Sheikh Jongo asema ujenzi wa msikiti wa Kinondoni haukuombwa na Hayati Magufuli kama ilivyodaiwa

Sheikh Jongo asema ujenzi wa msikiti wa Kinondoni haukuombwa na Hayati Magufuli kama ilivyodaiwa

Mwamba kakaa madarakani kwa miaka 6 tu ila ameacha kazi sana nyuma yake. Imeshapita miaka mitatu tangu kifo chale lakini kila kukicha watu wanahangaika kufuta kazi zake.
Kikwete kakaa madarakani miaka 10 huo Msikiti hakuomba wala haikujulikana.
Kumbukumbu itawekwa misikitini na kwenu mnaopambana na aliyekufa.
Lakini historia itabaki katika kumbukumbu kwa maandishi na video za wakati wa uhai wake.
Na huo ndio ukweli mchungu !
 
Basi ni vema wakae kimya hata baada ya umauti wake, je uislam unataka unafiki?
Sio unafiki. Ni ukweli . Unafiki pale hapo mwanzo wangalikua BAKWATA wamesema hadharani kama kajenga magufuli lkn wao walikaa kimya..hivi sasa taifa linapewa taarifa
 
Nashangaa mnazidi kupambana na marehemu.
 
Dunia haina siri, waislamu wamefunguka kwamba ule msikiti ambao JPM alikuwa anatamba kuwaombea waislamu wajengewe kumbe ni kazi iliyoanza enzi ya JK mpaka Mufti akasafiri kwenda kwa nchi iliyofadhili ili wakajadiliane.

Iwe bhojo!

Kwa nini hawakuyasema msukuma akiwa hai, kama wao ni vidume! Wanafiki wakubwa, walijichekesha tu kama demu kaona iphone 15! Nguruwe poli
 
Kwenye uislamu tunaamini misikiti yote ni ya Allah.

As long as unaswaliwa na waislamu hayo mengine hayana haja ya kujua.
Kwahiyo huyu Sheikh Jongo sio Muislam mpaka akanushe ukweli au ajadili kuhusu Msikiti?
 
Waislam huwa wanapenda sana Ubishi na Ushindani wa kitoto...sasa anachokisema Huyu Sheikh kina umuhimu gani?

Kama aliomba JPM au JMK so What?

Ni kama Wanavyopendaga kusema kuwa wao wapo wengi kuliko Wakristo nchi hii
 
Huyo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 28 Februari, 2020 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Msikiti mkubwa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) unaojengwa Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
U sjj
Msikiti huo unajengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohammed VI wa Morocco baada ya kuombwa na Mhe. Rais Magufuli alipofanya ziara rasmi hapa nchini Oktoba 2016.

Akiongozwa na Mufti wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zubeir bin Ally, Mhe. Rais Magufuli amejionea kazi za ukamilishaji wa jengo jipya la Msikiti na jengo la ofisi ya Taasisi ya Mfalme Mohammed VI wa Morocco zikiendelemilishwa, na ameelezea kufurahishwa kwake na ubora na uzuri wa Msikiti huo.

Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mfalme Mohammed VI wa Morocco kwa kutekeleza ombi alilomuomba la kuwajengea Waislamu Msikiti mkubwa kuliko yote hapa nchini, na amempongeza Mufti wa Tanzania na Waislamu wote kwa kujengewa nyumba nzuri ya Ibada.

Mufti wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zubeir bin Ally amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwajali Waislamu na kuwaombea msaada wa kujengewa Msikiti huo ambao ujenzi wake umefikia asilimia 97.

Akiwa na viongozi wenzake wa BAKWATA, Sheikh Mkuu Aboubakar Zubeir bin Ally ameongoza Dua ya kumuombea Mhe. Rais Magufuli na kuliombea Taifa ili Mwenyezi Mungu aiepushe Tanzania dhidi ya maradhi ya homa ya virusi vya corona, kudumisha amani na utulivu na kuombea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu ufanyike vizuri na kwa amani.

