CHADEMA hawawezi kupata kura za kundi lolote lile katika jamii lenye akili Timamu na linalojitambua.kwa sababu CHADEMA ni genge na mkusanyiko wa watu wasio na busara wala hekima wala adabu. Ni watu wanaofanya vitu kama vipofu na ndio maana chama kimekosa nuru na muelekeo kwa kuwa kinaongozwa na vipofu ambao akili zao zinawaza madaraka na vyeo tu. CHADEMA wapo tayari kushirikiana hata na shetani ilimradi wapate madaraka. CHADEMA wapo tayari kulipasua Taifa kwa Udini ,ukabila ,ukanda na hata kuchochea machafuko hapa nchini ilimradi wao wapate madaraka na vyeo.
Watanzania tunapaswa kuwapuuza CHADEMA na kuwakemea kabla hawajaharibu Taifa letu. Tuwakatae kwa nguvu zetu zote .kamwe tusiwaunge mkono kwa lolote lile .tuwaogope CHADEMA kama ukoma maana hawana dhamira njema na Taifa letu.