Shambulio dhidi ya Mbowe: Kamanda Giles Muroto (RPC Dodoma), umewaona wa kuwakamata? Nakutajia...

Shambulio dhidi ya Mbowe: Kamanda Giles Muroto (RPC Dodoma), umewaona wa kuwakamata? Nakutajia...

Kuna habari kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ameshambuliwa na 'watu wasiojulikana' jijini Dodoma alipokuwa akirejea nyumbani kwake usiku wa kuamkia jana. CHADEMA, kupitia kwa Katibu Mkuu wake John Mnyika, wakatoa taarifa ya awali kwa umma juu ya shambulio hilo la Mwenyekiti na kingozi wao huyo wa juu kabisa kwenye chama chao.

Nilipata faraja nilipokuona Kamanda Muroto ukijitokeza mbele ya wanahabari na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kutoa kauli ya Jeshi la Polisi mkoa wa Dodoma kuhusu shambulio la Mbowe. Kwa umakini na ustadi mkubwa Kamanda Muroto ukauambia umma wa watanzania mambo makubwa matatu. Kwanza, uchunguzi dhidi ya tukio hilo umeanza na unafanywa na jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama.

Pili, tukio la Mbowe lisitumike kisiasa na kama mtaji wa kisiasa na yeyote. Na tatu, ni kupiga marufuku mtu yeyote kulizungumzia jambo hilo kwa minajiri ya kuingilia uchunguzi wa kipolisi. Nilikuelewa sana. Nilitamani na ninatamani kuona ukisimamia kauli zako juu ya shambulio dhidi ya Mbowe. Nikupe taarifa au nikukumbushe kama tayari unajua kuwa jana Bungeni Mbowe alikuwa gumzo kwenye mjadala wa kupitisha Azimio la kumpongeza Rais Magufuli.

Kiti cha Spika wa Bunge kikikaliwa na Job Ngugai mwenyewe kiliruhusu mjadala wa tukio la shambulizi la Mbowe. Wachangiaji walipangwa kimkakati ili kutimiza azma yao. Kuanzia kwa Spika Ndugai, Silinde, Lijualikali, Musukuma na hata Lusinde, wote walikejeli tukio hilo na kulihusianisha na ulevi. Walihitimisha kwa kusema kuwa Mbowe alikuwa amelewa na aliteleza kwenye ngazi zake na kuvunja/kutegua mguu wake. Tena akiwa na 'kimada'.

Wabunge hao niliowataja walikebehi na kumkejeli vya kutosha Mbowe na kulikejeli shambulo lake. Tayari wameshaingilia na kuvuruga uchunguzi wa Polisi kwenye tukio hilo. Wanaachwaje bila ya kukamatwa katika kutekeleza kauli ya kamanda Muroto? Wanaopaswa kukamatwa ni Spika Ndugai na Wabunge Silinde, Lusinde, Musukuma na Lijualikali. Wameshaingilia uchunguzi wa Polisi. Wameshakiuka marufuku ya Muroto.

Tunajua kuwa Mbowe anaponzwa na Lissu. Ukifika muda tutayasema yote. Kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2020. Kwanza tumalize hili la Mbowe.

RIP Pierre Nkurunzinza, mwanamichezo uliyeichezea hadi katiba na sheria!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Ahaaa! Kumbe wabunge hao walikuwepo kwenye tukio. Walimuona Mbowe kalewa akiwa na dadapoa. Afande Muroto, waite hao wasaidie polisi.
 
Hivi mlimuelewa katibu mkuu Jana wakati anazingumza na waandishi wa habari? Nakumbuka alisema kuna clip ya mtu mmoja hivi siku chache zilizopita ilikuwa inaonyesha kuwa Kuna tukio la shambulio kwa viongozi wa upinzani linaenda kutokea siku chache
Sasa cjui Ni kweli Mnyika alikuwa anamaanisha mi cjui

He is correct!
Kuna clip moja kwenye YouTube ilionekana siku 1 tu na iliondolewa kabla haijaenda viral!
Sikuwahi kui- download lakini ilikuwa inaashiria tishio la kifo Cha Kiongozi mmoja Mkuu wa Upinzani (very likely) ilimlenga Mbowe!
Aliyekuwa akisema hayo ni Mtu mmoja anajiita Nabii hivo alikuwa akitoa unabii
Acha tu mkuu inasikitisha sana ametamka na kasema bunge lijalo wanauhakika 100% watarudi na kuipitisha hiyo hoja ya kessy kwa kishindo hata kama Rais hataki wao wataongeza tu.

