Naanto Mushi
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 6,236
- 15,677
Biashara ya kutoa mikopo ni biashara kama biashara nyingine. Unavyouza mikopo Zaidi ndivyo unavyopata faida Zaidi.
Kwa nchi zilizoendelea kama Marekani, mataifa ya Ulaya, Japan, na hata China, hizi ni nchi ambazo zimefanikiwa kuwa na efficiency kubwa sana kwenye mabenki, na pia benki kuu katika nchi hizo kwa ndani ya miaka 15 iliyopita, walikuwa na sera ambazo zilipelekea interest rates (au kiwango cha riba) kwenye hizo nchi, kuwa chini sana.
Matokeo yake ni kwamba, benki, investors na wakopeshaji wengi sana wa hizi nchi tajiri, wamekuwa ni kama wana struggle kwenye kutengeneza faida ndani ya masoko yao, hususani kwasababu, cost of funds ni ndogo lakini pia lending costs ni ndogo, kwahiyo wamekuwa wakitengeneza ‘a very thin margin’ kwenye mikopo ndani ya nchi zao, kitu ambacho kwa investors huwa hakifurahishi.
Kwahiyo trick ikawa ni kwamba, hizi nchi tajiri ikabidi wa dizaini namna ya kuwabambika mikopo nchi maskini the likes of Zambia, Tanzania, Kenya nk. Kwasababu kama nilivosema kwenye utangulizi wangu, biashara ya mikopo, ni kama biashara nyingine, unavyouza mikopo zaidi ndo unavyozidi kutengeneza pesa zaidi.
Na kwa kutumia taasisi hizo hizo zao kwenye assessment ya credit ratings, imejikuta kwamba kumejengeka mfumo wa kuhakikisha kwamba risk profile ya mataifa mengi maskini inakuwa juu sana, ili basi hata riba ya mikopo ambayo watapewa pia itakuwa ni kubwa.
Mikopo inayofubaza uchumi – mikopo isiyoelekezwa kwenye matumizi yenye tija
Kikubwa ni kwamba, hizi taasisi za kifedha za nchi tajiri, wanataka kuhakisha kwamba, mikopo mingi ambayo nchi masikini watakopa, basi isiweze kulipika daima, ili kwamba iwe ni kama vile Ng’ombe unayemkamua maziwa kila siku.
Kwa hivo basi, nchi maskini zimekuwa zikijikuta zina finance miradi ambayo ‘payoff’ yake ni ndogo iki maanisha kwamba, mradi husika unaweza kuwa na impact ndogo kwenye uchumi kitu ambacho kitapelekea kukosekana kwa cash flow ya kulipa hiyo mikopo husika.
Lakini ni kama pia kuna agenda ambayo huwa inajificha kwenye hii mikopo ya kimataifa. Ni kwanini mikopo ambayo huwa inalenga mambo ya kipuuzi huwa inakuwa inatolewa haraka haraka sana? Na ile ambayo ina maslahi mapana nay a muda mrefu huwa inapigwa danadana?
Ukijijibu hayo maswali vizuri, utakuja kuona kwamba, hizi taasisi huwa hazina malengo ya kuona kwamba uchumi wa hizi nchi unaboreka, ndio maana kuna mikopo serikali inapata kwa haraka haraka na ukiangalia matumizi yake unaona ni matumizi ya kipumbavu kabisa.
Zaidi zaidi nadhani hii ni aina mpya ya ukoloni mamboleo kwa kutumia taasisi za kifedha za kimataifa kuhakikisha kwamba wanawalewesha na kufubaza maendeleo ya hizi nchi kupitia mikopo ya kinyonyaji, kwasababu ni mikopo isiyolipika, yenye riba kubwa, na ambayo inabeba systemic risks za kuangusha hata mfumo mzima wa uchumi wa nchi husika – ukiangalia kinachowakuta Ghana kwa sasahivi.
Inavoonekana ni kwamba pia Tanzania, hatuwezi kujikwepa na huu mtego, tayari tupo kwenye ile debt trap, maana kwa miaka saba iliyopita nchi imeongeza deni kwa karibu USD 12 billion (TZS 27 Trillioni) ambazo mimi binafsi ukiniuliza zilipokwenda, bado ntachelea kukupa majibu.
External debt stock as per BOT
December 2015 – USD 15,408 millions
October 2022 – USD 27,482 millions
Changes between Dec 2015 to Oct 2022 = USD 12,074 millions
Watu wengi wanasema ‘Tanzania bado haipo kwenye high risk category na deni ni stahimilivu kwa just kuangalia tu upande wa debt to GDP ratio’ lakini ukiangalia kwenye upande wa ‘cash flow’ iliyopo ambayo ni kodi na tozo za kila uchao na projected cash flow ya hivi vilivyoombewa mikopo ambayo mimi naona bado ni dhaifu, huwezi kuona huo ustahimilivu ulipo.
Nawaachia swali serikali, ‘pesa unayokopa unaifanyia nini?’ hilo swali nadhani ndio tungependa kuskia bunge likijadili kabla ya serikali kwenda kukopa, vinginevyo naona hizi deal zinafanyika kimya kimya na wizara ya fedha, naona kila kukicha kwa miaka 7 iliyopita wapo busy kila siku wakisaini mikataba ya kukopeshwa mabilioni lakini hawataki kutujibu hilo swali, wanafanyia nini mikopo? Je unakopa ulipe mishahara? Je unakopa ili ulipe madeni?
