Shangazi Fatma Karume afika mbele ya kikosi kazi kutoa maoni yake kuhusu mambo ya katiba na mengineyo

Shangazi Fatma Karume afika mbele ya kikosi kazi kutoa maoni yake kuhusu mambo ya katiba na mengineyo

Tena haraka sana maana wanatumia kodi tulizolipa , zoezi hili linatakiwa kuwa live mubasgara TBC na vituo vingine vya televisheni vya binafsi pia online tujue zoezi hili muonendo wake ni kwa manufaa ya wananchi wote au ni kwa ajili ya kakikundi cha watu wachache wa chama fulani na siyo kwa manufaa ya taifa letu na raia wote bila kujali vyama vya siasa.
Tatzo kuna masuala watachakachua ili impendeze Maza kinyume na matakwa ya wananchi
 
kuna mtu hapo kaahidiwa kazi kwenye kikosi kazi kwa miaka 9 hadi 2030 ila 2025 anautaka U Rais...maajabu sana
 
Mwanadada mpigania haki za binadamu na demokrasia nchini, amefika mbele ya kikozi kazi cha mheshimiwa rais kwa ajili ya kutoa maoni yake namna gani ya kupata tume huru ya uchaguzi, namna gani kufanya siasa safi nchini na katiba mpya.

View attachment 2223143
Nendeni mkajadkliane, mkisha kubaliana mtuletee na SISI tuyaangalie tuone kama yanafaa. (in voice of chief Hangaya) HAKUNA KITU HAPO
 
Mwanadada mpigania haki za binadamu na demokrasia nchini, amefika mbele ya kikozi kazi cha mheshimiwa rais kwa ajili ya kutoa maoni yake namna gani ya kupata tume huru ya uchaguzi, namna gani kufanya siasa safi nchini na katiba mpya.

View attachment 2223143
Huyo bibi wa pembeni anavyomkata jicho la husda atakua mchawi tu kama huyo wa pembeni yake.
 
Kamisheni ya Haki za Binaadamu ya UN yatua nchini; hiki ndio wanachofanya kufuatilia ahadi ilizotoa Tanzania, pia serikali yabanwa na UN kuwa iwe wazi waTanzania wafahamu serikali yao iliridhia nini ktk masuala 252 iliyosaini na kuikubali kwa niaba ya wananchi

MAONI YA MABADILIKO YA KATIBA MPYA YANAYOWASILISHWA MBELE YA KIKOSI KAZI YANATAKIWA KUWA MUSHASHARA / LIVE , HII NI HAKI YA MSINGI KWA RAIA
 
Swali Kuu kwa Kikosi Kazi cha Mabadiliko ya Katiba

13 May 2022

Rais Samia Suluhu Hassan anauliza je watanzania wanaijua haki yao, na vilevile elimu kwa umma imefanyika ? Bila kusahau Uwazi yaani transparency amesisitiza Rais.

 
Ile kamati ya mzee Warioba na wenzake ilivyokuwa inaundwa kufanya Mambo ya kikatiba,tuliona Bunge likibadiri na kupitisha sheria mbali mbali ili kuipa ile kamati nguvu za kisheria kufanya kazi zake..
Lilivyokuwa linaundwa Bunge la katiba kulikuwa na utungaji na upitishwaji wa sheria ili kulipa uhalali wa kisheria lile Bunge kufanya kazi zake.
Kilichonishangaza kwenye hii kamati Ni jinsi ilivyoibuka ghafla kwa tamko la mtu mmoja,tena mbaya zaidi walivyotoa taarifa ya kwanza Kama walivyokuwa wamepewa maelekezo,mwenye kamati akafurahi na kuwaongezea muda wa miaka 9 ya kufanya kazi hiyo hiyo
Ninajiuliza ndani ya hiyo miaka 9 hiyo kamati itakuwa inakusanya kitu gani kikubwa hivyo kisichoisha?
Pili,wanapata wapi uhalali wa kisheria kujishugulisha na Mambo ya kikatiba ?
Tatu,ule utaratibu wa kuipata tume ya Warioba na hatimae Bunge la katiba haukuwa utaratibu uliolazimishwa na sheria Bali ulikuwa utashi wa Rais aliyeko madarakani kiasi kwamba kila Rais aliyeko madarakani aweza tumia utashi wake binafsi juu ya kufanikisha Jambo Hilo Hilo moja?
Kwa hiyo kwangu Mimi mhimu siyo maoni yanayotolewa na hao wanaoitwa wadau kuwa Live kwenye TV, Bali hao wanaoongoza huo mchakato wana uhalali gani kisheria?
 
Aisee..
Hivi vita ya Ukraine imefanya kila mtu anaonekana kachoka na kuzeeka.....

1652474459942.png
 
Delaying tactics.CCM is buying time so that they continue to have more cake.It's very unfortunate for Tanzanians.

Jumuiya ya kimataifa ina iangalia na kufuatilia mwenendo wa Tanzania chini ya awamu 6 kwa karibu sana kuona kama utawala wa sasa una hila na hadaa au inasema na kutenda vile ilivyoridhia masuala 252 mbele ya wadau wa maendeleo Geneva Uswisi kuhusu haki.
 