Acha waongeze tu...Marehemu Nkurunziza alitaka kubadili Katiba aongoze kwa miaka 30 (2005~2035) lakini Warundi wakapiga kelele ndipo akaamua kuishia mwaka huu 2020 na Mungu naye akaamua kumpumzisha milele....!!
CCM wathubutu, sanasana wataambulia kilichomtokea Pierre!
Ni hayo tu!
 
Wewe ndo unapaswa kukamatwa kwa kulisingizia Bunge kwamba lilipanga wazungumzaji. Hivi unajua kwamba Mbunge ana kinga na akishaongea ndani ya Bunge hakuna chombo chochote chenye mamlaka ya kumhoji isipokuwa Kamati za Bunge kama kuna haja ya kufanya hivyo?

Kwani hao walio zungumzia tukio zima na kuhalalisha ndani ya Bunge ushahidi waliupata wapi !!?.Waachwe tu waongee hata kama wana vunja Sheria!!.Uhakika wa walicho kizungumza ni kipi !?.Jeshi la Polis na hao wabunge ni nani wa kusikilizwa !!?
 
Hayo ni maoni yako japo ni ya kipumbavu sana; serikali inaweza kukudhuru au kukutoa uhai ata kama wewe siyo Mbunge au KUB.

Suala la Mh Mbowe kutorudi Mbungeni ni baada ya uchaguzi wewe kuisemea utadhani kura imeshabigwa unaonesha ushaidi wa ujinga kwenye hoja yako.

Kumbuka pia serikali isiyolinda raia wake na kutopata wale wote wanaousika kwenye matukio yenye nia ya kuondoa uhai wa raia wake basi yenyewe ndiyo inakua inahusika kuyaratibu hayo matukio.

Kwaushauri japo siyo lazima uipokee; punguza ujinga kwani unaelekea kwenye upumbavu.
Jibu hoja za ruhi acha kupagawa na kuongea lugha chafu, Kama huwezi jibu kaa kimya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mvamizi anayo sababu, hivyo mvamizi ni yeyote mwenye sababu ya uvamizi huo. Na huyo ni yule ambaye uwepo wa mvamiwa haumpi amani mvamiaji. Sisi wengine wote ni mashabiki wa hilo tukio.
 
Kuna habari kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ameshambuliwa na 'watu wasiojulikana' jijini Dodoma alipokuwa akirejea nyumbani kwake usiku wa kuamkia jana. CHADEMA, kupitia kwa Katibu Mkuu wake John Mnyika, wakatoa taarifa ya awali kwa umma juu ya shambulio hilo la Mwenyekiti na kingozi wao huyo wa juu kabisa kwenye chama chao.

Nilipata faraja nilipokuona Kamanda Muroto ukijitokeza mbele ya wanahabari na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kutoa kauli ya Jeshi la Polisi mkoa wa Dodoma kuhusu shambulio la Mbowe. Kwa umakini na ustadi mkubwa Kamanda Muroto ukauambia umma wa watanzania mambo makubwa matatu. Kwanza, uchunguzi dhidi ya tukio hilo umeanza na unafanywa na jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama.

Pili, tukio la Mbowe lisitumike kisiasa na kama mtaji wa kisiasa na yeyote. Na tatu, ni kupiga marufuku mtu yeyote kulizungumzia jambo hilo kwa minajiri ya kuingilia uchunguzi wa kipolisi. Nilikuelewa sana. Nilitamani na ninatamani kuona ukisimamia kauli zako juu ya shambulio dhidi ya Mbowe. Nikupe taarifa au nikukumbushe kama tayari unajua kuwa jana Bungeni Mbowe alikuwa gumzo kwenye mjadala wa kupitisha Azimio la kumpongeza Rais Magufuli.

