoro kupitia Amri ya tangazo la Serikali namba 673

Tahadhari, :-

MAMBO MUHIMU YA UHIFADHI WA RASILIMALI ZA MBUGA ZETU ZILIZOPO KWENYE MIPANGO YA UHIFADHI NA URITHI WA DUNIA, TUSIGEUZE KUWA MASUALA YA KISIASA, UHIFADHI HAINA UDUGU NA SIASA! TUELEWE HILI.
this is among very visionary comments within this very esteemed platform JF...

thank you gentleman 👊💪
 
kwani hiyo section ilikua hakuna wakati wa wenye kiburi na jeuri walipokua mabosi wa TLS japo sifahamu inaeleza au kuhusu nini 🐒
Ilikuwepo lakini machawa wamekuwa hawaifanyii kazi.
Wale wachache waliyojaribu kuitumia waliminywa na madikteta wa CCM, mfano Fatuma Karume alifungiwa leseni yake ya uwakili mpaka leo na Tundu Lissu alipigwa risasi 16 na kuishia kulazwa Belgium kwa karibu mwaka!
 
kwani hiyo section ilikua hakuna wakati wa wenye kiburi na jeuri walipokua mabosi wa TLS japo sifahamu inaeleza au kuhusu nini 🐒
Kila zama na kitabu chake subiri Mwabukusi aifanyie kazi ndiyo utajua ilikuwepo au haikuwepo. Kumbuka Tundu Lissu na Fatuma Karume ni wahanga wa section hiyo na kwa sasa msitegemee kumdhuru Mwabukusi hamtabaki salama!
 
Kila zama na kitabu chake subiri Mwabukusi aifanyie kazi ndiyo utajua ilikuwepo au haikuwepo. Kumbuka Tundu Lissu na Fatuma Karume ni wahanga wa section hiyo na kwa sasa msitegemee kumdhuru Mwabukusi hamtabaki salama!
ni wahanga wa kiburi na jeuri yao usipotoshe tafadhali :pulpTRAVOLTA:
 
Serikali kupitia kifungu cha 30 cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Sura ya 287 kinachotoa ruhusa kwa mamlaka za Serikali kufanya mgawanyo wa Halmshauri za Wilaya;

Imetoa AMRI rasmi iliyotangazwa kwenye Gazeti la Serikali namba 673 la tarehe 02 Agosti, 2024; ili kufuta baadhi ya maeneo ya kiutawala kwenye mamlaka za Serikali za Mitaa hapa nchini kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa tarehe 27 Novemba, 2024.

Amri hii rasmi sasa inafuta Kata, Vijiji na Vitongoji katika Halmashauri za Wilaya zifuatazo; Ngorongoro, Bahi, Chemba, Kasulu, Kakonko, Hai na Rombo.

Katika Halmshauri ya Wilaya ya Ngorongoro pekee, kupitia AMRI hii, Serikali imezifuta Kata 11, Vijiji 25 na Vitongoji 96.

Garatwa,
Dar es Salaam, Tanzania.
20 Agosti, 2024.
View attachment 3074791
Lakini hii siyo amri ya 'KUFUTA' Vijiji na Vitongoji.
Ni amri ya Marekebisho ya Amri ya MGAWANYO.

Kuna mtu anaweza kuinterpret hiyo notice vizuri na nini implications yake?
 
Lakini hii siyo amri ya 'KUFUTA' Vijiji na Vitongoji.
Ni amri ya Marekebisho ya Amri ya MGAWANYO.

Kuna mtu anaweza kuinterpret hiyo notice vizuri na nini implications yake?
Kwa mujibu wa serikali amri hii inafuta kata, vijiji na vitongoji na ndiyo sababu wananchi katika maeneo hayo wamesitishiwa huduma za jamii kama ujenzi na ukarabati wa shule, zahanati, barabara na huduma zingine. Pia wamehamishiwa maeneo mengine kujiandikisha katika daftari la kupiga kura na pia kurekebisha au kuboresha taarifa zao katika daftari la kupiga kura.

TLS na wabobezi wengine wa sheria wamepinga hatua hiyo na kutumia kifungu hicho cha 30 wanasema hakimpi mamlaka waziri kufuta maeneo bali kurekebisha mipaka ya utawala. Kwa hiyo wanakwenda mahakamani kupinga amri hiyo.
 
Kwa mujibu wa serikali amri hii inafuta kata, vijiji na vitongoji na ndiyo sababu wananchi katika maeneo hayo wamesitishiwa huduma za jamii kama ujenzi na ukarabati wa shule, zahanati, barabara na huduma zingine. Pia wamehamishiwa maeneo mengine kujiandikisha katika daftari la kupiga kura na pia kurekebisha au kuboresha taarifa zao katika daftari la kupiga kura.

TLS na wabobezi wengine wa sheria wamepinga hatua hiyo na kutumia kifungu hicho cha 30 wanasema hakimpi mamlaka waziri kufuta maeneo bali kurekebisha mipaka ya utawala. Kwa hiyo wanakwenda mahakamani kupinga amri hiyo.
Asante sana
 
Hawa wamasai tusiwachukulie poa.

Wao wanasema waliruhusu watoto wao wahamie msomera lakini wao kamwe hawatohama pale hata iweje,
Tena aliyekua anaongea anasema wao wana akili eti wahamishwe kisa eti ujenzi wa mahoteli ya kitalii? Hapana rafiki.

Wamasai ni watu jasiri sana na hua hawana maneno na mtu ukiona hadi wao wanajua wanaonewa ujue kweli umewaonea vya kutosha.

Viongozi ogopeni wananchi wanaosema wako tayari kufa, yaani hao inabidi uwape haki yao mapema kabisa.
 
Back
Top Bottom