Yaani sura ya zitto imekaa kama jambazi hivi makovu kibao yaani mwami sijui yukoje
 
Ushasema hayana akili unategemea yatajihoji hizo pesa za umma wanazochezea?

Halafu watafunga safari kwenda kukopa fedha za kulihonga hilo genge la Mukandara; huku wakidanganya kuwa ni fedha za kuthibiti mfumuko wa bei!!
 
Huyu mdada si ndiye alienda mahakamani akafanya utetezi kwa kutumia sheria iliyokuwa imeshafutwa tayari? Au labda namfananisha!
 
Ivi hawa wajumbe wa icho KKK wana lamba bei gani kila wakutanapo ?
 
Nilikuwa nategemea kitu kama hiki kutokana na ukimya wake wa hivi karibuni. Kwenye misimamo Maria amemshinda kwa mbali.

Amandla...
Wanachokifanya Zitto na Fatma Karume ni kitu kisicho na mantiki

Niweke wazi, kwenda kutoa maoni, aina ya maoni ni haki yao na isihojiwe na mtu yoyote

Tatizo ni hili, walitakiwa wajiulize;
Maoni ya Wananchi kupitia tume ya Mzee Warioba yanamatatizo gani?
Kikosi kazi kimeundwa kwa utaratibu gani wa katiba?
Tatu, nani anahakiki maoni yanayotolewa yapo kwenye rekodi?

Kikosi kazi kilisema katiba isubiri.2025. kwa Mujibu wa Prof Lipumba aliyekuwa ndani kama Zitto hayakujadiliwa.

Mwisho wa siku 'uzushi' ukaingizwa katika ripoti na kujenga uhalali, vyama vimesema hadi 2025
Zitto anajua huu ni uharamia kwasababu hakuweza kudhibiti wala kukemea uongo huo.

Fatma anakwenda kujenga uhalali akijua maoni yake hayawezi kuwekwa katika mizani sawa na maoni yaliyotengenezwa tayari yanayotafutiwa majibu

Mwisho Fatma atajikuta analalama kama ambavyo Lipumba analalama lakini bila kufanya lolote

Kuwemo katika kikosi kazi au kutoa maoni katika kikosi kazi ni kujenga ''legitimacy' ya kikozi kazi ambayo ni utapeli tu wakati huo huo waki deligitimize maoni ya Wananchi kupitia Warioba

Nitashangaa sana nitakapomsikia Fatma akizungumzia tena Katiba! yeye keshaungana na wasiotaka kwa kuwajengea uhalali na uwezo wa kuendelea. Fatma , Zitto katika boti moja

Jiulize kwanini Msajili anatoa hiyo picha! kuna hoja hapo itakayotumiwa na Fatma ni sehemu yake

JokaKuu Tindo
 
Wanachokifanya Zitto na Fatma Karume ni kitu kisicho na mantiki

Niweke wazi, kwenda kutoa maoni, aina ya maoni ni haki yao na isihojiwe na mtu yoyote

Tatizo ni hili, walitakiwa wajiulize;
Maoni ya Wananchi kupitia tume ya Mzee Warioba yanamatatizo gani?
Kikosi kazi kimeundwa kwa utaratibu gani wa katiba?
Tatu, nani anahakiki maoni yanayotolewa yapo kwenye rekodi?

Kikosi kazi kilisema katiba isubiri.2025. kwa Mujibu wa Prof Lipumba aliyekuwa ndani kama Zitto hayakujadiliwa.

Mwisho wa siku 'uzushi' ukaingizwa katika ripoti na kujenga uhalali, vyama vimesema hadi 2025
Zitto anajua huu ni uharamia kwasababu hakuweza kudhibiti wala kukemea uongo huo.

Fatma anakwenda kujenga uhalali akijua maoni yake hayawezi kuwekwa katika mizani sawa na maoni yaliyotengenezwa tayari yanayotafutiwa majibu

Mwisho Fatma atajikuta analalama kama ambavyo Lipumba analalama lakini bila kufanya lolote

Kuwemo katika kikosi kazi au kutoa maoni katika kikosi kazi ni kujenga ''legitimacy' ya kikozi kazi ambayo ni utapeli tu wakati huo huo waki deligitimize maoni ya Wananchi kupitia Warioba

Nitashangaa sana nitakapomsikia Fatma akizungumzia tena Katiba! yeye keshaungana na wasiotaka kwa kuwajengea uhalali na uwezo wa kuendelea. Fatma , Zitto katika boti moja

Jiulize kwanini Msajili anatoa hiyo picha! kuna hoja hapo itakayotumiwa na Fatma ni sehemu yake

JokaKuu Tindo

Uko sahihi kabisa, hiki kikosi waliokitengeneza wanajifanya wana nia njema, lakini lengo lao ni kuhalalisha majibu waliyonayo tayari. Na hapo walipo wanajitahi watu wenye kupaza sauti zao wafike kwenye hicho kikosi kazi ili kuhalalisha lengo lao.
 
Back
Top Bottom