Ipo siku mtamruka hadi Mkapa kwenye majengo ya MMU sijui MUM!
Hao ni wanafiki, na wameambiwa wasema hivyo na watu Fulani hivi ambao, wanamchafua JPM. Kwanza sisi tuliosoma CUBA, unaanza unatafakari, unajiuliza. Hivi, inakuaje Sheikh huyu aanze tu kusema hayo maneno?Je, Sheikh alikuwa na ugomvi na JPM? Jibu ni hapana.Je, kwann, Sheikh akusema kipindi JPM yupo? Okay, labda alimwogopa Rais. Kwann ha kusema miaka yote mitatu toka JPM afariki? Alikuwa anasubiri nn?? Je, kama ni JK aliomba huo msaada,, mbona haikutangazwa kwenye vyombo vya habari? Je, JK aliomba huo msaada alipokwenda Morocco au Mfalme alipokuja? Hii, inasikitisha sana kuona vitu vidogo na vya hovyo, vinapandikizwa kwa viongoz wetu wa dini.Tumeona picha za Mfalme wa Morocco akiwa ziarani Tanzania na Rais Magufuli. Tunaomba pia picha za Kikwete akiwa ziarani na Kikwete. Pia, napenda kuwakumbusha watanzania, kuwa tuepuke mitego ya wapumbavu wachache wanaotaka kutuvuruga eti kisa ujenz wa msikiti. Miaka ya nyuma, Tanzania ilipigana vita na Uganda. Uganda ya marehemu Idd Amin. Majeshi ya Libya yaliingia vitani kuisadia Uganda. Ushupavu wa JWT ulifanikisha kuwateka askari wengi sana wa kiarabu kutoka Libya. Lakin, Mwalimu JK Nyerere aliwarudisha kwa huko Libya. Gaddafi Rais wa Libya, hakuamin kilichotokea kwa Nyerere kuwarudisha nyumba na bila kuwajeruhi askari wake. Gadaffi, alikuja kumpenda sana Mwalimu Nyerere na wakawa marafiki. Ikifika kipindi mwalimu alimuomba Gaddafi ajenge msikiti wa waislamu pale Butiama. Na kweli Gaddafi ali Jenga msikiti wa waislamu na Kanisa pale Butiama. Watanzania sisi ni ndugu, tusikosane kwa vitu vidogo, vinavyoanzishwa na wapumbavu wachache.
 
Dunia haina siri, waislamu wamefunguka kwamba ule msikiti ambao JPM alikuwa anatamba kuwaombea waislamu wajengewe kumbe ni kazi iliyoanza enzi ya JK mpaka Mufti akasafiri kwenda kwa nchi iliyofadhili ili wakajadiliane.

Iwe bhojo!

Haya Ok.. tumekubali.. hakuwafanyia lolote alijisingizia tu
 
Ndugu Zangu Katika Imani Tuache Unafk Mwezi Huu
Jiwe Akiwa Hai Alisema Wazii AliwAombe Mjengewe Msikiti
 
Magufuli Sa hizi anagekwa na kila mtu, hii nchi hii
Ni wakati utatujia sote.

Ukikata pumzi dunia hii na lako limeisha,inasikitisha sana kama hadi kiongozi wa kidini anasimama ndani ya nyumba ya kumuabudu Mungu wake anadanganya umma kiasi hiko.
 
huo ni unafiki kwanini hakusema wakati magufuli yupo hatuwezi kusikiliza maneno ya upande mmoja tu kama kwenye kanga angesema na magufuli yupo ili tusikie naye atasemaje hapo mzee umefeli pakubwa sanaaaaaaaaaa
Uwe unasikikiza mpaka na kudadisi kabla haujaonekana humu. Hilo ni swali kaulizwa na muumini wake na hilo ndo jibu alilopewa. Kwani hata angekuwepo ingeondoa uhalisia kwani? Jamaa hana mkono wala ushawishi wake kwenye ujenzi wa huo msikiti. Jikaze tu hata kama unaumia
 
Back
Top Bottom