Shemeji yangu anaona wivu mimi kuwa karibu na mumewe

Shemeji yangu anaona wivu mimi kuwa karibu na mumewe

EL ELYON

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2013
Posts
1,565
Reaction score
1,918
Wakuu mmebarikiwa Sana na Mwenyezi Mungu mliofunga Mungu Awakumbuke Sana.....

Nipo mkoa Fulani kikazi mbali kabisa na familia yangu. Huku kwa bahati nzuri kuna ndugu yangu kabisa ni askari.

Nilipofika nilifikia kwake kama siku tatu hivi nikawa nimehamia kwenye nyumba niliyokuwa nimeandaliwa na ofisi.

Nilifurahi Sana kukutana na ndugu yangu kwani tumekua wote tumesoma wote na hata alipoondoka kwenda depo alitokea kwangu yaani nilikuwa naishi naye kabla hata sijaoa.

Sa imekuwa kawaida nikitoka kazini yeye jioni hunitafuta au Mimi humtafuta tunatoka kidogo kisha usiku by saa mbili mi huwa tayari nmerudi kwangu lakini ndugu yangu huwa mara zote namuacha huko mtaani na jamaa zake sjui huwa anarudi kwake saa ngapi.

Nilianza kuhisi ni kama shemeji yangu mke wa ndugu yangu anahisi mume wake anapochelewa kurudi anadhani huwa Niko naye wakati si kweli akiamini mi ndo namchelewesha nilihisi Hilo mapema sana ila nikapotezea tu.

Sasa imeibuka tabia ambayo ni mpya ndugu yangu siku zingine huwa ananipigia simu nipite kwake kumpitia lakini kuna kitu nakiona ni kama mke wa ndugu yangu anajaribu kushindanisha ni Nani mwenye nguvu kwa mume wake je ni yeye mke au Mimi ndugu kwani wakati mwingine naweza nikawa nimekaa namsubiri ndugu yangu tutoke unashangaa mkewe anaongelea dirishani akiwa nje WE BABA FULANI USTOKE.....🤔 Mi kama kawa sjari kabisa hata ila huwa nashangaa tu.

Na kinachonishangaza mara nyingi nikiwa pale ndo utashangaa anamuomba mumewe hela hadharani kuna siku alimuomba hela mumewe akamwambia sina weeee dada aliwaka OOOH MBONA WENGINE WAKIKUOMBA UNAWAPA...🤔 nilishtuka Sana Ile kauli maana ni kama alikuwa ananilenga Mimi as if mi huwa namuomba hela mumewe wakati mumewe ndo huwa namtoa sana.

Kingine akiona nimeshika simu ya mumewe weeee huo mdomo utakavyovutwa nadhan mnaelewa wanaume ukiwa na mshikaji wako kushika simu yake ni kawaida sana.

Nilichogundua Yule shemeji yangu anaona kama ndugu yangu Yuko vizuri Sana na Mimi story kucheka Sana sasa ni kama hiyo Hali inamuumiza Sana kwamba kwanini mumewe hacheki naye Sana wala kupiga naye Sana story kama anavyokuwa na Mimi.

Anatumia nguvu nyingi kutaka kuonyesha ye ana nguvu kwa mumewe kuliko Mimi ndugu wa mumewe.

Cha ajabu pale kwake hata maji tu huu mwaka toka umeanza sjanywa hata maji kwake chakula ndo kabisa hata nikute wanakula sili tarudi kwangu takula niliamua hivyo maana wanawake bwana hivi ni vitu vidogo Sana lakini kwao ni vikubwa nadhani wenye uzoefu mnanielewa yaani mkeo anaweza akamnyanyasa Sana ndugu yako kisa ugari tu japo si wote.

