Sheria hazilindi Mabwege, Watu dhaifu; na Mamlaka huheshimu Mamlaka

Sheria hazilindi Mabwege, Watu dhaifu; na Mamlaka huheshimu Mamlaka

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Mimi pia ni mdau wa Ile Kanuni isemayo kuwa Watu wote ni Sawa Mbele ya sheria, ikiwa ni nguzo muhimu kwenye Rule of law. Yaani kila mtu anapaswa kuwajibika Mbele ya sheria na hakuna ambaye atakuwa juu ya sheria.

Lakini tukija kwenye Falsafa na uhalisia Kanuni hiyo sio halisi, haiko Logically. Kusema Watu wote wawe Sawa Mbele ya sheria ni kauli janjajanja, kauli za kisiasa zinazotumiwa na viongozi kuwalaghai Watu wa kawaida.

Ulimwengu, Una nguvu zake ambazo zinazalisha vijinguvu vidogovidogo kulingana na uhitaji.
Hata hivyo nguvu zimegawanyika katika makundi makuu manne;

1. Nguvu ya Nishati
2. Nguvu ya AKILI (Utashi)
3. Nguvu ya Imani
4. Nguvu ya vitu vilivyopewa thamani na wenye Akili na Imani.

Mwenye nguvu ndiye anayetunga sheria. Hapo ndipo Rule of Law inapoanza kupoteza mwelekeo.
Nguvu ndio inayozalisha Mamlaka.

Ikiwa Mwenye nguvu ndiye anayetunga sheria hapo automatically yeye yupo juu ya Sheria.
Nguvu hutunga sheria zitakazolinda nguvu zake.

Sheria haziwalindi Watu wanyonge, makabwela au mabwege,

Taikon ninapoingia kwenye migogoro na MTU yeyote, cha Kwanza ni lazima niangalie nguvu na mamlaka ya MTU huyo Kabla sijaamua Jambo lolote katika kukabiliana naye. Ukishajua Fulani amekuzidi nguvu za kimamlaka tafsiri yake MTU huyo kisheria hautamuweza.

Zipo Njia zingine za kudili na MTU ambaye amekuzidi kimamlaka na kinguvu kuliko Kutumia sheria ambazo kimsingi hautawezana naye.

Mamlaka huheshimu Mamlaka.
Kama huna mamlaka huwezi kuheshimiwa na wenye mamlaka. Hiyo kiasili haipo hivyo.

Ili mamlaka ikuheshimu lazima uwe na mamlaka zingine ndani yako. Mfano ili viongozi wa kisiasa wa kuheshimu basi itakupasa uwe aidha na nguvu au mamlaka ya kiimani, labda ni Kuhani, Nabii, sheikhe, mtume, au mganga uliyebobea mwenye uwezo wa Hali ya juu.

Au uwe na kipaji kikubwa na ambacho kimewatiisha Watu wengi Mbele yako. Kwa mfano Uwe Mwanamuziki wa kiwango cha juu kama kina Diamond Kwa hapa nchini, au mwanasoka mkubwa kama Ronaldo.

Au uwe na utajiri au Mali ambazo Watu wengi WA kawaida Hawana.

Ukiwa bwege bwege elewa sheria haitakuwa upande wako. Ingawaje watakufanyia unafiki ili ujione nawe unaheshimiwa. Sheria haitakuwa upande wako Kwa sababu haikutungwa kulinda Watu wadhaifu.

Mungu Mtawala na mwenye uweza na mwenye nguvu na mamlaka yote, hata sheria alizoziweka za Asili na zile ambazo alizikasimisha Kwa wanadamu au viumbe wengine ambao watatawala aliunda sheria zinazomlinda yeye mwenyewe.

Mimi na wewe hatuwezi kuwa MUNGU Sio Kwa sababu tuliumbwa nop! Bali ni Kwa sababu tuliwekewa sheria(mipaka) ili tubaki kuwa hivi tulivyo.

Taikon ninaamini kuwa Nguvu hutumia nguvu zingine ili izidi kuwa na nguvu. "Power use other powers to become stronger".

Sio ajabu kuona Mwanasiasa kuungana na matajiri, au watu maarufu ili kuimarisha nguvu zake. Ni Jambo ambalo MTU yeyote mwenye Akili lazima alifanye ili kustawi na kuongezeka.

Kuungana na wanyonge sio tuu kunakupunguzia nguvu Bali pia kunakuangusha Kwa hakika.

Sisemi Watu wasiungane na watu dhaifu, au wanyonge, na mabwege. Nop! Hapa nipo kuzungumzia ukweli na uhalisia wa mambo.

