Mkata-tamaa
Senior Member
- Nov 21, 2018
- 180
- 312
Check tyres zako uimara wake.
Sina gari lakini
Wakuu poleni na pilika za kutafuta tonge la kila siku
Wiki mbili zijazo natarajia kusafiri mimi na familia yangu kwa kutumia usafiri binafsi
safari ni kutoka mbeya kuja Dar
Lengo la kufungua uzi huu ni kuomba ushauri kwenu,ni servise gani hasa natakiwa kufanya ili niweze kusafiri salama na ki ISt changu?
Maana binafsi servise nilizozoea ni zile za kumwaga oil tu na kubadili filter.
Nini nikifanye hasa kwenye gari langu ili kuliweka katika hali salama ya kusafiri nalo?
Natanguliza shukrani zangu kwenu.
Elimu kidogo hapa mkuu!Kumbuka usifunge tairi na kuondoka nazo siku hiyo hiyo zitembelee hata siku mbili kama utabadili tairi mpya
Cheki kwanza fan belt kama haijachoka engine oil iwe mpya maji kwenye betri na regetor na mfuta ya brek jeki na tringle angle reflector(huo ni uangalizi wa ndani)kwa nje check stads tyre zako zote kama zimekaza vizuri uwe na tyre spare nzima upepo kwenye tyre mafuta ya kutosha kwenye tank na majibya reserve kwenye kidumu au mle kwenye reserve yake og.
Nyongeza: uwe na angalau kalaki ka emegency njiani wale wa nguo nyeupe same time wanazinguaga sana huko njiani
Kama hujawahi masafa marefu kuwa makini
Mkuu usisahau kuweka nyimbo mpya kwny redio yako itasaidia safar kuwa fupi
Mimi nasema weka tairi mpya.
Tembea na jeki.
Tembea na spana inayozifungua na kuzifunga vizuri nati zako.
Kuna balaa lilinipata nilisafiri na IST haina jeki, spana, wala tairi la akiba. Nilienda kukwama kijiji fulani hivi nyuma ya Ruaha Mbuyuni na kilometa 15+ baada ya Mikumi. Jina limenitoka.
Ila hapo hakuna netwek siyo ya simu tu hata ya redio. Safari ya kutoka Dar kwenda Mbeya nilitumia siku 2 na nusu badala ya saa 10.
Matairi jambo la msingi sana chief.
PS. Jf inadhalilisha mno wenye baby walker hadi mtu anaandika 'Ki IST changu' badala ya 'IST yangu'
Pia mi sina gari nilikua dereva tu
kama amewahi asiwe makini au sio mkuuKama hujawahi masafa marefu kuwa makini
Hii sio necessary Sana ni concepts Tu kama vipi jaza upepo Kwa Matairi yote Kwa pressure ya 35 Kwa kila tairi..Ubarikiwe sana boss
Kwenye matairi kuna suala zima kubalance upepo
Wengine wananiambia upepo wa tairi za mbele uwe mdogo kuliko upepo wa tairi za nyuma ,je kuna ukweli hapa?
Na ni upepo kiasi gani unaotakiwa kwa tairi za mbele na tair za nyuma ni upepo kiasi gani?
Hii sio necessary Sana ni concepts Tu kama vipi jaza upepo Kwa Matairi yote Kwa pressure ya 35 Kwa kila tairi..
nenda kwenye garage ya maana mwambie akufanyie safari check ,atafanya vyote