SASA WAKUU HIVI NI KWANINI WANAWAKE WAKE ZA WATU HUWA WANALAZIMISHA WAWE NA NGUVU KWA WAUME ZAO KULIKO NDUGU WA MUME WAKATI HIZO NI NAFASI MBILI TOFAUTI MAANA MI SIWEZI KUWA MKE WA NDUGU YANGU WALA MKE WA NDUGU YANGU HAWEZI CHUKUA NAFASI YA UNDUGU WANGU KWA MUMEWE. ndoa huvunjika ila udugu ni wa milele wanawake Wana shida gani kwenye hili?
Mpka nilikuwa nawaza ingetokea mi nimekuja huku may be sina ramani naishi hapo kwake uwenda ndo ningejua kwanini Putin Hana picha akiwa anacheka...

KARIBUNI kwa maoni wenye uzoefu wa haya mambo.....
 
Sioni sababu ya kuumiza kichwa,
Hebu achana na maisha yao, ndugu yako akikuhitaji atakuja kwako, na wewe nyumbani kwa ndugu yako usikanyage kabisa. Matatizo yao waachie wao watamalizana
 
Sioni sababu ya kuumiza kichwa,
Hebu Achana na maisha yao, ndugu yako akikuhitaji atakuja kwako, na wewe nyumbani kwa ndugu yako usikanyage kabisa.. Matatizo yao waachie wao watamalizana
Uko sahihi lakini msimamo wangu siwezi Acha kwenda kwa ndugu yangu kwa namna yoyote kisa mwanamke kikubwa nisiwaingilie mambo yao wala nisiulize yasiyonihusu hata kama yananihusu wasponiambia nisiulize huo na wala sili wala kunywa pale kwao. ILA la kutoenda kwa ndugu yangu tena wa damu Hilo asahau kama yule mwanamke anataka nisikanyage pale basi MUMEWE ndo aniambie nisiende kwake si mpuuzi mwingine....😬😬😬😬❗
 
Huna shughuli za kufanya zaidi ya kufuatana fuatana na so called ndugu yako???

Jifunze kuweka mipaka!!!


Halafu sio kitu cha kawaida kushika simu ya mtu hususan mwanaume mwenzio.

Huyo ndugu yako ajifunze kutenga muda wa familia na muda wa kuzurura hovyo kabla hujarudi na uzi wa kulalamika jirani anamfariji shemeji yako.
 
Sijui kwann
Mkuu nakuhakikishia jehanamu wanawake watakuwa wengi Sana kuliko wanaume wengi wao Wana roho mbaya Sana fatilia hata namna wanavyoishi na wadada wa kazi kama wanaishi na mbwa Sisi wanaume scandal zetu huwa ni za mapenzi Sana si roho mbaya za kunyanyasa dada wa kazi au ndugu wa mke.
 
Sio lazima kwenda kwake, mnapatana tu mkutane sehemu Fulani alafu ndiyo mnaenda mnakohitaji kwenda Ili kuepusha uo ugomvi.

Na kengine usianze kumlaumu tu uyo shemeji yako, huwezi jua ndani ya ndoa yao kuna mambo Gani yanaendelea, ambayo wewe wa nje huwezi kuyafahamu. Mambo mengine ya ndani huwa ni tofauti na yanvyoonekana nje. Sasa ili kuepusha Ayo yote, ekeni sehemu ya kukutania, na apo Nyumbani kwao nenda siku 1 moja tuu.
 
Wakuu mmebarikiwa Sana na Mwenyezi Mungu mliofunga Mungu Awakumbuke Sana.....

