BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Upande wa Jamhuri katika kesi ya mauaji ya mtoto mwenye ualbino, Asimwe Novath (2) umewasilisha maelezo ya ushahidi katika hatua ya awali, ukieleza utakuwa na mashahidi 52 na vielelezo 37.
Katika maelezo hayo ya ushahidi, mmoja wa mashahidi ameeleza mbinu iliyotumiwa na washtakiwa kumpora mtoto huyo na kutokomea, pia ikitajwa ahadi ya gari aina ya Toyota V8, maarufu kama shangingi, kwa baba wa mtoto.
Asimwe aliporwa na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwao Kijiji cha Bulamula, Kata ya Kamachumu wilayani Muleba mkoani Kagera, Mei 30, 2024 saa 2:00 usiku na kutokomea naye kusikojulikana.
Siku 17 baadaye mabaki ya mwili wake yalipatikana yakiwa yamefungwa kwenye mfuko wa sandarusi (kiroba) na kutelekezwa chini ya kalavati lililoko Barabara ya Makongora, Kitongoji Kabyonda, Kata ya Ruhanga wilayani humo.
Pia Soma:
- Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba limemsimamisha Padre Rwegoshora kufuatia tuhuma za kuhusika mauaji ya Asimwe Novath
Siku kadhaa baadaye, Jeshi la Polisi lilitoa taarifa ya kuwashikilia watu tisa akiwemo baba wa marehemu, Novath Venanth na Padri Elpidius Rwegoshora na kuwafungulia kesi ya mauaji namba 17740/2024, katika Mahakama ya Wilaya ya Bukoba mkoani humo.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Nurdini Masudi, Ramadhani Selestine, Rweyangira Alphonce, Dastan Bruchard, Faswiu Athuman, Gozbert Alikad na Desdery Everigist wote wakazi wa mkoani Kagera.
Katika maelezo hayo ya ushahidi, mmoja wa mashahidi ameeleza mbinu iliyotumiwa na washtakiwa kumpora mtoto huyo na kutokomea, pia ikitajwa ahadi ya gari aina ya Toyota V8, maarufu kama shangingi, kwa baba wa mtoto.
Asimwe aliporwa na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwao Kijiji cha Bulamula, Kata ya Kamachumu wilayani Muleba mkoani Kagera, Mei 30, 2024 saa 2:00 usiku na kutokomea naye kusikojulikana.
Siku 17 baadaye mabaki ya mwili wake yalipatikana yakiwa yamefungwa kwenye mfuko wa sandarusi (kiroba) na kutelekezwa chini ya kalavati lililoko Barabara ya Makongora, Kitongoji Kabyonda, Kata ya Ruhanga wilayani humo.
Pia Soma:
- Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba limemsimamisha Padre Rwegoshora kufuatia tuhuma za kuhusika mauaji ya Asimwe Novath
Siku kadhaa baadaye, Jeshi la Polisi lilitoa taarifa ya kuwashikilia watu tisa akiwemo baba wa marehemu, Novath Venanth na Padri Elpidius Rwegoshora na kuwafungulia kesi ya mauaji namba 17740/2024, katika Mahakama ya Wilaya ya Bukoba mkoani humo.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Nurdini Masudi, Ramadhani Selestine, Rweyangira Alphonce, Dastan Bruchard, Faswiu Athuman, Gozbert Alikad na Desdery Everigist wote wakazi wa mkoani Kagera.