Maneno hayo ya Martin Luther King Junior miongo kadhaa iliyopita yana ukweli leo kuliko wakati mwingine wowote. Ndugu zetu wa kitanzania leo watalala nje na kushindia kula mikate kwa vile tu serikali yao haiko tayari kukubali makosa na kusahihisha. Binafsi, sina sababu hata chembe ya kufuatilia suala hili kwani sina maslahi yoyote nalo, sina ndugu, rafiki, jamaa n.k. Hata hivyo nina kifungo kimoja na ndugu zetu hawa kwamba sisi sote ni Watanzania na kama mazingira yangekuwa tofauti bila ya shaka tungeweza kukutana, kusoma pamoja, kucheza pamoja na hata kuoleana!!
Kiburi cha serikali kinaudhi na kinakera. Hata hivyo haitoshi kulalamika na kuwaonea huruma tukiwa tumeketi kwenye vyumba vyetu na sebule zetu huku tukipunga upepo wa starehe zetu. Binafsi nimejitolewa kuwasaidia kiasi kidogo nilichonacho kuwapa chakula cha uhakika kwa siku hizi watakazoketi ubalozini.
Bila ya shaka kuna baadhi ya wananchi wenzangu ambao nao wameguswa na stori hii. Kama unataka kupiga simu piga namba hii na uulize jinsi ya kuwasaidia. Namba 380-936 411476 na utazungumza na Bashiri (kiongozi wa msafara huo) na utaamua mwenyewe nini na jinsi utawasaidia.
Maneno na huruma peke yake haitoshi.. this is a call to action!!! Stand up and be counted! you sons and daughtrers of my beloved motherland, dare to act now! you visionaries of the new springtime of hope for Tanzania, you fellow Tanzanians, a breed of a new generation of courage and you who have desired greatness for your nation it is about time to rise! Stand up and act, speak and be heard! But as I always say, if you are a follower then wait, but if you have a spark of leadership in you, then lead!! It is about time.