Nipo mkoa Fulani kikazi mbali kabisa na familia yangu. Huku kwa bahati nzuri kuna ndugu yangu kabisa ni askari.
Nilipofika nilifikia kwake kama siku tatu hivi nikawa nimehamia kwenye nyumba niliyokuwa nimeandaliwa na ofisi. Nilifurahi Sana kukutana na ndugu yangu kwani tumekua wote tumesoma wote na hata alipoondoka kwenda depo alitokea kwangu yaani nilikuwa naishi naye kabla hata sijaoa.
Sa imekuwa kawaida nikitoka kazini yeye jioni hunitafuta au Mimi humtafuta tunatoka kidogo kisha usiku by saa mbili mi huwa tayari nmerudi kwangu lakini ndugu yangu huwa mara zote namuacha huko mtaani na jamaa zake sjui huwa anarudi kwake saa ngapi.
Nilianza kuhisi ni kama shemeji yangu mke wa ndugu yangu anahisi mume wake anapochelewa kurudi anadhani huwa Niko naye wakati si kweli akiamini mi ndo namchelewesha nilihisi Hilo mapema sana ila nikapotezea tu.
Sasa imeibuka tabia ambayo ni mpya ndugu yangu siku zingine huwa ananipigia simu nipite kwake kumpitia lakini kuna kitu nakiona ni kama mke wa ndugu yangu anajaribu kushindanisha ni Nani mwenye nguvu kwa mume wake je ni yeye mke au Mimi ndugu kwani wakati mwingine naweza nikawa nimekaa namsubiri ndugu yangu tutoke unashangaa mkewe anaongelea dirishani akiwa nje WE BABA FULANI USTOKE.....🤔 Mi kama kawa sjari kabisa hata ila huwa nashangaa tu.
Na kinachonishangaza mara nyingi nikiwa pale ndo utashangaa anamuomba mumewe hela hadharani kuna siku alimuomba hela mumewe akamwambia sina weeee dada aliwaka OOOH MBONA WENGINE WAKIKUOMBA UNAWAPA...🤔 nilishtuka Sana Ile kauli maana ni kama alikuwa ananilenga Mimi as if mi huwa namuomba hela mumewe wakati mumewe ndo huwa namtoa sana.

Kingine akiona nimeshika simu ya mumewe weeee huo mdomo utakavyovutwa nadhan mnaelewa wanaume ukiwa na mshikaji wako kushika simu yake ni kawaida sana.

Nilichogundua Yule shemeji yangu anaona kama ndugu yangu Yuko vizuri Sana na Mimi story kucheka Sana sasa ni kama hiyo Hali inamuumiza Sana kwamba kwanini mumewe hacheki naye Sana wala kupiga naye Sana story kama anavyokuwa na Mimi.
Anatumia nguvu nyingi kutaka kuonyesha ye ana nguvu kwa mumewe kuliko Mimi ndugu wa mumewe.
Cha ajabu pale kwake hata maji tu huu mwaka toka umeanza sjanywa hata maji kwake chakula ndo kabisa hata nikute wanakula sili tarudi kwangu takula niliamua hivyo maana wanawake bwana hivi ni vitu vidogo Sana lakini kwao ni vikubwa nadhani wenye uzoefu mnanielewa yaani mkeo anaweza akamnyanyasa Sana ndugu yako kisa ugari tu japo si wote.

SASA WAKUU HIVI NI KWANINI WANAWAKE WAKE ZA WATU HUWA WANALAZIMISHA WAWE NA NGUVU KWA WAUME ZAO KULIKO NDUGU WA MUME WAKATI HIZO NI NAFASI MBILI TOFAUTI MAANA MI SIWEZI KUWA MKE WA NDUGU YANGU WALA MKE WA NDUGU YANGU HAWEZI CHUKUA NAFASI YA UNDUGU WANGU KWA MUMEWE. ndoa huvunjika ila udugu ni wa milele wanawake Wana shida gani kwenye hili?
Mpka nilikuwa nawaza ingetokea mi nimekuja huku may be sina ramani naishi hapo kwake uwenda ndo ningejua kwanini Putin Hana picha akiwa anacheka...

KARIBUNI kwa maoni wenye uzoefu wa haya mambo.....

Bro, sorry lakini haya ni mambo ya kike!! Nawe una element za kumfuatilia mienendo mke wa nduguyo! Mambo ya kike kabisa, mawifi ndiyo ugomvi wao huanzia hapo nachojua mashemeji hupendana sana! Una madhaifu somewhere yanayokuingiza kwenye ushindani baina yako na mke wa nduguyo! Change
 
Huna shughuli za kufanya zaidi ya kufuatana fuatana na so called ndugu yako???