Kiti cha Spika wa Bunge kikikaliwa na Job Ngugai mwenyewe kiliruhusu mjadala wa tukio la shambulizi la Mbowe. Wachangiaji walipangwa kimkakati ili kutimiza azma yao. Kuanzia kwa Spika Ndugai, Silinde, Lijualikali, Musukuma na hata Lusinde, wote walikejeli tukio hilo na kulihusianisha na ulevi. Walihitimisha kwa kusema kuwa Mbowe alikuwa amelewa na aliteleza kwenye ngazi zake na kuvunja/kutegua mguu wake. Tena akiwa na 'kimada'.

Wabunge hao niliowataja walikebehi na kumkejeli vya kutosha Mbowe na kulikejeli shambulo lake. Tayari wameshaingilia na kuvuruga uchunguzi wa Polisi kwenye tukio hilo. Wanaachwaje bila ya kukamatwa katika kutekeleza kauli ya kamanda Muroto? Wanaopaswa kukamatwa ni Spika Ndugai na Wabunge Silinde, Lusinde, Musukuma na Lijualikali. Wameshaingilia uchunguzi wa Polisi. Wameshakiuka marufuku ya Muroto.

Tunajua kuwa Mbowe anaponzwa na Lissu. Ukifika muda tutayasema yote. Kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2020. Kwanza tumalize hili la Mbowe.

RIP Pierre Nkurunzinza, mwanamichezo uliyeichezea hadi katiba na sheria!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)


Kazi ya polisi siku hizi ni kuchonga uongo kama wa Lissu. Sababu kubwa ni hao hao wa serikalini ndiyo wamefanya haya
 
Mzee wangu leo umeamua kutupa kweli Kama jina lako linavyo shabihisha. Sitomkebehi wala kumkashifu bali nitajitahidi kuhoji;

1. Kiongozi Mkuu wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni saa 6 - 7 ulikua wapi bila ya kuwa na ulinzi wa ainayoyote?

2. KUB ni nani aliyemkimbiza hospitali baada ya shambulio?

3. Kauli za kujikanganya za John Mnyika Katibu Mkuu, taarifa ya kwanza hakujibu hoja ya pili taarifa ya pili katuambia wakati anashamvuliwa hakuwa peke yake!

A. Umeongozana na mtu anavamiwa na kuvunjwa mguu usipigwe hata kofi?

B. Aliongozana naye au huyu mtu wa pili alikua mbali na eneo la tukio hivyo washambuliaji hawakumuona?

IWAPO B NDIVYO ILIVYOKUA;
i. Maneno ya kwamba unaisumbua Serikali hayana ushahidi kwakua yanaweza kuwa ya kupika

ii. Hatuna shida ya kukuua ila kukuvunja mguu ili tuone kampaini zako utafanyaje?

Tuna muda gani umebaki kabla ya kuanza kampeini? Mguu unapona baada ya muda gani? Jinsi alivyoonekana jana hakupigwa antena bali POP ambalo hufungwa kwa kuteguka na si kuvunjika?

YOTE TISA KUMI DHANA YA KWAMBA SERIKALI IMEHUSIKA KWENYE TUKIO

Ni upuuzi au mpuuzi kiasi gani anayeweza kumvamia KUB ambaye muda wake uko ukingoni na kurejea ni majaaliwa?

Serikali imvamue Mbowe kwa lipi hasa? Miezi michache iliyopitwa walikua na Golden chance ya kumfunga si wangemalizana naye kule?

MUDA NI RAFIKI MWEMA, IWAPO HOJA HIZO ZITAPATIWA MAJIBU NA AFANDE MUROTTO HIYO NDIO ITAKUA PONA PONA YAKE NA IWAPO MATOKEO YATATHIBITISHA KWAMBA ALITELEZA TU!

