Shaka : Baada ya kifo cha Hayati Dkt Magufuli,wale wote Waliombeza Rais Samia Ujenzi wa miradi ya kimkakati leo wanaumbuka, Wami ilikuwa 47% leo 89.2%

Huyu mama Samia ni mchapakazi hakuna mfano, halafu haongei ongei na kubwatuka, watu wanaona nchi inajengwa tuu
 
Magufuli angekuwepo hii miradi ingekuwa imekamilika kitambo hadi tungekuwa tumesahau.kwa kuwa hii ni awamu ya wazembe na maneno mengi ndiyo matokeo yake miradi imechelewa kukamilika.miradi kama ya umeme wa mwl nyerere tungekuwa tunafaidi matunda yake,sgr morogoro tungekuwa tunafaidi na mradi wa mwendokasi morocco-mwenge ambao umekufa baada ya mwamba kufariki tungekuwa tunaseleleka tu mwanzo mwisho.Tuivumilie tu hii awamu ya wazembe
 
Mkuu unaemsema kwa miaka minne kajenga asilimia 47 na unaemuona hawezi 42% Kwa mwaka mmoja na nusu ,sijui hapo nani ni bora
 
Kwanza apongezwe mtoa maono,stupid
 
Shaka asisahau flyover ya veta pale ina matuta na haifanani hata kidogo na mfugale wala kijazi. Tena kwa macho ya kawaida tu.

Sasa anatakiwa ajue kuna kujenga ili liishe na kuna kujenga kwa kuzingatia viwango. Hilo daraja hata kwa picha tu halina tofauti na lililojengwa kwa kuchangishana wananchi.
 
Rais Samia anafanya vizuri Sana hata kama hutaki huo ndio ukweli wenyewe
 
 
Usimpuuze alieona hayo maono akaanzisha,yeye amalizie yalioanzishwa
Maoni yapi? Miradi yote kuanzia Mwendo Kasi, Flyovers, upanuzi wa airport,miradi ya maji from ziwa Victoria n.k ilikuwepo kwenye mpango wa Taifa, framework za DMDP n.k so sio kwamba inaanzishwa na JPM Ila hizo blueprint zipo toka enzi za Mkapa na hata Samia naye anafanya kazi blue print alizozikuta na zitaendelea hata Rais angekua Lissu.

Tatizo waTanzania hatusomi tunapenda kuona kama miradi ni zawadi ya mtu Fulani ilihali ni Kodi zetu na tayari imeshapangwa miaka na miaka na tume ya mipango tokea enzi za Mkapa huko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…