Jifunze kuweka mipaka!!!


Halafu sio kitu cha kawaida kushika simu ya mtu hususan mwanaume mwenzio.

Huyo ndugu yako ajifunze kutenga muda wa familia na muda wa kuzurura hovyo kabla hujarudi na uzi wa kulalamika jirani anamfariji shemeji yako.
Mkuu si siku zote nipo na ndugu yangu na mara zote yeye ndio huniita jioni nikiwa free maana Mimi huku ni mgeni pia huyu ndugu huku ana miaka sasa ana marafiki zake pia ana maaskari wenzie mtumiaji mzuri wa kilevi ila mimi stumii kilevi na siku zote huwa namuacha na wenzake huko mtaani.

Kuhusu simu kwa akili yako inavyokutuma kwamba ni kosa kushika simu ya ndugu yako au rafiki yako may be labda ana dk au ana data kuna kitu unatka kufanya kisha kumrudishia.

Mambo ya kukaa na familia yake mi yananihusu nini wakati mimi nimewakuta wanaishi hivyo na jamaa ana michepuko yake huko kitaa sa kama hakai na mkewe mimi ndio nimfundishe au hayo hayanihusu.
 
Huna shughuli za kufanya zaidi ya kufuatana fuatana na so called ndugu yako???

Jifunze kuweka mipaka!!!


Halafu sio kitu cha kawaida kushika simu ya mtu hususan mwanaume mwenzio.

Huyo ndugu yako ajifunze kutenga muda wa familia na muda wa kuzurura hovyo kabla hujarudi na uzi wa kulalamika jirani anamfariji shemeji yako.
Ndiyo mana Mimi nikasema mambo ya ndani ya ndoa mtu wa nje huwezi jua nini kinaendelea. Asianze kumlaumu shemeji huwenda ndugu yake umo ndani anafanya mambo yasiyofaa, iyo upelekea uyo shemeji kuact tofauti na kuhisi lbd ujio wa shemeji yake ndiyo chanzo au lah kitu kengine.

Ni hatari Sana kutetea upande 1 bila kusikia kauli ya upande wa 2.
 
Sio lazima kwenda kwake, mnapatana tu mkutane sehemu Fulani alafu ndiyo mnaenda mnakohitaji kwenda Ili kuepusha uo ugomvi.

Na kengine usianze kumlaumu tu uyo shemeji yako, huwezi jua ndani ya ndoa yao kuna mambo Gani yanaendelea, ambayo wewe wa nje huwezi kuyafahamu. Mambo mengine ya ndani huwa ni tofauti na yanvyoonekana nje. Sasa ili kuepusha Ayo yote, ekeni sehemu ya kukutania, na apo Nyumbani kwao nenda siku 1 moja tuu.
Si siku zote naenda kwake ni mara moja moja Sana ila mara nyingi huwa ananicol tunaonana kama nipo kitaa tamwambia nipo kitaa na sometime hatuonani kabisa mfano toka wiki hii imeanza hatujaonana kbs.
 
Ndiyo mana Mimi nikasema mambo ya ndani ya ndoa mtu wa nje huwezi jua nini kinaendelea. Asianze kumlaumu shemeji huwenda ndugu yake umo ndani anafanya mambo yasiyofaa, iyo upelekea uyo shemeji kuact tofauti na kuhisi lbd ujio wa shemeji yake ndiyo chanzo au lah kitu kengine.