Ni hayo tu.
N.Mushi
Kwa nchi zilizoendelea kama Marekani, mataifa ya Ulaya, Japan, na hata China, hizi ni nchi ambazo zimefanikiwa kuwa na efficiency kubwa sana kwenye mabenki, na pia benki kuu katika nchi hizo kwa ndani ya miaka 15 iliyopita, walikuwa na sera ambazo zilipelekea interest rates (au kiwango cha riba) kwenye hizo nchi, kuwa chini sana.
Matokeo yake ni kwamba, benki, investors na wakopeshaji wengi sana wa hizi nchi tajiri, wamekuwa ni kama wana struggle kwenye kutengeneza faida ndani ya masoko yao, hususani kwasababu, cost of funds ni ndogo lakini pia lending costs ni ndogo, kwahiyo wamekuwa wakitengeneza ‘a very thin margin’ kwenye mikopo ndani ya nchi zao, kitu ambacho kwa investors huwa hakifurahishi.
Kwahiyo trick ikawa ni kwamba, hizi nchi tajiri ikabidi wa dizaini namna ya kuwabambika mikopo nchi maskini the likes of Zambia, Tanzania, Kenya nk. Kwasababu kama nilivosema kwenye utangulizi wangu, biashara ya mikopo, ni kama biashara nyingine, unavyouza mikopo zaidi ndo unavyozidi kutengeneza pesa zaidi.
Na kwa kutumia taasisi hizo hizo zao kwenye assessment ya credit ratings, imejikuta kwamba kumejengeka mfumo wa kuhakikisha kwamba risk profile ya mataifa mengi maskini inakuwa juu sana, ili basi hata riba ya mikopo ambayo watapewa pia itakuwa ni kubwa.
Mikopo inayofubaza uchumi – mikopo isiyoelekezwa kwenye matumizi yenye tija
Kikubwa ni kwamba, hizi taasisi za kifedha za nchi tajiri, wanataka kuhakisha kwamba, mikopo mingi ambayo nchi masikini watakopa, basi isiweze kulipika daima, ili kwamba iwe ni kama vile Ng’ombe unayemkamua maziwa kila siku.
Kwa hivo basi, nchi maskini zimekuwa zikijikuta zina finance miradi ambayo ‘payoff’ yake ni ndogo iki maanisha kwamba, mradi husika unaweza kuwa na impact ndogo kwenye uchumi kitu ambacho kitapelekea kukosekana kwa cash flow ya kulipa hiyo mikopo husika.
Lakini ni kama pia kuna agenda ambayo huwa inajificha kwenye hii mikopo ya kimataifa. Ni kwanini mikopo ambayo huwa inalenga mambo ya kipuuzi huwa inakuwa inatolewa haraka haraka sana? Na ile ambayo ina maslahi mapana nay a muda mrefu huwa inapigwa danadana?
Ukijijibu hayo maswali vizuri, utakuja kuona kwamba, hizi taasisi huwa hazina malengo ya kuona kwamba uchumi wa hizi nchi unaboreka, ndio maana kuna mikopo serikali inapata kwa haraka haraka na ukiangalia matumizi yake unaona ni matumizi ya kipumbavu kabisa.
Zaidi zaidi nadhani hii ni aina mpya ya ukoloni mamboleo kwa kutumia taasisi za kifedha za kimataifa kuhakikisha kwamba wanawalewesha na kufubaza maendeleo ya hizi nchi kupitia mikopo ya kinyonyaji, kwasababu ni mikopo isiyolipika, yenye riba kubwa, na ambayo inabeba systemic risks za kuangusha hata mfumo mzima wa uchumi wa nchi husika – ukiangalia kinachowakuta Ghana kwa sasahivi.
Inavoonekana ni kwamba pia Tanzania, hatuwezi kujikwepa na huu mtego, tayari tupo kwenye ile debt trap, maana kwa miaka saba iliyopita nchi imeongeza deni kwa karibu USD 12 billion (TZS 27 Trillioni) ambazo mimi binafsi ukiniuliza zilipokwenda, bado ntachelea kukupa majibu.
External debt stock as per BOT
December 2015 – USD 15,408 millions
October 2022 – USD 27,482 millions
Changes between Dec 2015 to Oct 2022 = USD 12,074 millions
Watu wengi wanasema ‘Tanzania bado haipo kwenye high risk category na deni ni stahimilivu kwa just kuangalia tu upande wa debt to GDP ratio’ lakini ukiangalia kwenye upande wa ‘cash flow’ iliyopo ambayo ni kodi na tozo za kila uchao na projected cash flow ya hivi vilivyoombewa mikopo ambayo mimi naona bado ni dhaifu, huwezi kuona huo ustahimilivu ulipo.
Nawaachia swali serikali, ‘pesa unayokopa unaifanyia nini?’ hilo swali nadhani ndio tungependa kuskia bunge likijadili kabla ya serikali kwenda kukopa, vinginevyo naona hizi deal zinafanyika kimya kimya na wizara ya fedha, naona kila kukicha kwa miaka 7 iliyopita wapo busy kila siku wakisaini mikataba ya kukopeshwa mabilioni lakini hawataki kutujibu hilo swali, wanafanyia nini mikopo? Je unakopa ulipe mishahara? Je unakopa ili ulipe madeni?
Ni hayo tu.
N.Mushi