KERO Sheria inayompa mamlaka makubwa DPP, kuwa apeleke au asipeleke kesi mahakamani, ni mbaya na inafaa ifutwe

KERO Sheria inayompa mamlaka makubwa DPP, kuwa apeleke au asipeleke kesi mahakamani, ni mbaya na inafaa ifutwe

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Ofisi ya DPP, haina chama, ila DPP anaruhusiwa kuwa mwanachama wa chama chochote.
P
Hatujali yeye kuwa mwanachama wa CCM.

Tunachopinga sisi ni yeye kupendelea Kwa uwazi kabisa watawala wa. CCM na kuwakandamiza wapinzani wa serikali hii ya CCM, kinyume Cha kiapo chake
 
Miongoni mwa sheria mbovu sana zilizopo nchini ni inayompa mamlaka DPP ya kuweza kupeleka au kutopeleka kesi yoyote ya jinai, inayomkabili mwananchi yeyote na asitoe sababu za kutoipeleka kesi yoyote Ile mahakamani!

Hii ni sheria mbovu sana, ambayo ilitungwa Kwa nia ya kuwafanya baadhi ya wananchi kuwa ni "untouchables"

Nalielezea hili baada ya Jeshi la Polisi, kutamka hadharani, kuwa limeshakamilisha uchunguzi wake wa kesi inayomkabili yule Mama anayetambukika Kwa jina la "afande" na wamelipeleka jalada la kesi hiyo Kwa DPP, Ili eti aamue kuipeleka au kutoipeleka kesi hiyo mahakamani!

Hivi Kwa kosa kubwa kama hili la kuagiza vijana watano waende wakambake yule Binti Kwa kile kinachoitea " rape gang" ambayo Kwa Kila mwananchi aliyesikia huu mkasa anahuzunika sana, sasa inashangaza kusikia kuwa Jeshi la Polisi, limeshakamilisha upelelezi wake, lakini limepeleka jalada la kesi hiyo Kwa DPP, Ili akiamua apeleke kesi hiyo mahakamani na vile vile akiamua asiipeleke kesi hiyo mahakamani na hakuna raia yeyote mwenye mamlaka ya kumuhoji, Kwa nini hajapeleka kesi hiyo mahakamani!😚

Hii sheria ni mbovu sana, ambayo ilitungwa maalum Kwa kuwakinga baadhi ya watu mashuhuli nchini, Ili hata wakitenda makosa makubwa ya jinai ya aina Gani, Ili wajue kuwa wanayo kinga Kwa DPP.

Eti sheria hiyo imempa mamlaka hayo ya kupeleka au kutoipeleka kesi yoyote Ile na Wala asiulizwe sababu za kutoipeleka kesi yoyote mahakamani!

Hawa watawala wetu, wasitufanye sisi watanzania wote kuwa ni wajinga sana, kiasi Cha kututungia sheria za aina hiyo za ubaguzi wa dhahiri ambapo DPP ataangalia hadhi ya mtuhumiwa na kuamua kutoipeleka kesi yake mahakamani na kuamua kupeleka kesi za walala hoi pekee wasio na kinga hiyo ya DPP na kupeleka kesi zao mahakamani!

Hii sheria inaji-contradict na sheria mama ya Katiba ya nchi, inayosema kuwa watu wote nchini, wako sawa mbele ya sheria.

Nitoe wito Kwa waheshimiwa wabunge wetu, wapeleke muswada wa dharura Bungeni, Ili kuibadili sheria hii, ambayo inaonyesha upendekeo wa dhahiri Kwa watu wachache, wenye hadhi mbalimbali hapa nchini.

Mungu ibariki Tanzania
Ikisimamiwa kwa haki sio mbaya ila ikifanya Kazi kwa maslahi ya watawala ni mojawapo ya sheria mbovu na mbaya kabisa
20240827_220701.jpg
 
