Sheikh Jongo asema ujenzi wa msikiti wa Kinondoni haukuombwa na Hayati Magufuli kama ilivyodaiwa

Na huo ndio ukweli mchungu !
 
Basi ni vema wakae kimya hata baada ya umauti wake, je uislam unataka unafiki?
Sio unafiki. Ni ukweli . Unafiki pale hapo mwanzo wangalikua BAKWATA wamesema hadharani kama kajenga magufuli lkn wao walikaa kimya..hivi sasa taifa linapewa taarifa
 
Nashangaa mnazidi kupambana na marehemu.
 
Kwa nini hawakuyasema msukuma akiwa hai, kama wao ni vidume! Wanafiki wakubwa, walijichekesha tu kama demu kaona iphone 15! Nguruwe poli
 
Kwenye uislamu tunaamini misikiti yote ni ya Allah.

As long as unaswaliwa na waislamu hayo mengine hayana haja ya kujua.
Kwahiyo huyu Sheikh Jongo sio Muislam mpaka akanushe ukweli au ajadili kuhusu Msikiti?
 
Waislam huwa wanapenda sana Ubishi na Ushindani wa kitoto...sasa anachokisema Huyu Sheikh kina umuhimu gani?

Kama aliomba JPM au JMK so What?

Ni kama Wanavyopendaga kusema kuwa wao wapo wengi kuliko Wakristo nchi hii
 
Huyo

Ipo siku mtamruka hadi Mkapa kwenye majengo ya MMU sijui MUM!
Hao ni wanafiki, na wameambiwa wasema hivyo na watu Fulani hivi ambao, wanamchafua JPM. Kwanza sisi tuliosoma CUBA, unaanza unatafakari, unajiuliza. Hivi, inakuaje Sheikh huyu aanze tu kusema hayo maneno?Je, Sheikh alikuwa na ugomvi na JPM? Jibu ni hapana.Je, kwann, Sheikh akusema kipindi JPM yupo? Okay, labda alimwogopa Rais. Kwann ha kusema miaka yote mitatu toka JPM afariki? Alikuwa anasubiri nn?? Je, kama ni JK aliomba huo msaada,, mbona haikutangazwa kwenye vyombo vya habari? Je, JK aliomba huo msaada alipokwenda Morocco au Mfalme alipokuja? Hii, inasikitisha sana kuona vitu vidogo na vya hovyo, vinapandikizwa kwa viongoz wetu wa dini.Tumeona picha za Mfalme wa Morocco akiwa ziarani Tanzania na Rais Magufuli. Tunaomba pia picha za Kikwete akiwa ziarani na Kikwete. Pia, napenda kuwakumbusha watanzania, kuwa tuepuke mitego ya wapumbavu wachache wanaotaka kutuvuruga eti kisa ujenz wa msikiti. Miaka ya nyuma, Tanzania ilipigana vita na Uganda. Uganda ya marehemu Idd Amin. Majeshi ya Libya yaliingia vitani kuisadia Uganda. Ushupavu wa JWT ulifanikisha kuwateka askari wengi sana wa kiarabu kutoka Libya. Lakin, Mwalimu JK Nyerere aliwarudisha kwa huko Libya. Gaddafi Rais wa Libya, hakuamin kilichotokea kwa Nyerere kuwarudisha nyumba na bila kuwajeruhi askari wake. Gadaffi, alikuja kumpenda sana Mwalimu Nyerere na wakawa marafiki. Ikifika kipindi mwalimu alimuomba Gaddafi ajenge msikiti wa waislamu pale Butiama. Na kweli Gaddafi ali Jenga msikiti wa waislamu na Kanisa pale Butiama. Watanzania sisi ni ndugu, tusikosane kwa vitu vidogo, vinavyoanzishwa na wapumbavu wachache.
 
Haya Ok.. tumekubali.. hakuwafanyia lolote alijisingizia tu
 
Ndugu Zangu Katika Imani Tuache Unafk Mwezi Huu
Jiwe Akiwa Hai Alisema Wazii AliwAombe Mjengewe Msikiti
 
Magufuli Sa hizi anagekwa na kila mtu, hii nchi hii
Ni wakati utatujia sote.

Ukikata pumzi dunia hii na lako limeisha,inasikitisha sana kama hadi kiongozi wa kidini anasimama ndani ya nyumba ya kumuabudu Mungu wake anadanganya umma kiasi hiko.
 
huo ni unafiki kwanini hakusema wakati magufuli yupo hatuwezi kusikiliza maneno ya upande mmoja tu kama kwenye kanga angesema na magufuli yupo ili tusikie naye atasemaje hapo mzee umefeli pakubwa sanaaaaaaaaaa
Uwe unasikikiza mpaka na kudadisi kabla haujaonekana humu. Hilo ni swali kaulizwa na muumini wake na hilo ndo jibu alilopewa. Kwani hata angekuwepo ingeondoa uhalisia kwani? Jamaa hana mkono wala ushawishi wake kwenye ujenzi wa huo msikiti. Jikaze tu hata kama unaumia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…