Shaka: Watanzania watege sikio tarehe 09 Oktoba Dodoma, Rais ana jambo la kuwaambia watanzania

Shaka: Watanzania watege sikio tarehe 09 Oktoba Dodoma, Rais ana jambo la kuwaambia watanzania

Wasaka urais kuelekea mwaka 2025 kuondolewa rasmi ndani ya Baraza la Mawaziri siyo!? Uamuzi huu unapaswa kuangaliwa kwa uangalifu mkubwa sana.

Uwepo wa wateule wa JPM ndani ya baraza bado una umuhimu mkubwa sana kwa utengamano wa CCM ya sasa. Ili kuthibiti pilikaplika za hapa na pale, ni vyema wakazidi kuwepo.

Natambua kauli ya "niguse ninuke" iliyotolewa kule jimbo la kusini wakati wa ziara ya PM inafungua "codes" fulani muhimu ili kuhalalisha mabadiliko tarajiwa. Hamasa inafanyika ili kuondoa makapi ya 'champion" wa Chato.

Ila tahadhari ichukuliwe kama washika hatamu wameazimia kumundoa mtu huyu na huyu katika wizara hizo nyeti kwa muda huu. Ni vyema wavute sunira, ili kwa "timing" kubwa akapanguliwa mmoja baada ya mwingine kuliko kuwaondoa wote kwa pamoja. Kwa pupa hii, hakika chama twawala kinakwenda kupasuka rasmi katika makundi mawili na kuelekea katika kifo chake.
Shaka siyo msemaji wa serikali msichanganye mambo.

Hapo ni issue za chama na siyo za serikali.
 
Mama samia ni msemaji mzuri, lakini katika vitendo na matoke ni hafifu.


Samia Anaweza akasema au akaagiza kitu kifanyike, na hakuna matokeo chanya.


Mtangulizi wake Hayati Joseph Magufuli alikuwa akiagiza kitu fulani kifanyike, basi matokeo wote mnayaona.

Mswahili huwa hana haya au soni bali Huogopa

Nafikiri mtangulizi alikuwa analielewa hilo na ndio maana alikuwa anawaita wapumbavu
 
🤣🤣🤣

Godbless Lema ndiye waziri wa fedha.....🙄🤣🤣
Ataiba mpaka vikiko hapo mbunge tu alupokuwa kaiba mpaka anazurumu watu sasa hivi kakimboa kesi mwizi mkubwa halafu awe waziri wa fedha kweli?
 
Mkuu, usilinganishe CCM ile ambayo ilikuwa na makada wahafidhina na wenye kuaminika, na hii ya sasa ambayo ni sawa na sikio la kufa.
CCM ni imani....imani HAIFI mkuu wangu.....

Changamoto inaonekana kwa kuwa wanachama wa CCM wameongezeka mno kulingana na raia kuongezeka......ndipo pale unapoambiwa CCM NI BAHARI....na bahari Ina kila aina ya VITU.....
 
Shaka siyo msemaji wa serikali msichanganye mambo.

Hapo ni issue za chama na siyo za serikali.
Mkuu, hivi unaweza kutukumbusha ni kwa wakati gani umewahi kusikia "veggies" wanatenganisha shughuli za chama na za kiserikali.
 
Mkuu, usilinganishe CCM ile ambayo ilikuwa na makada wahafidhina na wenye kuaminika, na hii ya sasa ambayo ni sawa na sikio la kufa.
Yani Polepole na Bashiru ndio wa kuaminika?

Kweli dikteta uchwara amewaacha yatima na wajane, mtakoma kumtegemea binadamu mwenzenu.

Inaoneka mlikuwa hamuamini kuna siku atakufa na atakokotwa kwenye kitoroli kwenda kufukiwa.
 
Anasema uongo UN, amembambikia kesi Mbowe halafu unasema hana longo longo?

Kupata Rais anayefaa ni lazima tuwe ná uchaguzi huru na wa haki. Ni lazima tuwe na Tume huru ya uchaguzi. Ni lazima tuwe na Bunge linaloelewa wajibu wake kwamba wao ni wawakilishi wa Watanzania Bungeni na si wawakilishi wa maccm au chama chao Bungeni hivyo wawe tayari wakati wowote ule KUIKEMEA Serikali bila woga wa kutishiwa kwamba Bunge litavunjwa.

Yaani kwa kiongozi wa nchi sasa hivi ndiyo tunaye mama Yuko makini anapiga kazi hana longo longo ni mtu wa matokeo hivi viti anavyofanya hamvioni kweli au kama kawaida yenu kubisha Kila kitu? Hebu tuambie wewe ulitaka nani awe rais ili akifanya kitu uone kweli kimefanywa n rais? Hebu taja mmoja tu nikuone kama una akili
 
Mkuu, hivi unaweza kutukumbusha ni kwa wakati gani umewahi kusikia "veggies" wanatenganisha shughuli za chama na za kiserikali.
Msemaji wa serikali ni Msigwa, sijui hizi bangi huwa mnavuta saa ngapi?
 