Hizi sheria wakati zinatungwa huwa mnakuja na maelezo haya ili kufanya ziweze kupita, lakini kiuhalisia huwa zinaacha mianya mikubwa hadi kutumika na kikundi hasa cha viongozi kutekeleza nia ovu. Ni nani asiyeona haya mamlaka ya DPP jinsi yanavyotumika kunyima haki za watu, na jinsi mamlaka haya yalivyogeuka kinga kwa viongozi wanasiofuata sheria? Acha kutetea uovu ukidhani kila sheria ni sheria halali kisa zimepitishwa na bunge.
eleza, ni namna gani haki zinanyimwa, usionge kiujumla. pia, peruzi hata mtandaoni nchi zingine mamlaka ya DPP yapoje ndio uje hapa kujadili kwa hoja sio mihemko. sikatai, kuna mazingine DPP huwa anaweza kuegemea kwa watawala na kutumika kama zana, ila hiyo haiondoi umuhimu wa yeye kama mwakilishi wa republic kuwa na mamlaka ya control of prosecutions kwa namna ilivyo sasa. zaidi ya yote, akiabuse powers, kuna remedy kwenye sheria pia ndio maana hata tukienda Mahakamani kuyapinga hayo mamlaka, tutapigwa chini kwasababu remedy ipo.
 
Hebu nieleze huyo mwendesha mashitaka alikuwa na ushahidi Gani wa ugaidi, Hadi aidhinishe Freeman Mbowe, ashitakiwe Kwa kosa kubwa la jinai la ugaidi??

Nikuuluze swali jingine, unaweza kuniambia, hivi ushahidi aliokuwa nao DPP "uliyeyuka" ghafla na kumlamisha yeye DPP aiondoe kesi hiyo ya ugaidi, iliyokuwa ikimkabili Mbowe??

Tuwe wakweli, nyinyi watawala wa CCM mkishirikiana na Jeshi la Polisi nchini na Mkurugenzi wenu wa mashtaka (DPP) mmezoea mno kuwabambikia kesi, hususani wapinzani wa "dizaini" ya Chama kikuu Cha upinzani nchini Cha Chadema!😗
kwa fununu zilizopo (mimi na wewe hatuna jalada, sote ni raia, majadala ni ya serikali) ushahidi ulikuwepo, kama unazijua definitions za ugaidi.wengi wanaamini ugaidi hadi mtu avae mabom ajilipue au alipue wengine. mbowe inasemekana ushahidi ulikuwepo na yeye alikuwa anajua upo nata lisu alijua upo ndio maana alikimbia mbio nyingi kwenda ubelgiji, na samia alimsaidia tu. hakuwa na mabom ila kwa mujibu wa sheria ya ugaidi, wanasema evidence ilikuwepo.
 
Mkuu Yesu Anakuja , kwanza nimefurahi sana kujua kuwa niko humu na mdogo wangu wa UDSM sheria, ni kweli nilimaliza LL.B mwaka 2007 Dean akiwa Dr. Ibrahim Juma. Ni kweli nilikuwa biker na 2008 ile pikipiki imenifanya kitu mbaya.

Hongera kwa kufanya kazi Ofisi ya DPP.
Mimi ni muumini wa haki bin haki, baadhi ya mamlaka, sheria zetu, taratibu na kanuni sio za haki bin haki.

Moja ya mamlaka hayo ni ile mamlaka presidential preventive detention order, ya rais wa JMT anapoelezwa mtu fulani ni hatari kwa usalama wa Taifa, ana mamlaka ya kukukamata na kuwekwa kizuizini indefinitely bila kuambiwa kosa wala kufikishwa mahakamani. Kina Prof. Shivji, Kanywani, Mgongo Fimbo, Chris Peter, wakaichallenge kwa mandamus na sechorari, Mahakama Kuu ikatengua power hiyo na sasa Rais akimtia mtu kizuizini kwa sheria hiyo, has to give reasons na lazima mtuhumiwa afikishwe mahakamani.

Everything happens for a reason, mamlaka ya DPP kwenye Nolle bado yapo, DPP hapaswi kutoa sababu yoyote kwa yeyote na hakuna mamlaka ya kuhoji nolle!.

Naunga mkono kuwa kwenye Nolle DPP has to give reasons.
P
pole kwa bike, ila hizo makitu ya kina shivji na wengine unataja, hayapo siku hizo bro, kwa sasa kuanzia arrest hadi mahakamani CPA imecontrol, yale mambo ya kuambiwa hakuna kutoka mkoa huu unaambiwa na serikali hayapo yalikufa zamani sana. na ukiona haupo huru siku hizi umenyimwa uhuru na Mahakama kutokukupatia bail ila sio DPP, na mahakama inafanya hivyo kwa kufuata sheria. naelewa shivji miaka hiyo alishawahi pelekwa sumbawanga akaambiwa hakuna kutoka mkoa ule, na alitii, ila sheria hizo hazipo tena. ubarikiwe.
 
