Sheikh mkuu mkoa wa Dar aonya maneno ya Lukuvi kutafsiriwa vibaya

Sheikh mkuu mkoa wa Dar aonya maneno ya Lukuvi kutafsiriwa vibaya

Sheikh mkuu wa mkoa wa dar es salaam amesema maneno ya mh lukuvi kutasfiriwa vibaya.ameonya waislamu kuwa waungwana na wasimwelewe vibaya lukuvi sbb hakuwa na nia mbaya,ni watu wachache au kikundi cha watu wenye nia ovu kutumia maneno ya lukuvi kisiasa na kiimani alisema sheikh.hi ni kwa mujibu wa magezeti asubuhi rfa



Mwambie aache kutumika!
 
Thanks mkuu, inasikitisha kuona mtu anaweka maslahi yake mbele kuliko kutetea Uislam.

Kaka suala hapa si kuutetea UISLAMU,hapa tatizo ni viongozi wetu wamekuwa waropokaji mno.Waathirika ni sisi wananchi wa kawaida ambao tunaishi vyema bila kujali dini zetu.

Sijaona sababu za msingi za Lukuvi kupanda madhabahuni nakuanza kufanya nasaha zisizokuwa na kichwa wala miguu.Na kwa mawazo yangu sababu huyu alienda kumwakilisha WM basi nina uhakika aliloliongea linabaraka ya serikali yetu sikivu.

Na mwsiho kaka yangu muda wote wanaoanzisha vita ni viongozi waliomadarakani.Hebu tuone Cetral Afrika kinachotokea leo,viongozi wamekimbilia ughaibuni wao na familia zao, wamewaacha raia wakiuana wenyewe kwa wenyewe kama kuku kwa sababu ya dini zao.Leo mashekhe na maaskofu ndiyo wanaopiga kwata kutafuta marithiano, na wakifanikiwa watakuja haraka kutaka kufanyika kwa UCHAGUZI,na waliokuwa wanauawa hawatadhaminiwa kamwe,dhamani yao ni kwenye KURA tu.

Tuwaone na hawa nchi changa zaidi Afrika South Sudan,nao ni yale yale waliopingana ni wanasiasa leo kiama kwa raia wa kawaida,masikini wasio na hata muelekeo wa kesho tutakuwa hai au lah,viongozi wamezikimbiza familia zao ughaibuni na wanasiasa wako busy kwenye 5STAR hotels wakifaidi maisha,wakibishana huku raia wakiteketea.

Leo Lukuvi anafanya yale yale yaliyofanywa na Viongozi wa Central Afrika na South Sudan,chama tawala,wanasheria,waandishi wahabari,kiongozi mkuu wa nchi,hawa wote wamenyamaza kimya wanasubiria bomu lipasuke wakimbilie ughaibuni wao na familia zao na raia tumalizane,vita ikiisha (Tukishamalizana)watarudi kuendelea kutawala.:shock::A S cry:😕
 
Huyu lazima afie korokoroni!

Kwani huyo Shekhe Ponda anatofauti gani na Lukuvi?Au huyu sababu ni Waziri kwenye chama chetu?Tuwe watu tunaomuogopa Mungu,haki lazima itendeke.Hata Lukuvi anastahili kufia korokoroni.Haijalishi wadhifa wake.
 
Kaka suala hapa si kuutetea UISLAMU,hapa tatizo ni viongozi wetu wamekuwa waropokaji mno.Waathirika ni sisi wananchi wa kawaida ambao tunaishi vyema bila kujali dini zetu.

Sijaona sababu za msingi za Lukuvi kupanda madhabahuni nakuanza kufanya nasaha zisizokuwa na kichwa wala miguu.Na kwa mawazo yangu sababu huyu alienda kumwakilisha WM basi nina uhakika aliloliongea linabaraka ya serikali yetu sikivu.

Na mwsiho kaka yangu muda wote wanaoanzisha vita ni viongozi waliomadarakani.Hebu tuone Cetral Afrika kinachotokea leo,viongozi wamekimbilia ughaibuni wao na familia zao, wamewaacha raia wakiuana wenyewe kwa wenyewe kama kuku kwa sababu ya dini zao.Leo mashekhe na maaskofu ndiyo wanaopiga kwata kutafuta marithiano, na wakifanikiwa watakuja haraka kutaka kufanyika kwa UCHAGUZI,na waliokuwa wanauawa hawatadhaminiwa kamwe,dhamani yao ni kwenye KURA tu.

