Sheria Kuu Kumi za Ulimwengu na Akili (10 Laws of the Mind and Universe/Universal Laws)

Sheria Kuu Kumi za Ulimwengu na Akili (10 Laws of the Mind and Universe/Universal Laws)

Duu... nimefunguliwa kiasi flan!! Ata akili yangu ina sheria kumbe!!@

Akili yako ni Mgodi mkubwa sana wa Ufahamu. Usiache kuichunguza akili yako kwa kuangalia na maisha yako.
Nimefurahi sana kwa kuwa umeelewa kiasi fulani, ni sehemu ambayo utazidi kufunuka ukizidi kuchunguza zaidi baada ya kuelewa.
 
Niliandika mimi kwa kiswahili katika kujifunza vyanzo tofauti tofauti. Sijaandika ya kingereza kwani nilipenda watumiaji wa kiswahili waielewe vyema, kwani hao ndio walengwa wangu hasa.

Sawa mkuu nashukuru....ngoja niisome maana niliipitia tu juu juu.... siku hizi naonaga uvivu kusoma mada za Kiswahili hasa zikiwa ndefu kidogo nahisi ninamajini ya kizungu
 
Karma ni uhalisia wa ulimwengu kuwa, kila chanzo kina matokeo yake. Ni sawa na kusema tenda mema upate mema. Ulivyo hivi sasa ni kutokana na matendo yako, mawazo yako na maneno yako yaliyopita. Karma ni kama mkia ambao unakufuata kutokana na ulivyo na utendavyo.

Karma ni kama mkusanyiko wa matendo yako, mabaya na mema, pamoja na matokeo yake mabaya na mema. Ni msemo unaoaminika hasa katika imani za Mashariki kama vile Hinduism na Buddhism. Kila mwanadamu ana Karma yake, Karma inapaswa kuwa safi kwa kutenda mema, kuwaza mema na kisema mema. Kila hali imetokana na Karma fulani, inaweza ikawa sio yako au ikawa ya mwenzio ambayo ikakuadhiri na wewe kutokana na muunganiko wa Karma zenu.

Wapo waliofika mbali na kusema kuwa, Unapokufa Karma inaondoka na wewe, kama ulitenda mema karma yako inakuwa nyepesi na sio nzito. Karma ya mabaya ni nzito kulinganisha na roho yako, karma ya mema ni nyepesi sana. Ukifa kama ulikuwa na Karma nyepesi nafsi yako inakuwa nyepesi na kuruhusu nafsi yako kurudi katika chanzo kikuu (ulipokwepo kabla ya kuzaliwa), lakini kama ulikuwa na karma mbaya, nafsi yako inazidi kushikiliwa katika ulimwengu wa chini kwa uzito wa karma na unaendelea kuzunguka katika ulimwengu wa chini, wengine huzaliwa upya katika form tofauti tofauti ya uhai bila kujitambua kuwa umerudi lakini deeply inside roho inakumbuka. Kukumbuka ulipopitia katika maisha yako ni mpaka uungane na roho yako kwani inahifadhi maisha yako yote. Wapo walioona hayo, wengine walibahatika mpaka kukumbuka walipokwepo zamani.

Huo ni mtazamo ambao sikupenda sana watu waanze kuuelewa, lakini cha msingi fahamu kuwa Karma ni matokeo ya matendo yako na mawazo yako. Hukufuata kama vile kivuli kikufuatavyo, nakaribisha na wewe uelezee uelewa wako wa Karma ili nami nifahamu zaidi.

Another useful post from Apollo...

Received_with thanks mkuu.
 
HAKIKA! sijapata kuona mwalimu mzuri, mpole,mcheshi, mwenye hekima, busara, anayejua nini amfundishe mwanafunzi, asiyekuwa mchoyo wa maarifa aliyo nayo nk: niishie tu kwa kusema kuwa wewe ni mwalimu mwema. Kwa jinsi nimesoma kwa utaratibu sana yameniingia kweli kweli. Kumbe kwa kusoma tu haya unakuwa na uwezo wa kumtazama mtu na ukajua mawazo anayowaza. Shukrani sana mkuu.
 
Apollo sheria ya 2, 3, 4 etc vipi tunazingoja kwa hamu kubwa sana!
 
Last edited by a moderator:
Naomba kila uandikapo makala/ishus fikirishi kama hizi ukumbuke kum mention mtu anaitwa UNDENIABLE ni fan mkubwa sana wa hizi fikra fikirishi!

Ubarikiwe tena!

Kwanza ubarikiwe mkuu Appolo kwa mada adimu na za thamani kama hizi,

Naomba ku declare interest na mimi mkuu usinisahau ili twende wote,japo sii kazi yako lakini utukumbuke mkuu

Long live jamii forum na wakuu wote kama wewe.
 
just reward of the nature caused by your own effects, can be both -ve/+ve.........hope nimekuchanganya zaidi!

helpline kwa: Apollo

Siku ukianza kufundisha karma tafadhali tag me..

nasoma mada zako,napenda unavyofundisha ni elimu nzuri.
 
Hizi mada zinanihamisha toka fikra moja kwenda fikra nyingine. Asanteni sana watoa mada.
 
Karma ni uhalisia wa ulimwengu kuwa, kila chanzo kina matokeo yake. Ni sawa na kusema tenda mema upate mema. Ulivyo hivi sasa ni kutokana na matendo yako, mawazo yako na maneno yako yaliyopita. Karma ni kama mkia ambao unakufuata kutokana na ulivyo na utendavyo.

Karma ni kama mkusanyiko wa matendo yako, mabaya na mema, pamoja na matokeo yake mabaya na mema. Ni msemo unaoaminika hasa katika imani za Mashariki kama vile Hinduism na Buddhism. Kila mwanadamu ana Karma yake, Karma inapaswa kuwa safi kwa kutenda mema, kuwaza mema na kisema mema. Kila hali imetokana na Karma fulani, inaweza ikawa sio yako au ikawa ya mwenzio ambayo ikakuadhiri na wewe kutokana na muunganiko wa Karma zenu.

Wapo waliofika mbali na kusema kuwa, Unapokufa Karma inaondoka na wewe, kama ulitenda mema karma yako inakuwa nyepesi na sio nzito. Karma ya mabaya ni nzito kulinganisha na roho yako, karma ya mema ni nyepesi sana. Ukifa kama ulikuwa na Karma nyepesi nafsi yako inakuwa nyepesi na kuruhusu nafsi yako kurudi katika chanzo kikuu (ulipokwepo kabla ya kuzaliwa), lakini kama ulikuwa na karma mbaya, nafsi yako inazidi kushikiliwa katika ulimwengu wa chini kwa uzito wa karma na unaendelea kuzunguka katika ulimwengu wa chini, wengine huzaliwa upya katika form tofauti tofauti ya uhai bila kujitambua kuwa umerudi lakini deeply inside roho inakumbuka. Kukumbuka ulipopitia katika maisha yako ni mpaka uungane na roho yako kwani inahifadhi maisha yako yote. Wapo walioona hayo, wengine walibahatika mpaka kukumbuka walipokwepo zamani.

Huo ni mtazamo ambao sikupenda sana watu waanze kuuelewa, lakini cha msingi fahamu kuwa Karma ni matokeo ya matendo yako na mawazo yako. Hukufuata kama vile kivuli kikufuatavyo, nakaribisha na wewe uelezee uelewa wako wa Karma ili nami nifahamu zaidi.

Kwamba karma yang ikiwa safi italudi sehemu nliokuwa kabla ya kuzaliwa ni wapi uko .....
 
Back
Top Bottom