Ni hatari Sana kutetea upande 1 bila kusikia kauli ya upande wa 2.
Ni kweli mambo ya ndoa yana mengi maana hata Mimi Nina familia uzuri sina time kabisa na maisha yao nilichoeleza hapo nadhani kama umegundua hakuna sehemu nimezungumzia maisha yao ila nimesema kile nimekiona kwa shemeji yangu khs Mimi basi na bado nimempuuza Sana yaani sjari chochote ukizingatia siingilii maisha yao kbs ila nachokijua jamaa ana michepuko bs
 
Si siku zote naenda kwake ni mara moja moja Sana ila mara nyingi huwa ananicol tunaonana kama nipo kitaa tamwambia nipo kitaa na sometime hatuonani kabisa mfano toka wiki hii imeanza hatujaonana kbs.
Sawa, Sasa apo mkuu wewe usianze kuweka ligi na uyo shemejio... Punguza kabisa kwenda kwao, mkutane juu kwa juu. Nenda kwa matukio maalum tu, lbd ni mgonjwa au Kuna kikao.
 
  • Thanks
Reactions: THT
Ni kweli mambo ya ndoa yana mengi maana hata Mimi Nina familia uzuri sina time kabisa na maisha yao nilichoeleza hapo nadhani kama umegundua hakuna sehemu nimezungumzia maisha yao ila nimesema kile nimekiona kwa shemeji yangu khs Mimi basi na bado nimempuuza Sana yaani sjari chochote ukizingatia siingilii maisha yao kbs ila nachokijua jamaa ana michepuko bs
Nimeelewa vzr nini wamaanisha. Ila nimeelezea kwamba usimlaumu shemejiyo kuwa anafanya ivi na ivi kwako ukiwa pale.... Huwez jua ndani ndugu yako anamfanyia matendo gani uyo shemejiyo. Huwenda anarudi saa 8 za usiku Kila siku , [emoji2372]. Huwenda ana majibu ya shombo kwa mkewe, huwenda hatoi Muda mzuri kwa familia yake? Na kama ivyo umesema ana michepuko ya kutosha. Na vile vile huwenda ni chuki zake tu kwako hakupendi. Sasa kuepuka tafuteni sehemu ya kukutana. Huyo ni mtoto wa kike usieke ligi nae [emoji2360]
 
  • Thanks
Reactions: THT
Nimeelewa vzr nini wamaanisha. Ila nimeelezea kwamba usimlaumu shemejiyo kuwa anafanya ivi na ivi kwako ukiwa pale.... Huwez jua ndani ndugu yako anamfanyia matendo gani uyo shemejiyo. Huwenda anarudi saa 8 za usiku Kila siku , [emoji2372]. Huwenda ana majibu ya shombo kwa mkewe, huwenda hatoi Muda mzuri kwa familia yake? Na kama ivyo umesema ana michepuko ya kutosha. Na vile vile huwenda ni chuki zake tu kwako hakupendi. Sasa kuepuka tafuteni sehemu ya kukutana. Huyo ni mtoto wa kike usieke ligi nae [emoji2360]
Sijawahi hata kujibizana naye wala sina story naye zaidi ya salamu ligi itoke wapi sasa ila nimekupata mkuu.......
 
Nimeelewa vzr nini wamaanisha. Ila nimeelezea kwamba usimlaumu shemejiyo kuwa anafanya ivi na ivi kwako ukiwa pale.... Huwez jua ndani ndugu yako anamfanyia matendo gani uyo shemejiyo. Huwenda anarudi saa 8 za usiku Kila siku , [emoji2372]. Huwenda ana majibu ya shombo kwa mkewe, huwenda hatoi Muda mzuri kwa familia yake? Na kama ivyo umesema ana michepuko ya kutosha. Na vile vile huwenda ni chuki zake tu kwako hakupendi. Sasa kuepuka tafuteni sehemu ya kukutana. Huyo ni mtoto wa kike usieke ligi nae [emoji2360]
Sijawahi hata kujibizana naye wala sina story naye zaidi ya salamu ligi itoke wapi sasa ila nimekupata mkuu.......
 
Kwani huyi mumewe kaanza kutoka na kuchelewa kurudi kwake baada ya wewe kuhamia huko au kabla?
 
Back
Top Bottom