MUNGU NDIYE AJUAYE HATIMA YAKE

Unadhan kwanini wanahusisha serikali na sio majambazi?

Kwani mlevi akiwa ametoka kulewa hana haki ya kuvamiwa?

Hoja sio yy kuwa na walinzi hoja ni eneo natwa kuwa linatakiwa kuwa na ulinzi swali ni je mbona ulinzi haukuwepo?
 
Unadhan kwanini wanahusisha serikali na sio majambazi?

Kwani mlevi akiwa ametoka kulewa hana haki ya kuvamiwa?

Hoja sio yy kuwa na walinzi hoja ni eneo natwa kuwa linatakiwa kuwa na ulinzi swali ni je mbona ulinzi haukuwepo?
Kwani mlevi akiwa ametoka kulewa hana haki ya kuvamiwa?

NI HAKI YAKE TENA YA KIKATIBA KABISA HATA KUVUNJIWA YAI

Natania bana usije ukanimind bure
 
Kuna habari kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ameshambuliwa na 'watu wasiojulikana' jijini Dodoma alipokuwa akirejea nyumbani kwake usiku wa kuamkia jana. CHADEMA, kupitia kwa Katibu Mkuu wake John Mnyika, wakatoa taarifa ya awali kwa umma juu ya shambulio hilo la Mwenyekiti na kingozi wao huyo wa juu kabisa kwenye chama chao.

Nilipata faraja nilipokuona Kamanda Muroto ukijitokeza mbele ya wanahabari na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kutoa kauli ya Jeshi la Polisi mkoa wa Dodoma kuhusu shambulio la Mbowe. Kwa umakini na ustadi mkubwa Kamanda Muroto ukauambia umma wa watanzania mambo makubwa matatu. Kwanza, uchunguzi dhidi ya tukio hilo umeanza na unafanywa na jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama.

Pili, tukio la Mbowe lisitumike kisiasa na kama mtaji wa kisiasa na yeyote. Na tatu, ni kupiga marufuku mtu yeyote kulizungumzia jambo hilo kwa minajiri ya kuingilia uchunguzi wa kipolisi. Nilikuelewa sana. Nilitamani na ninatamani kuona ukisimamia kauli zako juu ya shambulio dhidi ya Mbowe. Nikupe taarifa au nikukumbushe kama tayari unajua kuwa jana Bungeni Mbowe alikuwa gumzo kwenye mjadala wa kupitisha Azimio la kumpongeza Rais Magufuli.

Kiti cha Spika wa Bunge kikikaliwa na Job Ngugai mwenyewe kiliruhusu mjadala wa tukio la shambulizi la Mbowe. Wachangiaji walipangwa kimkakati ili kutimiza azma yao. Kuanzia kwa Spika Ndugai, Silinde, Lijualikali, Musukuma na hata Lusinde, wote walikejeli tukio hilo na kulihusianisha na ulevi. Walihitimisha kwa kusema kuwa Mbowe alikuwa amelewa na aliteleza kwenye ngazi zake na kuvunja/kutegua mguu wake. Tena akiwa na 'kimada'.

Wabunge hao niliowataja walikebehi na kumkejeli vya kutosha Mbowe na kulikejeli shambulo lake. Tayari wameshaingilia na kuvuruga uchunguzi wa Polisi kwenye tukio hilo. Wanaachwaje bila ya kukamatwa katika kutekeleza kauli ya kamanda Muroto? Wanaopaswa kukamatwa ni Spika Ndugai na Wabunge Silinde, Lusinde, Musukuma na Lijualikali. Wameshaingilia uchunguzi wa Polisi. Wameshakiuka marufuku ya Muroto.

Tunajua kuwa Mbowe anaponzwa na Lissu. Ukifika muda tutayasema yote. Kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2020. Kwanza tumalize hili la Mbowe.

RIP Pierre Nkurunzinza, mwanamichezo uliyeichezea hadi katiba na sheria!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)

RIP Pierre Nkurunzinza, mwanamichezo uliyeichezea hadi katiba na sheria!.
Ujumbe maridhawa.
 
Back
Top Bottom