Serikali yatimua wanafunzi UDSM


Rev umenipa kitu kinachoitwa men talk. Wanafunzi magenster ndio wanaochangia migomo ya kishenzi shenzi pale mlimani. Nilishasema kwamba Uhandisi shule yake ni nzito, mitihani ikikaribia na ujasoma nondo zako za static au thermo, unachofanya ni kuanzisha mgomo, mnapelekwa home, unachukua muda ule kusoma then unarudi ukiwa fresh and clean. Huo ndio mchezo.

Unagoma kisa maji? Wakati hapo hapo Ubungo kuna sehemu mabomba yamegeuzwa nguzo ya kucheza makida makida kwa watoto maana yalitoa maji wakati wa mzee mwinyi. Hatuna tabia ya kuanzisha mahojiano kuhusu kitu. Tunajali kugoma. I think it is about the time to clean the mess. Fukuza wote waliokuja kucheza wacha wanataka kusoma
 
NA NDIO MAANA NIKA KWAMBIA KUWA TATIZO SIO TATIZO..BALI TATIZO NI USUGU WA TATIZO!KWAMBA MIAKA NENDA RUDI NYIMBO NI ZILE ZILE NA HAKUNA JIPYA!HAYO NDIO HUPELEKEA CIVIL UNREST!WE NDO UNATAKA KUSPIN MAN!
 
Ama ile ya kasungura kama sikosei!
 


Nadhani Mkuu umeishi mno Marekani. hiyo kazi ambayo unasema hawa wanafunzi hawataki kuifanya iko wapi? Wanafunzi wengi marekani wanafanya kazi za uwaiter au waitress ili kujiongezea kipato. Unajua hao wahudumu wanalipwa ngapi bongo mbali na matzamo wa jamii kuhusu wote wanaofanya hizo kazi! Mimi wakati nasoma ilikuwa wakati wa likizo wanafunzi wa sekondari walikuwa wanaajiriwa tempo kwenye mashirika ya uma. Leo graduate lawyers na engineers wanakazi hata kupata kazi ya kibarua! last time i checked, Steers (McDonald yetu) hawaajiri wanafunzi!

Hiyo scientific calculator unayosema wajinunulie, unajua bei yake ni theluthi ngapi ya mshahara wa kima cha chini bongo? Na huko Marekani ni theluthi ngapi?

Aaah! Mikopo? unajua mbinde zinazotawala katika kupata hiyo mikopo? leo unasema waende wakakope? Wapi? Benki ipi?

Mara ya mwisho ulipanda ghorofa kumi na ndoo ya maji,Mkuu, ilikuwa lini? Mara ya mwisho umetumia choo cha shimo ukiwa Chuo Kikuu ni lini? Leo kweli unadiriki kusema kupanda ghorofa kumi kila siku ni great exercise? Na wale wenye ulemavu, wenye uja uzito nao utawaambia hivyo hivyo? Kwamba wajitahidi kupanda hizo ghorofa maana zitawajenga kiafya!

Kuna usemi, Mkuu, "the straw that broke the camel's back". Inawezekana sababu walizotoa kwenye hili ni inconsequential lakini ni hitimisho la mataizo ya muda mrefu. Mimi naamini huko marekani chuo kikuu ambacho hakina huduma ya maji ya hakika, lifti zimeota kutu kingeishafungwa na authorities. Kukosa maji katika jengo la ghorofa kumi ni public health hazard.

Wakina Mwabulambo waligoma kwenda JKT wakaitwa elitist kama wewe unavyotaka kuwaita hawa! Hakuna tofauti kati yao isipokuwa passage of time ndiyo inayotufanya tuone hivyo. unadhani wakina mwabulambo wangekubali hali iliyojiri sasa hivi? Thubutu! wakati wanasoma wao kila kitu kilikuwa bure na mess kulikuwa na waiters na menu na bado wakagoma!

Ni sis ambao tuko pembeni ambao tunatakiwa tu'get real' na kuacha kuimba nyimbo za kuwa washukuru upendeleo waliopata. tuwaangalie kama wananchi wengine na tuwatendee haki. Tusiwabeze.

Amandla!
 