CCM ni imani....imani HAIFI mkuu wangu.....

Changamoto inaonekana kwa kuwa wanachama wa CCM wameongezeka mno kulingana na raia kuongezeka......ndipo pale unapoambiwa CCM NI BAHARI....na bahari Ina kila aina ya VITU.....
Mkuu hakuna cha imani wala nini zaidi ya kutafuta maslahi na kimbilio la uhakika la kuficha historia ya ufisadi na hata kutakatisha fedha chafu.
 
😳😳Mara moja hii umeshasahau HOJA YAKO kuwa Mh.SSH anakiendeleza kipi katika slogan yake ya "kazi Iendelee" ?!!Khaaaa 🤣🤣🤣
Sijasahau hoja. Nimekupatia maans ya kuendeleza na sio kukopi na kupaste. Nimekuuliza kati ya miradi uliyoitaja nieleze maono yake mapya katika miradi hiyo. Nitajie mradi mmoja tu na unipe maono yake ya nyongeza tofauti na ya mtangulizi wake

Nakupa mfano mmoja. Alipoenda Uganda kusaini mkataba wa Bomba la Mafuta. Ulisikiliza Hotuba yake na ile ya Mseveni. Uliweza kubaini tofauti yoyote ya kimaono kati ya Viongozi hao wawili?
 
Ataiba mpaka vikiko hapo mbunge tu alupokuwa kaiba mpaka anazurumu watu sasa hivi kakimboa kesi mwizi mkubwa halafu awe waziri wa fedha kweli?
🤣🤣🤣🤣

Hiyo ndiyo serikali anayotaka kuona BAK ikitutawala....yaani full vichekesho.....

Nisalimie katibu mkuu wao kiongozi ndugu MDUDE NYAGALI.....🤣🤣
 
Wana CCM bhanaa!!!
Shaka ni CCM.
Mh. Samia Suluhu H. ni Mwenyekiti wa CCM - Taifa, ambaye pia ni Rais wa JMT.
Kwa Uenezi wake Shaka,automatically atakuwa anamzungumzia "mwenyekiti wa CCM - Taifa.
Automatically hilo jambo lake litakuwa la CCM.
Kumuaddress SSH kama "rais" na huku yeye si msemaji wa rais, na kuhusisha jambo la chama na taasisi ya urais ni kuonyesha jinsi gani watu wa Lumumba na White House hawajui "job descriptions" zao wala mipaka ya nafasi zao.
Tatizo kubwa sana lililopo kwa Watanzania wengi.
Km dingilai aliepaka v8 zote za sirikali rangi ya yanga na kuzipigia kampeni
 
Hivi ni lini araonekana Raisi mwenye maono na Falsafa? Mwl. Nyerere, Mkapa na Magufuli wote hao ulikuwa ukiwasikiliza unaona wamebeba Falsafa na maono Fulani. Hebu tusaidie maono na Falsafa yake
Kwa sasa Samia anafanya vizuri kuwazidi hao uliowataja. Halafu umekosea mno kumuweka na Magufuli kwenye hiyo orodha. Yule hakuwa na falsafa yoyote. Alikuwa msanii tu ambaye ametumia ujinga na ukosefu wa maadili wa watanzania kujijenga.

Raisi gani mwenye falsafa anatumia fedha za umma kama mali ya familia yake?

Raisi gani mwenye falsafa anatumia pesa za umma kununua wapinzani?
 
Kwa sasa Samia anafanya vizuri kuwazidi hao uliowataja. Halafu umekosea mno kumuweka na Magufuli kwenye hiyo orodha. Yule hakuwa na falsafa yoyote. Alikuwa msanii tu ambaye ametumia ujinga na ukosefu wa maadili wa watanzania kujijenga.

Raisi gani mwenye falsafa anatumia fedha za umma kama mali ya familia yake?

Raisi gani mwenye falsafa anatumia pesa za umma kununua wapinzani?
Kuwa na maono haimaanishi kukosa udhaifu. Huyu wa sasa hana maono na ana udhaifu pia.
 
Sijasahau hoja. Nimekupatia maans ya kuendeleza na sio kukopi na kupaste. Nimekuuliza kati ya miradi uliyoitaja nieleze maono yake mapya katika miradi hiyo. Nitajie mradi mmoja tu na unipe maono yake ya nyongeza tofauti na ya mtangulizi wake

Nakupa mfano mmoja. Alipoenda Uganda kusaini mkataba wa Bomba la Mafuta. Ulisikiliza Hotuba yake na ile ya Mseveni. Uliweza kubaini tofauti yoyote ya kimaono kati ya Viongozi hao wawili?
Kabla ya kuendelea na mjadala...

Unamuwekea mdomoni mwake maana ya "KAZI INAENDELEA"?!!!

Unanipa "sherehe" ya maneno hayo jinsi utakavyo wewe iwe na si walioyatoa?!!!
2935090_IMG-20210717-WA0000.jpg
 
Back
Top Bottom