Tuwaone na hawa nchi changa zaidi Afrika South Sudan,nao ni yale yale waliopingana ni wanasiasa leo kiama kwa raia wa kawaida,masikini wasio na hata muelekeo wa kesho tutakuwa hai au lah,viongozi wamezikimbiza familia zao ughaibuni na wanasiasa wako busy kwenye 5STAR hotels wakifaidi maisha,wakibishana huku raia wakiteketea.

Leo Lukuvi anafanya yale yale yaliyofanywa na Viongozi wa Central Afrika na South Sudan,chama tawala,wanasheria,waandishi wahabari,kiongozi mkuu wa nchi,hawa wote wamenyamaza kimya wanasubiria bomu lipasuke wakimbilie ughaibuni wao na familia zao na raia tumalizane,vita ikiisha (Tukishamalizana)watarudi kuendelea kutawala.:shock::A S cry:😕

umeeleweka
 
lukuvi anapaswa kulaaniwa,na wala shekh usimtetee huyo kaishiwa hoja,kama na wewe una maslahi binafsi utuambie
 
Huyu mkuu wa bakwata dsm nilikuwa namheshimu sana na hata kwenye vikao vya dini tulipokuwa tunakutana naye tulijua ni miongoni mwa watu wasafi na wenye mtazamo wa kitaifa. Kwa alilofanya Jana ninaanza kuwa na wasiwasi nae

Hajaanza leo huyu, ndivyo alivyo kila kukicha, kazi yake siku zote ni kujikomba kwa CCM utafikiri kapewa usheikh na Kikwete! Huyu ni Sheikh wa Interahamwe, kama mwenzie Jongo aliyelia Bungeni kutokana na mahaba ya CCM yaliyomkolea! Sheikh mzima ovyoooooooo!!!!!!!!!
 
Mungu anasema ktk vitabu vitakatifu kuwa, waheshimuni wale wenye mamlaka juu yenu! Watanzania jifunzeni kuwaheshimu viongozi wenu hata kama wamekosea , tuoyeshe alipo kosea kwa hoja sio matusi

Mtu asiyejiheshimu mwenyewe, kamwe hawezi kuheshimiwa na watu wengine! Sheikh huyu wa Interahamwe anatutafsiria lugha nyepesi iliyo wazi kabisa, aliyosema Lukuvi, kama vile kazungumza Kijapani!!!!!??? Huyu kayatafuta mwenyewe matusi, yatajaa magunia, halafu ayapeleke nyumbani kwake kama mshahara wa kazi yake aliyopewa, ili iwe funzo kwa Viongozi wengine wa dini kwamba, kujikomba kwa Interahamwe kamwe hakulipi!!!!!
 
Alichosema sheikh wa
Bakwata
NA MWANDISHI WETU
SHEIKH wa mkoa wa Dar
es Salaam,
Alhad Mussa Salum,
amewataka
waislamu nchini kuacha
kumshambulia
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais (Sera,
Uratibu na Bunge),
William Lukuvi kwa tofauti
za kiitikadi. Akizungumza
na waandishi wa habari
mjini Dar es Salaam jana,
Sheikh Alhad
alisema katika siku za
karibuni,
kumekuwepo na
propaganda
zinazowataka waislamu
kumchukia
Lukuvi bila sababu za
msingi. Alisema hatua
hiyo imewafanya baadhi
ya waumini kuomba dua
maalumu dhidi
ya Lukuvi bila kutambua
msingi wa hoja
hiyo.
Kwa mujibu wa Sheikh
Alhad, chuki
dhidi ya Lukuvi inadaiwa
kutokana na kauli yake ya
kupinga serikali tatu kwa
kuwa pamoja na mambo
mengine, haina
vyanzo vya mapato jambo
ambalo
linaweza kuiweka nchi
sehemu mbaya
na pengine hata
kuchukuliwa na jeshi.
“Tunasema hivyo baada ya
kugundua kuwa kuna
kundi la fulani la
waislamu,
ambao ni wafuasi wa
chama kimoja cha
siasa, ambao wamelibeba
suala la
hotuba ya Lukuvi kwa
mlengo wa
kisiasa unaowanufaisha.
“Waislamu tukumbuke
kuwa dini yetu
inatufundisha kuwa
kumchukia mtu
kusitufanye kutomtendea
haki. Hivyo ni
vizuri tukamtendea haki
hata kama
hatokani na chama chako
unachokipenda au si
muumini wa dini
yako. “Tunawaomba
waislamu kutokubali
kutumiwa na vyama vya
siasa kwa
maslahi binafsi, jambo
ambalo linaweza
kusababisha chuki
miongoni mwetu
pasipo na sababu za
msingi,” alisema.
Akizungumzia suala la
Zanzibar kuwa dola ya
kiislamu, alisema Lukuvi
aliwasaidia waislamu
kujua wasiwasi
walionao viongozi wa
serikali kuhusu
Zanzibar na kwamba huo
ndio mlengo
wa wanaotaka kujitenga
kwa kuachana
na Tanzania Bara.
 
