Serikali yazungumzia tishio la Serikali ya Marekani kusitisha misaada

Serikali yazungumzia tishio la Serikali ya Marekani kusitisha misaada

Makini

Senior Member
Joined
Dec 23, 2014
Posts
154
Reaction score
59
attachment.php


Serikali imezungumzia tishio la Serikali ya Marekani la kusitisha misaada kwa Serikali ya Tanzania kutokana na mgogoro wa kisiasa Zanzibar na kukamatwa kwa maofisa wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu.

Ofisi ya Ikulu yasema masharti yaliyotolewa na Serikali ya Marekani yanatekelezeka na yatamalizwa kabla ya kikao cha Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Milenia (MCC) kukaa Desemba, mwaka huu.

Wiki iliyopita, Serikali ya Marekani iliitaka Serikali ya Tanzania kumaliza haraka mgogoro wa kisiasa wa Zanzibar, vinginevyo upo uwezekano wa kusitishwa msaada wa zaidi ya Dola za Marekani milioni 472 (Sh. bilioni 999.4), za awamu ya pili ya fedha za MCC la nchi hiyo.

Chanzo: EATV
 

Attachments

  • Ombeni Sefue.png
    Ombeni Sefue.png
    59.3 KB · Views: 34,067
Nawasitishe tu hakuna jinsi, dhahabu tunazo, gesi ya kufa MTU, mlima kilimanjaro, mbuga za wanyama Bandar sasa mungu atupe nini sie watanganyika??? Naomba mungu wasitishe tuone km tutakufa
 
Nawasitishe tu hakuna jinsi, dhahabu tunazo, gesi ya kufa MTU, mlima kilimanjaro, mbuga za wanyama Bandar sasa mungu atupe nini sie watanganyika??? Naomba mungu wasitishe tuone km tutakufa

Hivi unajua maana ya neno Marekani au wale wakiamua kukubania utajuta mnaweza ambiwa mwisho kusafiri kenya, hamkawii kuambiwa dhahabu zenu hazina ubora mtaziangalia? Wana mikwara balaa.
 
Kama suluhu itapatikana kabla ya kikao cha bodi December ina maana hakuna uchaguzi ni kukamilisha tu sehemu iliyobaki.
 
Mdetichia hiv wafikiri kuna nini chapoteza hadisasa, n?hi ina wenyewe hii wenye kuamua nini kiwe na nani awe nani kwa faida zao, me mtanganyika wa hali ya chini nasema liwalo na liwe nimechoshwa na ushenzi unaoendelea, na imani sipo peke Yangu nilochoshwa na hii hali
 
Ona viongozi wakubwa wanavyojibu kwa busara. Kuna wafuasi humu sijui wanafananisha uongozi wa nchi na kitu gani walitaka serikali ijibu jeuri!!

Hatuendi hivyo siku zote wenye akili wanaangalia maslahi makubwa zaidi
 
Unafikiri Rais wako Magufuli hajui kwamba tuna dhahabu, gesi na mlima Kilimanajaro ? Wewe unafikiri kwa nini kanywea pamoja na kulijua hilo ?Watu wanawawekea vikwazo Russia iliyo na nguvu za kijeshi, inauza silaha za kufa mtu, ina mafuta na gesi kibao, itakuwa sisi ambao hata bajeti yetu wenyewe hatujitoshelezi !?
Nawasitishe tu hakuna jinsi, dhahabu tunazo, gesi ya kufa MTU, mlima kilimanjaro, mbuga za wanyama Bandar sasa mungu atupe nini sie watanganyika??? Naomba mungu wasitishe tuone km tutakufa
 
Tujitahidi tuondokane na "Kwa hisani ya watu wa Marekani"
 
nawasitishe tu hakuna jinsi, dhahabu tunazo, gesi ya kufa mtu, mlima kilimanjaro, mbuga za wanyama bandar sasa mungu atupe nini sie watanganyika??? Naomba mungu wasitishe tuone km tutakufa

we nawe ,,kwani havikuwepo hivyo vitu toka mwanzo,,bado tunahitaji hizo fedha,,unafikiri rea na miradi ya maendeleo vijijini inafanywa na serikali,,hebu google upate uelewa,,tena zitafanya kazi nyingi maana za nyuma zilikua zinaliwa sana
 
Marekani ina mambo yake; wamemvunja mrusi na umoja wake, hapa hata wakiamua kumleta/kumwingiza mtu wamtakaye au atakayewapa maslahi wanafanya hivyo...
Angalia nchi zilizo na vita, akiingia mmarekani pale lazima atamleta mtu wake..Angalieni sana kauli za Marekani
 
Back
Top Bottom