Serikali yaunda Kamati kuchunguza chanzo cha moto Soko Kuu Kariakoo. Waziri Mkuu asema hatua zitachukuliwa moja kwa moja ikijulikana kuna mkono wa mtu

Serikali yaunda Kamati kuchunguza chanzo cha moto Soko Kuu Kariakoo. Waziri Mkuu asema hatua zitachukuliwa moja kwa moja ikijulikana kuna mkono wa mtu

Kuna yule Kamishna Mkuu wa Zimamoto aliwahi kutumbuliwa enzi za JPM kwa tuhuma za kusaini mkataba aghali wa vifaa vya Zimamoto saa hizi atakuwa anachekelea tumboni. Alidhalilishwa sana kama mnakumbuka japo kwa sasa nadhani ana kau- RC sijui wapi huko...
Usisahau hakuna njia inayopitika kirahisi around the market pamoja na kuwa na lami

Tumeachia machinga wakamate mamlaka

SoMo kubwa Sana hili
 
Hapo wamekosea kuunda kamati. Kawaida Fire wanapaswa wasubmit investigation report. Na wanapaswa waweke wazi fire inspection ya mwisho ilifanywa lini hapo kariakoo, na mapendekezo maana kwa layman pale kulikuwa na mambo mengi tu ya kurekebisha...

Kwenye sehemu za umma ambazo serikali ndio muwajikabi hizo sheria hazifuatwi, lakini taasisi za binafsi utakuta watu wa fire brigade wanashinda hapo kufanya ukaguzi.

Huu mchezo uko pia kwenye shule za private. Utakuta uhakiki kila siku, nenda shule za serikali sasa, unakuta wanafunzi zaidi ya 300+ wana matundu mawili ya choo na shule haifungwi!
 
Ule mkataba ulikuwa unaleta Dron hapo sokon ingefanyaje kazi? Lakini ata hivo huwezi kufanya mipango ya kusaini mkono wa takriban Trilion 1 huku baraza la waziri halijui chochote
Baraza lijue kwani panawahusu? Sasa ndiyo pameungua wanalipana posho kuchunguza hasara ambayo hata ikifahamika wafanyabiashara hawatalipwa fidia.
 
Kwa nini badala ya kamati vyombo tofauti visichunguze? Kwa nini lazima iwe ni KAMATI?
Kamati ni mjumuiko wa vyombo mbalimbali,vinavyopaswa kufuatilia kujua nini kimetokea,,
Unaweza kuita vyovyote unavyotaka,kamati,chama,jumuia,kikundi,etc
 
Kwa nini iwe mjumuiko wa vyombo vyote na sio kila chombo kichunguze kivyake na kitoe ripoti yake?
Kamati ni mjumuiko wa vyombo mbalimbali,vinavyopaswa kufuatilia kujua nini kimetokea,,
Unaweza kuita vyovyote unavyotaka,kamati,chama,jumuia,kikundi,etc
 
Kwa nini iwe mjumuiko wa vyombo vyote na sio kila chombo kichunguze kivyake na kitoe ripoti yake?
Synergy,,,
Itakua vurugu mechi, kwamba Tanesco achunguze kivyake, osha kivyake, bima kivyake, polisi kivyake,mkandarasi kivyake etc
Huo sio uchunguzi, ni vurugu mechi.
 
Usisahau hakuna njia inayopitika kirahisi around the market pamoja na kuwa na lami

Tumeachia machinga wakamate mamlaka

SoMo kubwa Sana hili
... uko sahihi. Maisha ni bora kuliko mali. Kuliko kuumiza machinga waliotanda barabarani ni bora huo msoko uungulie mbali.
 
Majanga yanatokea kokote pale viongozi, serikali haijakosea kuunda kikosi kazi #kamati# kubaini chanzo cha mlipuko wa moto kama hakijulikani kuwa ni miundombinu isiyo rafiki na inayoweza kuwa imechakaa kitambo (chakavu).

Janga ni hasara pia fursa kwa wengine kama wajumbe wa kamati. Kwa kuwa kariakoo ni soko la kimataifa ni vema na vidhibiti majanga vikawa vya kimataifa zaidi ( zana za kukabiliana na majanga ziwe karibu na soko).
 
Hilo ni suala linalohusu jeshi la zimamoto.Wakiona kuna hujuma ndio watawaita polisi .
Tanesco, Osha na Bima, mkandarasi wa nini? Au jeshi la zimamoto halina utalaamu wa kubaini vyanzo vya moto?
Synergy,,,
Itakua vurugu mechi, kwamba Tanesco achunguze kivyake, osha kivyake, bima kivyake, polisi kivyake,mkandarasi kivyake etc
Huo sio uchunguzi, ni vurugu mechi.
 
Back
Top Bottom