Hivi hawa Masheikh wetu wana nini?? Mbona nashindwa kuwaelewa?..

Uislam Tz Unawakati mgumu sana 🙁..

Yani tunapigwa vita waziwazi Sheikh Unatetea?..Bado siamini..

Sheikh jua Nimekudharau Sana.. Yani basi tu..

Ndio Maana Zanzibar wanataka Nchi yao..Na wapewe
 
Huyu Sheikh wa mkoa wa Dar kila siku amezoea kushinda ikulu unategemea ataongea nini tofauti na hicho?Aanze kukosa bahasha?Tangu lini huyu sheikh amekuwa dictionary ya tafsiri?Maelezo ya Lukuvi tuliyasikiliza neno kwa neno alipokuwa akiongea mwenyewe,Sasa ni mtanzania gani aliyemtuma huyu sheikh atoe tafsiri ya maneno ya Lukuvi?Au Lukuvi alikuwa anaongea kichina hadi watanzania tuhitaji tafsiri toka kwa sheikh?Nawahurumia sana Waislamu sababu viongozi wao wanapenda kutumiwa sana na CCM na mwisho wa siku wanapuuzwa.Wapi FaizaFoxy?Sheikh wake ameshamwambia akome mara moja kuipotosha kauli ya Lukuvi!
 
...huyu jamaa mahali fulani nilimsikia akimsifia EL juu ya mshiko flani walimuomba awachangie. Sikuona shida EL kuwachangia au wao kumuomba mchango,bali mazungumzo yake na wenzake ndo yalinipa shaka kidogo,nikapotezea. Kwa kauli hii ya juzi tayari nimeconclude doubts zangu...
 
Kwani huyo Shekhe Ponda anatofauti gani na Lukuvi?Au huyu sababu ni Waziri kwenye chama chetu?Tuwe watu tunaomuogopa Mungu,haki lazima itendeke.Hata Lukuvi anastahili kufia korokoroni.Haijalishi wadhifa wake.
Lukuvi hajahamasisha watu kufanya vurugu, bali ametoa maoni yake na namna anavyoiona nchi inakoelekea! Lakini Ponda amekuwa akiwahamasisha watu kufanya vurugu na pia amekuwa akifanya mikutano ambayo mwisho wake huchochea watu kufanya vurugu!

Nadhani utakumbuka alivyowahamasisha watu kususia sensa na pia alivyowaongoza watu kuvamia kiwanja cha wenyewe akidai ni mali ya waislamu!
 
Lukuvi hajahamasisha watu kufanya vurugu, bali ametoa maoni yake na namna anavyoiona nchi inakoelekea! Lakini Ponda amekuwa akiwahamasisha watu kufanya vurugu na pia amekuwa akifanya mikutano ambayo mwisho wake huchochea watu kufanya vurugu!

Nadhani utakumbuka alivyowahamasisha watu kususia sensa na pia alivyowaongoza watu kuvamia kiwanja cha wenyewe akidai ni mali ya waislamu!

Kaka yangu unapoangalia kwa jicho la ushabiki tu,utaona Lukuvi yupo sahihi,lakini tafakari kwa kina!Baada ya matamshi yake mbele ya kanisa unategema reaction gani kutoka upande wa pili?Je,kwa dini zilizo naIMANI tofauti kabisa unafikiri kiongozi mwenye madaraka na responsibility kwa Taifa yupo sahihi?Unadhani Shekhe Ponda ana responsibility sawa na aliyonayo Lukuvi?

Kumbuka issue za Udini zipo bado katika hali tete,kuna mapadre wamajeruhiwa na mmoja kuuawa Zanzibar na Shekhe pia amejeruhiwa huko huko Zanzibar,wewe bado unafikiri mpaka aongee kama shekhe Ponda?

Amekosea anatakiwa kuwa responsible na mdomo wake,na mwisho anatkiwa kuwaomba radhi aliyowakosea.Kama Mkristu sitavumilia kauli za watu kama hawa wanaotuvuruga watanzania.Aliyemteua anawajibika sana.Tena nafuu angekuwa ni MUISLAM ameongea hayo kidogo ingekuwa na unafuu fulani,lakini Mkristu anaongea pumba lazima wajibike,tusiendelee kubebana imetosha kwa sasa.

Angalia watu wanavyouana Afrika ya Kati ni sababu ya viongozi kama Lukuvi wa kutamka ujinga kama huo.
 
ImageUploadedByJamiiForums1399452595.643457.jpg
 
Back
Top Bottom