Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,362
- 48,879
Shambulio la alfajiri ya leo, la jeshi la Israel, tunaambiwa limehusisha ndege 100. Ndege zimeshambulia, na zote zimerudi salama. Ina maana, jeshi la Iran limeshindwa kudungua hata ndege moja ya Israel. Jambo kama hilo la kwenda kumshambulia adui yako kwa ndege, sidhani kama Iran inaweza kuthubu kulifanya.
Hata kule Lebanon, mashambulio mengi yamekuwa ya kutumia ndege, nako haijawahi kusikika Hezbollah kufanikiwa kuangusha hata ndege moja.
Hata ule mwezi April, Israel ilipoishambulia Iran, ilitumia ndege, na kuteketekeza mtambo mmoja wa ulinzi wa anga wa Iran (Iran kwa aibu ikasema walitumia drones ili kuficha udhaifu wa jeshi lake - ilikuwaje ndege iingie kwenye anga lake, ishambulie na kurudi salama).
Shambulio la alfajiri ya leo, Israel inasema lilikuwa ni kwa vituo vya shughuli za kijeshi pekee, na ilikuwa ni precise strike. Hii inatupa ujumbe. kuwa kama Hezbollah na Hamas wasingekuwa wanafanya ule ushetani wa kujificha katikati ya nraia au kuishambulia Israel kutokea kwenye makazi au shughuli za kiraia, kusingekuwa na mauaji ya raia ya kiwango tulichoshuhudia Gaza au Lebanon.
Kwa sababu vituo vya shughuli za kijeshi vya Iran vimejitenga na makazi na shughuli za kiraia, precise targeting ya IDF kwa vituo vya shughuli za kijeshi nchini Iran, havijaleta madhara yoyote kwa raia wa kawaida.
Ni vema Dunia ikaweka mwongozo na sheria kali kuharamisha shughuli zozote za kijeshi kutokea kwenye makazi au shughuli za kiraia. Kitendo wanachokifanya Hamas na Hezbollah, cha kujificha katikati ya watoto, akina mama na raia ni cha kishetani kinacholenga kuwaangamiza raia. Ikitokea hawa magaidi wanaweka miundombinu yao katikati ya makazi ya kiraia, raia waruhusiwe kuyakimbia maeneo hayo. Tunaambiwa huko Gaza, Hamas wakiweka miundombinu ya kijeshi kwenye nyumba yako au karibu na makazi yako, ukitaka kuhama hilo eneo, wanakuua. Jambo hili siyo halali hata kidogo.
ALjAZEERA
Hata kule Lebanon, mashambulio mengi yamekuwa ya kutumia ndege, nako haijawahi kusikika Hezbollah kufanikiwa kuangusha hata ndege moja.
Hata ule mwezi April, Israel ilipoishambulia Iran, ilitumia ndege, na kuteketekeza mtambo mmoja wa ulinzi wa anga wa Iran (Iran kwa aibu ikasema walitumia drones ili kuficha udhaifu wa jeshi lake - ilikuwaje ndege iingie kwenye anga lake, ishambulie na kurudi salama).
Shambulio la alfajiri ya leo, Israel inasema lilikuwa ni kwa vituo vya shughuli za kijeshi pekee, na ilikuwa ni precise strike. Hii inatupa ujumbe. kuwa kama Hezbollah na Hamas wasingekuwa wanafanya ule ushetani wa kujificha katikati ya nraia au kuishambulia Israel kutokea kwenye makazi au shughuli za kiraia, kusingekuwa na mauaji ya raia ya kiwango tulichoshuhudia Gaza au Lebanon.
Kwa sababu vituo vya shughuli za kijeshi vya Iran vimejitenga na makazi na shughuli za kiraia, precise targeting ya IDF kwa vituo vya shughuli za kijeshi nchini Iran, havijaleta madhara yoyote kwa raia wa kawaida.
Ni vema Dunia ikaweka mwongozo na sheria kali kuharamisha shughuli zozote za kijeshi kutokea kwenye makazi au shughuli za kiraia. Kitendo wanachokifanya Hamas na Hezbollah, cha kujificha katikati ya watoto, akina mama na raia ni cha kishetani kinacholenga kuwaangamiza raia. Ikitokea hawa magaidi wanaweka miundombinu yao katikati ya makazi ya kiraia, raia waruhusiwe kuyakimbia maeneo hayo. Tunaambiwa huko Gaza, Hamas wakiweka miundombinu ya kijeshi kwenye nyumba yako au karibu na makazi yako, ukitaka kuhama hilo eneo, wanakuua. Jambo hili siyo halali hata kidogo.
ALjAZEERA