Miongoni mwa sheria mbovu sana zilizopo nchini ni inayompa mamlaka DPP ya kuweza kupeleka au kutopeleka kesi yoyote ya jinai, inayomkabili mwananchi yeyote na asitoe sababu za kutoipeleka kesi yoyote Ile mahakamani!

Hii ni sheria mbovu sana, ambayo ilitungwa Kwa nia ya kuwafanya baadhi ya wananchi kuwa ni "untouchables"

Nalielezea hili baada ya Jeshi la Polisi, kutamka hadharani, kuwa limeshakamilisha uchunguzi wake wa kesi inayomkabili yule Mama anayetambukika Kwa jina la "afande" na wamelipeleka jalada la kesi hiyo Kwa DPP, Ili eti aamue kuipeleka au kutoipeleka kesi hiyo mahakamani!

Hivi Kwa kosa kubwa kama hili la kuagiza vijana watano waende wakambake yule Binti Kwa kile kinachoitea " rape gang" ambayo Kwa Kila mwananchi aliyesikia huu mkasa anahuzunika sana, sasa inashangaza kusikia kuwa Jeshi la Polisi, limeshakamilisha upelelezi wake, lakini limepeleka jalada la kesi hiyo Kwa DPP, Ili akiamua apeleke kesi hiyo mahakamani na vile vile akiamua asiipeleke kesi hiyo mahakamani na hakuna raia yeyote mwenye mamlaka ya kumuhoji, Kwa nini hajapeleka kesi hiyo mahakamani!😚

Hii sheria ni mbovu sana, ambayo ilitungwa maalum Kwa kuwakinga baadhi ya watu mashuhuli nchini, Ili hata wakitenda makosa makubwa ya jinai ya aina Gani, Ili wajue kuwa wanayo kinga Kwa DPP.

Eti sheria hiyo imempa mamlaka hayo ya kupeleka au kutoipeleka kesi yoyote Ile na Wala asiulizwe sababu za kutoipeleka kesi yoyote mahakamani!

Hawa watawala wetu, wasitufanye sisi watanzania wote kuwa ni wajinga sana, kiasi Cha kututungia sheria za aina hiyo za ubaguzi wa dhahiri ambapo DPP ataangalia hadhi ya mtuhumiwa na kuamua kutoipeleka kesi yake mahakamani na kuamua kupeleka kesi za walala hoi pekee wasio na kinga hiyo ya DPP na kupeleka kesi zao mahakamani!

Hii sheria inaji-contradict na sheria mama ya Katiba ya nchi, inayosema kuwa watu wote nchini, wako sawa mbele ya sheria.

Nitoe wito Kwa waheshimiwa wabunge wetu, wapeleke muswada wa dharura Bungeni, Ili kuibadili sheria hii, ambayo inaonyesha upendekeo wa dhahiri Kwa watu wachache, wenye hadhi mbalimbali hapa nchini.

Mungu ibariki Tanzania
Ikisimamiwa kwa haki sio mbaya ila ikifanya Kazi kwa maslahi ya watawala ni mojawapo ya sheria mbovu na mbaya kabisa
Huyu spika na hilo bunge kwa ujumla LIMEWADHARAU NA LINAWAONA WATANZANIA NI WAENDAWAZIMU TU

ova
20240827_223620.jpg
 
kwa fununu zilizopo (mimi na wewe hatuna jalada, sote ni raia, majadala ni ya serikali) ushahidi ulikuwepo, kama unazijua definitions za ugaidi.wengi wanaamini ugaidi hadi mtu avae mabom ajilipue au alipue wengine. mbowe inasemekana ushahidi ulikuwepo na yeye alikuwa anajua upo nata lisu alijua upo ndio maana alikimbia mbio nyingi kwenda ubelgiji, na samia alimsaidia tu. hakuwa na mabom ila kwa mujibu wa sheria ya ugaidi, wanasema evidence ilikuwepo.
Huo ni uongo wa mchana!

Hivi unaweza kukubaliana na huu ushahidi wa Kingai, aliyedai eti kuwa Mbowe, ali-mobilize watu, Ili wakate miti na kuilaza barabarani??

