Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,509
- 3,756
Serikali kupitia kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesema kuwa kufuatia kusitishwa kwa lesini ya gazeti hilo, halitaruhusiwa kuchapishwa wala kusambazwa popote nchini au nje ya nchi
Serikali imebainisha kuwa uamuzi huo umetokana na kukithiri na kujirudia kwa makosa yanayokiuka sheria ya nchi na maadili ya uandishi wa habari na kuwa juhudi za kuwaonya na kuwaelekeza Wahariri wa gazeti hilo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa hazijazaa matunda
Taarifa ya Serikali inasema Mkurugenzi wa wa Idara ya Habari, amefuta leseni ya gazeti hilo ikiwa ni baada ya kulionya kwa zaidi ya mara 10 huku gazeti lenyewe likilazimika kuomba radhi mara mbili kwa uvunjifu wa maadili ya Kitaaluma na Sheria za nchi ikiwemo kuchapisha habari za uongo, uchochozi na uzandiki
Aidha, Serikali imesema kwa mujibu wa Sheria Wachapishaji wa gazeti hilo wanayo fursa ya kuomba tena leseni kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari ili kuruhusiwa kurejea tena kuchapisha na kusambaza watakapoona wamejitafakari na kuwa tayari kufuata taratibu
Soma pia > Gazeti la Tanzania Daima latoka kifungoni baada ya kufungiwa kwa siku 90
Serikali imebainisha kuwa uamuzi huo umetokana na kukithiri na kujirudia kwa makosa yanayokiuka sheria ya nchi na maadili ya uandishi wa habari na kuwa juhudi za kuwaonya na kuwaelekeza Wahariri wa gazeti hilo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa hazijazaa matunda
Taarifa ya Serikali inasema Mkurugenzi wa wa Idara ya Habari, amefuta leseni ya gazeti hilo ikiwa ni baada ya kulionya kwa zaidi ya mara 10 huku gazeti lenyewe likilazimika kuomba radhi mara mbili kwa uvunjifu wa maadili ya Kitaaluma na Sheria za nchi ikiwemo kuchapisha habari za uongo, uchochozi na uzandiki
Aidha, Serikali imesema kwa mujibu wa Sheria Wachapishaji wa gazeti hilo wanayo fursa ya kuomba tena leseni kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari ili kuruhusiwa kurejea tena kuchapisha na kusambaza watakapoona wamejitafakari na kuwa tayari kufuata taratibu
Soma pia > Gazeti la Tanzania Daima latoka kifungoni baada ya kufungiwa kwa siku 90