Serikali yaunda Kamati kuchunguza chanzo cha moto Soko Kuu Kariakoo. Waziri Mkuu asema hatua zitachukuliwa moja kwa moja ikijulikana kuna mkono wa mtu

Na ameshafanya uchunguzi na kugundua ni hujuma!na wala sio electric fault au sababu nyingine,sasa nimeelewa why hatuhitaji idara ya forensic ndani ya idara zetu za kiusalaama
Hatari sana mkuu.
 
Hebu tuwekee ushahidi tuone hizo hujuma unazosema zimefanyika.
 
Wakati tukisubiri matokeo ya uchunguzi Kwa mtazamo wangu hasara itayopatikana ni kubwa.

Pia nishauri tuache waliopewa jukumu la uchunguzi walifanye.

Kuanza kuspeculate tunaharibu.
 
mama Samia anasukumwa kuwa mkatili!
Unapohujumu soko kuu nchini kama la kariakoo ni wazi unatenda tendo la kigaidi kwani mfumuko wa bei kariakoo ni mfumuko wa bei Tanzania.

iwapo ikithibitika kuna uhujumu lazima wahisika wachukuliwe hatua Kali
Wachina wanelitaka soko kwa muda mrefu bila mafanikio.

Kuna soko la Kisutu likaboreshwa kwa kujengwa la ghorofa...Sasa linahitaji wapangaji.

Machinga complex kuna ulazima wa kulitafutia wapangaji pia.
Soko kuu la Kariakoo likisimama kufanya kazi ni wazi hayo masoko mengine yatapata wateja na wapangaji pia... Na mchina atapata nafasi ya kulinyakua.

Je, tufanyeje ili Soko la kariakoo liache kufanya kazi kwa muda?
 
Serikali ya nini kuchunguza hapo, watamalizana na insurance company kama walikuwa nayo😁, can't believe soko kubwa kama hilo kukosa fire insurance, fukuza then prosecute management yote kama kweli no insurance, ajali za moto ni kawaida kitu ambacho si kawaida ni soko kama kariakoo kutokuwa na insurance
...fanya mfano hao
 
Majibu ya kamati ya uchunguzi,ukiwa tayari na wa kiuambia umma mni tag

Ova
 
Gaidi no 1 Mbowe ndio amelipua soko....wanahangaika nini ....si ndio akili zao mwisho hapo
 
Masoko yote makubwa huwa yanachomwa Ili kupisha ujenzi wa masoko ya kisasa au watu washalipa Sana bima hivyo utaka walipwe bima
 
Mpaka leo holaa

Nilishapoteza imani kwa huyu waziri mkuu, ni moja ya viongozi ambao siwaamini matamko yao.
Yaani alivodanganya ishu ya mwendazake macho makavu kabisa tena msikitini na yeye ni muislam.
 
Ok .

Kuna mwenye report ya hii tume [au kuna mahali imekuwa published ]

Walikuja na findings zipi ?
 
Hii kamati mbona kimya hatujapata mrejesho wowote!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…