Ili Barabara hizo zisipitike??😎
 
Pascal, kwa bahati mbaya, waliounga mkono hoja hii wote sio wanasheria, wewe ukiwa mmojawapo (though najua ulisoma sheria). Hili suala lipo kwenye katiba, mipaka ya kipi DPP azingatie anapotaka kushitaki. kasome tu ibara ya 59 ya katiba. Pia, tulivyosoma chuo, DPP ni Jamhuri, na jamhuri haiwezi kuruhusu kila shitaka liende mahakamani, mengine yanapoteza muda tu hayana ushahidi, mengine ya maonezi, mengine yakutunga n.k, lazima awepo mtu wa kuamua badala ya wote, hatuwezi wote tukawa DPP anatuwakilisha tu. Paschal tulivyosoma chuo miaka ile, nadhani wewe ulitutangulia, ulimaliza 2007 udsm kama sikosei na lile pikipiki lako, (kidding) nakumbuka, tulikuwa wote, tulifundishwa haya, sisi wenzio tuliamua kuingia kufanya kazi hukohuko kwa DPP tukafahamu hayo yote kabla hatujaondoka, nadhani wewe pia kabla haujaja mtaani ulitakiwa upitie kwenye practice kwanza. samahani kama nimekukwaza.
Ni sheria ya kijinga sn, kwanini awe na uwezo wa kufungua kesi hapo hapo anaweza kuifuta bila maelezo? lazima kuwe na maelezo ya kufungua kesi na ya kufuta ni sheria ya kijinga sn ni kwa sababu hujawahi kubambikwa kesi lakini ndiyo ungejua kuwa ofisi ya DPP ni tawi kuu la CCM na haipo kwa maslahi ya umma, angalia kipindi cha Mganga kulikuwa na kesi kibao za uhujumu uchumi sahivi ziko wapi? mambo mengine ni ya kijinga sn.
 
Hata Petrol alisema siyo mfuasi wa Yesu lakini matendo yake yalimsuta, ulitaka DPP akiri kuwa ni kada wa CCM?
Hapana, kuna baadhi ya positions, mtu hatakiwa kuwa kada wa chama chochote wakiwemo watumishi wa ngazi kuanzia waandamizi wa serikali, polisi, jeshi na usalama, ila ndani ya mioyo yao, wanaruhusiwa kuwa na mapenzi na chama chochote, na baada ya kustaafu utumishi wa umma, wanaruhusiwa kuomba nafasi za kisiasa ambazo ni haki yao kikatiba, tumeshuhudia mtu aliyekuwa CJ, akigombea urais, ubunge ndio usiseme!, hiyo ni haki yao
P
 
Hapana, kuna baadhi ya positions, mtu hatakiwa kuwa kada wa chama chochote wakiwemo watumishi wa ngazi kuanzia waandamizi wa serikali, polisi, jeshi na usalama, ila ndani ya mioyo yao, wanaruhusiwa kuwa na mapenzi na chama chochote, na baada ya kustaafu utumishi wa umma, wanaruhusiwa kuomba nafasi za kisiasa ambazo ni haki yao kikatiba, tumeshuhudia mtu aliyekuwa CJ, akigombea urais, ubunge ndio usiseme!, hiyo ni haki yao
P
Hii katiba nani anaifuata Paschal? tuache basi kujitoa ufahamu, kipindi cha Magu ofisi ya DPP ilikuwa imejaa kesi za uhujumu uchumi wa matajiri sahivi zipo wapi? kwanini DPP awe na uwezo wa kuondoa kesi mahakamani bila maelezo? kuna mtu anaweza kuteuliwa Tanzania kwa nafasi yoyote bila kuwa kada wa CCM? mimi nimekuwa kiongozi wa UVCCM 2014 mpk 2017 nilipojitoa kwa ngazi ya Mkoa madudu nayajua vizuri sn nimeyaishi ni utapeli tupu.
 
Hii sheria... ambayo ilitungwa maalum Kwa kuwakinga baadhi ya watu
Ilitungwa makusudi, ndio.

Julius Kambarage Nyerere is singlehandedly culpable of this criminal design.

Anaitwa Baba wa Taifa for a reason. Kila uovu wa kiutawala wa nchi hii aliusimika mizizi yeye.

And he knew better. Nyerere akiwa mwanafunzi Scotland alikuwa mwanachama wa the Fabian Society. Hawa kucha kutwa kazi ku debate tawala na siasa za dunia zinavyokwenda. Alijua tawala za dunia zinafanyaje kazi, akaja kutuletea uozo, sijui aliutoa wapi.

Hawa waliomfuata kina Mwinyi, Mkapa, JK, hawa ni monkey see, monkey do, hawana hatia, they can plead insanity, hawakuwa na upeo wa kubadilisha chochote cha Nyerere.

We unadhani Samia Suluhu Hassan akisoma hapa ataelewa tunalalamika nini ?
 
Back
Top Bottom