Ukiwa kama mwenye nguvu, ili nguvu zako zidumu Kwa muda mrefu basi itakupasa ujue namna ya kuzitumia nguvu za wenye nguvu wengine. Kisha ujue namna ya kuzishusha pasipo zenyewe kujua zinashushwa, polepole Kwa uhakika.

Ukiwa mtu dhaifu haitakuwa mbinu njema kupambana na wenye nguvu ikiwa wewe unataka kuwa na nguvu kama wao. Kwani Kwa hakika utaanguka na kushindwa tuu. Njia maalumu yenye matokeo yenye tija ni Kutumia nguvu za wenye nguvu ili kuongeza nguvu zako. Wamarekani wao husema " if you can't beàt them join them"

Acha nimalize Kwa kukuambia, Watu hawatumii vitu dhaifu kuwashinda wenye nguvu Bali hutumia vitu vyenye nguvu kuwashinda wenye nguvu au Kupata ñguvu.

Huwezi ipata nguvu Kwa Kutumia Watu wadhaifu au wanyonge, Ila waweza Kupata ñguvu Kwa Watu wenye nguvu ikiwa utawashawishi au utachukua nguvu zao.

Hii ni tofauti na MUNGU muweza wa yote. Yeye hutumia Watu au vitu dhaifu kuvipiga vile vitu au wale Watu wenye Nguvu. Hizo ni Kanuni Ndugu zangu.

Kwa mtakaoona ni useful haya chukueni, Kwa wale mtaoona ni takataka au nadharia zisizo na uhalisia puuzieni.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Tuna safari ndefu sana kama binadamu tunaotaka tufikie mahali pajuu na pakubwa!
 
labda hiyo ni aninalistic religion yenu ambapo rule of the jungle inatawala sokwe kubwa na lenye nguvu hupiga sokwe dhaifu na kuchukuwa kila kitu lkn kwenye jamii inayofwata christian civilization the weak are protected …
 
labda hiyo ni aninalistic religion yenu ambapo rule of the jungle inatawala sokwe kubwa na lenye nguvu hupiga sokwe dhaifu na kuchukuwa kila kitu lkn kwenye jamii inayofwata christian civilization the weak are protected …

Vizuri Sana.
Sasa tutajadili Kwa hoja ili kila atakayepitia hapa ajifunze.

Umesema kwenye Ukristoni hakutumiki Kanuni hiyo isipokuwa Kanuni inayotumika ni Kanuni ya mdhaifu ndiye analindwa?

Ni kipi kinakufanya uamini mfumo Kristo unamlinda mtu dhaifu ilhali Kanuni kuu mojawapo ya Ukristo ni kuwa mwenye nacho atazidi kuongezewa na Yule ambaye Hana hata kile kidogo anachodhani anacho basi atanyang'anywa.

Luka 19:26 NEN​

“Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
 
Ni Sahihi Kabisa.
Ili safari ya jumla ifike juu basi ni jukumu la kila MTU binafsi kuhakikisha anafika juu. Hiyo ndio Njia sahihi.
Lakini kufikiri Kwa ujumla ujumla hiyo ndio inayokwamisha Maendeleo
Tunavyohujumiana hivi pasipotokea mtu ama watu wakaongoza ili kufikia malengo hakuna kitafanyika!
 
Vizuri Sana.
Sasa tutajadili Kwa hoja ili kila atakayepitia hapa ajifunze.

liko wazi nchi zote zinazofwata western christian civilization watu wanaweza wakatoka chini na kufika juu kabisa kimaisha,

Mtu anaweza hata akazaliwa yatima lkn kama akijituma basi anaweza kufika mbali kimaisha kuna sababu kwa nini Dunia nzima watu wanataka kwenda kuishi nchi zinazofwata christian western civilization kwa maana you can make it hata kama ulizaliwa masikini,

Mifumo imewekwa kwa kila mtu kumsaidia atoke hiyo siyo kila mahali tanzania leo hii ukizaliwa barabarani na hauna uwezo kwa maana ya wazazi utafia hapo no body cares sababu system ni animalistic, mwenye nguvu mpishe hata raisi wenu anaamini hivyo kwamba mwenye nguvu ndiyo mwenye haki lkn kwenye christian civilization the system cares for the poor and weak …
 
liko wazi nchi zote zinazofwata western christian civilization watu wanaweza wakatoka chini na kufika juu kabisa kimaisha, mtu anaweza hata akazaliwa yatima lkn kama akijituma basi anaweza kufika mbali kimaisha kuna sababu kwa nini Dunia nzima watu wanataka kwenda kuishi nchi zinazofwata christian western civilization kwa maana you can make it hata kama ulizaliwa masikini, mifumo imewekwa kwa kila mtu kumsaidia atoke hiyo siyo kila mahali tanzania leo hii ukizaliwa barabarani na hauna uwezo kwa maana ya wazazi utafia hapo no body cares sababu system
ni animalistic, mwenye nguvu mpishe hata raisi wenu anaamini hivyo kwamba mwenye nguvu ndiyo mwenye haki lkn kwenye christian civilization the system cares for the poor and weak …