Wakati tukiendelea mjadala napenda kuwafahamisha kuwa sakata hili limechukua sura mpya baada ya prof Maghembe kukubali ombi la Uongozi wa UDSM kutengua adhabu yake ya kuwafutia udahili baadhi ya wanafunzi. Pia polisi wamekubali kuifuta kesi iliyofunguliwa dhidi ya wanafunzi 38. Lakini nabaki najiuliza kwa nini UDSM ilikwenda kumuomba Maghembe abadilishe uamuazi wake? Ina maana maghembe alifikia uamuzi bila kushauriana na uongozi wa UDSM?
Lipo pia suala la idadi ya wanafunzi ambao walifutiwa udahili. hakuna aliyesema mpaka sasa idadi ya waliofutiwa udahili wala kutaja majina yao. Sasa sijui msamaha huu unawahusu wote au wale tu ambao walikuwa wamefunguliwa kesi?
 


Juu ya hayo, naamini hakuna mtu ambaye amezaliwa perfect na amezaliwa kuwa kiongozi, na hapa inaonyesha kama vile rais alimpa mukandala cheo kwa mtindo wa ushkaji, je ni mchakato gani unaofanywa ili kumpata kiongozi wa chuo? au rais anachagua jina kama vile anavyochagua mawaziri au wabunge wa kuteuliwa na rais?

Binafsi nahisi mkandala anaandamwa na matusi kwa vile yeye ni mwanaCCM au chuki binafsi kwa huyu bwana.

Hili la maji na umeme naona wanafunzi wamezidi, wana kiburi na majivuno ya kujiona wao ndio wanastahili kupata hizo huduma kuliko mtu mwingine yeyote yule.
 

Jamani jamboforums kuna watu wanafikiri. Yaani nimesoma hadi nikasisimkwa na akili. Inaonekana huyo Rev alikuwa anaongea tu bila kufikiria haya yote.
 

Wamepigiwa simu kutoka ndani na nje ya nchi na wakapata kibano cha uhakika hapa JF hadi wamechoka wenyewe.

Huwezi kuingilia uchaguzi huru wa wanafunzi, wanafunzi hao wakagoma, ukawafukuza chuo, wenzao wakaandamana, ukawapiga kwa mabomu, kisha ukakamata wenzao na kuwabambikia kesi za kuvuta bangi na madawa ya kulevya, halafu ukategemea kulala usingizi mnono usiku.

No way. Jamboforums imesema NO kwa ufisadi. Pongezi kwa wote walioshiriki.
 

Kama umezaliwa na kukulia mlimani, na kama umesoma mlimani na kisha unaandika english mbaya kiasi hiki basi kuna sababu ya kufuaatilia matokeo yako.

Ahhh umesema kuwa wazazi wako wanafundisha mlimani kwa hiyo inawezekana ulikuwa unapass kwa nguvuu ya wazazi wako ambao nao inabidi wachunguzwe walipataaje kazi hapo.

Kwani unalazimishwa kutumia kiingereza? Kama huwezi kingereza si utumie tu kiswahili kuliko kubaka lugha ya wenzako? Unadhani utamtisha mtu kwa kusema kuwa umezaliwa nakukulia mlimani? Point zako zinaonyesha vinginevyo.
 


Kukosekana maji katika jengo lenye ghorofa kumi si tu ni public hazard kiafya bali ni hatari hata pakitokea moto! Majengo yote marefu yanakuwa na mabomba yanayoitwa wet na dry risers ambayo zima moto wakija wanayatumia kukabiliana na moto. Magari ya zima moto hayabebi maji ya kutosha kuzima moto katika majengo kama haya hata siku moja. Kwa hiyo moto ukitokea na majengo yakiteteketea tutamlaumu nani?

Kuna wale wanaodai kuwa hao wanafunzi ni arrogant. On the contrary, nimekutana na walimu na wanafunzi kutoka ulaya ambao wanashangaa arrogance ya WAKUFUNZI! Wanashangaa jinsi wanafunzi wanavyowaogopa wakufunzi ambao wengi wao wamesoma nchi ambazo uhusiano kati ya mkufunzi na mwanafunzi wake ni wa kuheshimiana! Wanafunzi wetu wanatambulika kwa kuvumilia hali ngumu ambayo kama ingetokea kwa wenzetu si wao tu bali hata wazazi wao nao wangeandamana kudai majibu yenye uhakika!
 

Mkubwa hatupigani ngumi, we just arguing for the sake of our nation. Sasa nilisha kuuliza why are you supporting Migomo ya chuo? English or swahili has nothing to do na mabishano haya.