Ni Sahihi Kabisa.
Lakini hata Huko Western ili uwe na nguvu lazima ufuate matakwa(Sheria) ya wenye nguvu. Sheria za Western si unazijua lakini?
 
liko wazi nchi zote zinazofwata western christian civilization watu wanaweza wakatoka chini na kufika juu kabisa kimaisha, mtu anaweza hata akazaliwa yatima lkn kama akijituma basi anaweza kufika mbali kimaisha kuna sababu kwa nini Dunia nzima watu wanataka kwenda kuishi nchi zinazofwata christian western civilization kwa maana you can make it hata kama ulizaliwa masikini, mifumo imewekwa kwa kila mtu kumsaidia atoke hiyo siyo kila mahali tanzania leo hii ukizaliwa barabarani na hauna uwezo kwa maana ya wazazi utafia hapo no body cares sababu system
ni animalistic, mwenye nguvu mpishe hata raisi wenu anaamini hivyo kwamba mwenye nguvu ndiyo mwenye haki lkn kwenye christian civilization the system cares for the poor and weak …
Una hoja usikilizwe ila pia Taikon yuko sahihi pia.
 
Ngoja niweke hivi. Nini kitatokea endapo hao wenye nguvu walioungana wakienda against each other?
 
Mtibeli umesema kweli kabisa na sisi wanyonge tusio na chochote tunaimba kwa shangwe zote na kusema.

......ooh ohh tutapita katikati yao, ooh ooooh tutapita katikati yao🎶🎵.Mwaka huu tutapita katikati yao.

In every rule there is an exception.
My case will be different😉
 
Ni Sahihi Kabisa.
Lakini hata Huko Western ili uwe na nguvu lazima ufuate matakwa(Sheria) ya wenye nguvu. Sheria za Western si unazijua lakini?

ndiyo zinaprotect the weak and poor, na ndiyo maana kila (karibia) mtu anapataka haki yake hata kama ukidhurumiwa na hauna uwezo labda ni yatima kuna mahali utaenda na haki utaipata, kwenye western christian siyo mambo “unajua mimi ni nani?” hata watu wenye uwezo wako humble na down to earth …
 
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Mimi pia ni mdau wa Ile Kanuni isemayo kuwa Watu wote ni Sawa Mbele ya sheria, ikiwa ni nguzo muhimu kwenye Rule of law. Yaani kila mtu anapaswa kuwajibika Mbele ya sheria na hakuna ambaye atakuwa juu ya sheria.

Lakini tukija kwenye Falsafa na uhalisia Kanuni hiyo sio halisi, haiko Logically. Kusema Watu wote wawe Sawa Mbele ya sheria ni kauli janjajanja, kauli za kisiasa zinazotumiwa na viongozi kuwalaghai Watu wa kawaida.

Ulimwengu, Una nguvu zake ambazo zinazalisha vijinguvu vidogovidogo kulingana na uhitaji.
Hata hivyo nguvu zimegawanyika katika makundi makuu manne;

1. Nguvu ya Nishati
2. Nguvu ya AKILI (Utashi)
3. Nguvu ya Imani
4. Nguvu ya vitu vilivyopewa thamani na wenye Akili na Imani.

Mwenye nguvu ndiye anayetunga sheria. Hapo ndipo Rule of Law inapoanza kupoteza mwelekeo.
Nguvu ndio inayozalisha Mamlaka.

Ikiwa Mwenye nguvu ndiye anayetunga sheria hapo automatically yeye yupo juu ya Sheria.
Nguvu hutunga sheria zitakazolinda nguvu zake.

Sheria haziwalindi Watu wanyonge, makabwela au mabwege,

Taikon ninapoingia kwenye migogoro na MTU yeyote, cha Kwanza ni lazima niangalie nguvu na mamlaka ya MTU huyo Kabla sijaamua Jambo lolote katika kukabiliana naye. Ukishajua Fulani amekuzidi nguvu za kimamlaka tafsiri yake MTU huyo kisheria hautamuweza.

Zipo Njia zingine za kudili na MTU ambaye amekuzidi kimamlaka na kinguvu kuliko Kutumia sheria ambazo kimsingi hautawezana naye.

Mamlaka huheshimu Mamlaka.
Kama huna mamlaka huwezi kuheshimiwa na wenye mamlaka. Hiyo kiasili haipo hivyo.

Ili mamlaka ikuheshimu lazima uwe na mamlaka zingine ndani yako. Mfano ili viongozi wa kisiasa wa kuheshimu basi itakupasa uwe aidha na nguvu au mamlaka ya kiimani, labda ni Kuhani, Nabii, sheikhe, mtume, au mganga uliyebobea mwenye uwezo wa Hali ya juu.

Au uwe na kipaji kikubwa na ambacho kimewatiisha Watu wengi Mbele yako. Kwa mfano Uwe Mwanamuziki wa kiwango cha juu kama kina Diamond Kwa hapa nchini, au mwanasoka mkubwa kama Ronaldo.

Au uwe na utajiri au Mali ambazo Watu wengi WA kawaida Hawana.

Ukiwa bwege bwege elewa sheria haitakuwa upande wako. Ingawaje watakufanyia unafiki ili ujione nawe unaheshimiwa. Sheria haitakuwa upande wako Kwa sababu haikutungwa kulinda Watu wadhaifu.

Mungu Mtawala na mwenye uweza na mwenye nguvu na mamlaka yote, hata sheria alizoziweka za Asili na zile ambazo alizikasimisha Kwa wanadamu au viumbe wengine ambao watatawala aliunda sheria zinazomlinda yeye mwenyewe.

Mimi na wewe hatuwezi kuwa MUNGU Sio Kwa sababu tuliumbwa nop! Bali ni Kwa sababu tuliwekewa sheria(mipaka) ili tubaki kuwa hivi tulivyo.

Taikon ninaamini kuwa Nguvu hutumia nguvu zingine ili izidi kuwa na nguvu. "Power use other powers to become stronger".

Sio ajabu kuona Mwanasiasa kuungana na matajiri, au watu maarufu ili kuimarisha nguvu zake. Ni Jambo ambalo MTU yeyote mwenye Akili lazima alifanye ili kustawi na kuongezeka.

Kuungana na wanyonge sio tuu kunakupunguzia nguvu Bali pia kunakuangusha Kwa hakika.

Sisemi Watu wasiungane na watu dhaifu, au wanyonge, na mabwege. Nop! Hapa nipo kuzungumzia ukweli na uhalisia wa mambo.

Ukiwa kama mwenye nguvu, ili nguvu zako zidumu Kwa muda mrefu basi itakupasa ujue namna ya kuzitumia nguvu za wenye nguvu wengine. Kisha ujue namna ya kuzishusha pasipo zenyewe kujua zinashushwa, polepole Kwa uhakika.

Ukiwa mtu dhaifu haitakuwa mbinu njema kupambana na wenye nguvu ikiwa wewe unataka kuwa na nguvu kama wao. Kwani Kwa hakika utaanguka na kushindwa tuu. Njia maalumu yenye matokeo yenye tija ni Kutumia nguvu za wenye nguvu ili kuongeza nguvu zako. Wamarekani wao husema " if you can't beàt them join them"

Acha nimalize Kwa kukuambia, Watu hawatumii vitu dhaifu kuwashinda wenye nguvu Bali hutumia vitu vyenye nguvu kuwashinda wenye nguvu au Kupata ñguvu.

Huwezi ipata nguvu Kwa Kutumia Watu wadhaifu au wanyonge, Ila waweza Kupata ñguvu Kwa Watu wenye nguvu ikiwa utawashawishi au utachukua nguvu zao.

Hii ni tofauti na MUNGU muweza wa yote. Yeye hutumia Watu au vitu dhaifu kuvipiga vile vitu au wale Watu wenye Nguvu. Hizo ni Kanuni Ndugu zangu.

Kwa mtakaoona ni useful haya chukueni, Kwa wale mtaoona ni takataka au nadharia zisizo na uhalisia puuzieni.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam

Nikiri umeeleweka sana tu
 
labda hiyo ni aninalistic religion yenu ambapo rule of the jungle inatawala sokwe kubwa na lenye nguvu hupiga sokwe dhaifu na kuchukuwa kila kitu lkn kwenye jamii inayofwata christian civilization the weak are protected …
Yale yale wapi katika " kwenye chritian civilization weak are protected? even hapo mnapopaita Vatican, only the powerful cardinal are only who make decisions on direction that church should follow!
 
Back
Top Bottom