I think hakuna poit yoyote ya muhimu ya kushambulia wazazi at this poit. Wanafunzi kugoma kunachangia kukiweka kile chuo kwenye coma. So, the last thing i was expecting from you ni kuanzisha malumbano mengine ambayo yako irrelevant na topic.

Why wanafunzi wanagoma? That is where we started, so can we go back and continue from that point? Tatizo la watanzania ni kutafuta shelter pindi tukishindwa kubattle kwa point.
 
Hivi kuna uhusiano gain kati ya Mgomo wa Calculator na Mukandala? Hivi kwenyw mgomo wa Calcutaor VC si alikuwa Luhanga? Nijibuni ili niendelee kushusha mambo
 
Naomba Nipate Haya Majibu ya Maswali haya

1: Je Odwang Odor Hana class mates wenzake kutoka chuo hicho ca Uganda?

2: Kama wapo je wao wana matokeo rasmi?

3: Kama hawana imekuwaje Odwang amefukuzwa ili akalete vyeti?

4: Jr ni nani mwenye mamlaka ya kutangaza Tarehe ya uchaguzi DARUSO na ni nani
Ana mamlaka ya kuahirisha uchaguzi?

5: Kama class mates za Odwang kutoka Uganda wana vyeti, je anaweza kuvionesha ili
Tumuone Odwang ni Muongo

Kama Maswali hayo hayana majibu basi mimi nauita huo ni UFISADI sio wa pesa bali UFISADI mbaya kabisa wa FIKRA na UHURU wa MAWAZO
 
Mimi haya mambo ndiyo nisiyoyaelewa. Unaenda polisi kushitaki unaambiwa kamlete mbaya wako! Kama utawala una wasi wasi na vyeti vya huyu jamaa, kwa nini wasiwasiliane na hizo shule anazodai amepitia? Je huko Uganda hamna mamlaka inayosimamia elimu ambayo ingeweza kutoa majibu ya uhakika? Kama hamna mawasiliano, si kuna balozi wetu? Utawala wamefanya jitihada gani katika kuthibitisha kuwa hivyo vyeti alifoji? Kama walivikubali mwanzo na sasa machale yamewacheza basi the burden of proof ni kwao na si kwa mwanafunzi! Akivileta si bado watadai kuwa amefoji? Iko kazi kweli.
 


Mkuu
mbona mbona wengi tunakosea sana kuandika kiswahili mimi mmoja wao.
mbona hapo hatuulizi?? mtu akikosea kiingereza eti wanahoji usomi
nani alikuambia kiingereza ndio usomi????

Inamaana mtoto wa darasa la nne kutoka uingereza ni msomi kuliko waafrika wote ,maana anaongea lugha maridadi ya kiingereza ,grama bomba .
Ama nchi zisizotumia kiingereza si wasomi kwa maana kiingereza kwao ni tabu kama vile ujerumani,norway,japan,urusi,holland,poland,austria,uberigiji,italia,ureno n.k

Samahani kwa kuvamia mada yako naomba uniileweshe zaidi una maana gani haswa.
 

Kama unaaweza kuandika kiswahili vizuri ni bora ukatumia kiswahili maana unabaka lugha ya wenzio na kuiharibu hivi hapa jamboforums.

Tumia lugha unayoielewa vyema na utaeleweka la sivyo utaonekana kama mtu ambaye unavuruga english kimakosa ili usieleweke na baadaye uanze kulaumu watuu kuwa hawataki kukuelewa.
 

Hakuna aliyemlazimisha kutumia kingereza ambacho anakikosea hapa kwa level ya juu kabisa. Anaweza akatumia kiswahiili na akaeleweka vizuri zaidi na asitie kichefuchefu wale wasiojua kiswahili na wanaojaribu kusoma mabandiko ya kiingereza.
 
Hakuna aliyemlazimisha kutumia kingereza ambacho anakikosea hapa kwa level ya juu kabisa. Anaweza akatumia kiswahiili na akaeleweka vizuri zaidi na asitie kichefuchefu wale wasiojua kiswahili na wanaojaribu kusoma mabandiko ya kiingereza.

Mkuu
nashukuru pointi yako uliyosimamia nimeshaiona
 

I decide to hang my gloves. I can't keep argueing with you anymore. I think kubishana kwa point is something which doesn't exist in third world nations. Wish you goodluck mr. Kifimbo cheza. I close arguments with you official.
 
I think kubishana kwa point is something which doesn't exist in third world nations.

Haka hakajakaa vizuri, Mkuu! Yaani unatulaani Third Worlders wote?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…