Sheria ya Ndoa: Maswali na majibu mbalimbali

Sheria ya Ndoa: Maswali na majibu mbalimbali

UTANGULIZI

Wenza ambao wameoana kwa sheria zinazotambulika tanzania (kimila, kidini na kiserikali) hudai talaka mahakamani (divorce). Pia ambao hawajaoana kwa sheria hzi na wameishi zaid ya miaka miwili hudani KUTENGANISHWA (separation order) so separation na divorce ni tofauti na hutumika mazingira tofauti.

Kwa wewe km unataka kuachana FOREVER/Milele huna budi kwnd mahakamani kuomba talaka (km ilikuwa ndoa ya kisheria tajwa hapo juu) kwa kutoa sababu zilizoainishwa kwny kifungu cha 107 cha sheria ya ndoa sura Na. 21 R.E 2002 ukiwa na hati ya usuluhushishi kuwa ndoa imeashindikana kuendelea (broken irrepairable).

Lakini pia km hauhtaji kutengana nae maisha/milele mwaweza (nyote wawili) kuandika makubaliano ya kutengana (kuishi mbali) chini ya kifungu cha 67 cha sheria tajwa hapo juu. Mkaishi kila mtu mbali ila bado wanandoa.
Mkuu kwani lazima uwe na hatu ya usuruhisho ndo ukubariwe kufungua shauri mahakamani? Ikiwa mwenza wako hakutaka usuruhisho katoroka na hataki kusuruhishwa inakuwaje ? Mahakama inaweza kupokea ombi la taraka?
 
Ili mahakama ivunje ndoa lazima mmepitia baraza la usuluhishi la ndoa (marriage conciliation board) ikashindikana kusuluhisha ndoa..kutoka kwenye baraza la usuluhishi mtapewa certificate kwamba usuluhishi umefeli kwahyo muende mahamakani.

Mahakama ktk kuvunja ndoa inakuwa inaongozwa na sheria ya ndoa ya Mwaka 1973 japo kuna revised edition ya 2002 ambayo inasema ndoa mpk ivunjwe n lazima iwe imefikia hatua ambayo haiwezi kurekebishika(the marriage has broken down irreperably) kumaanisha mmeenda usuluhishi Wa bodi imeshndkana na mnaweza pewa separation period Kwa muda almost miaka 2 muangalie km mtaweza kusuluhisha. Vyote vikishindikana basi mtafile petition for divorce itasikilizwa then ndoa itavunjwa na kubaki kuangalia mambo mengine kama division of matrimonial asset and custody of the children yani mgawanyo Wa mali na matunzo ya watoto kama wapo.

Vipi kama mliishi kwa makubaliao mutual tu, kwa miaka mingi tu inayozidi kumi, na mmefanya mengi pia. Inapofikia hatua ya kuachana mmekubaliana pia kuachana bila ugomvi wowote na hamtaki kushirikisha mtu yeyote kusuluhisha kwa sababu mmeshakubaliana uachana kuna njia yoyote ya kufuata kisheria ili baadae kusiwe na msuguano hasa kwenye mgawanyo wa mali. Mtu anaweza akaridhika na mlivogawana leo lakini baadae shida zikimshika analeta story tofauti!
 
Nianze kueleza kifupi[emoji120]

Niliajiriwa miaka kadhaa hapo nyuma na wakati naajiriwa nilikuwa desperate na ndoa hivyo nilipofika kazini tu 1st date yangu nikaamua kuishi nae.

Baada ya muda nikaona kukaa na mtoto wa watu kimya sio vizuri nikaamua kwenda kumlipia mahari. Baada ya kumlipia akaanza kuforce ndoa(cheti). Mwanzoni sikujua nia yake hivyo nikaridhia tukafunga ndoa(kupewa cheti serikali) tukiwa mimi na yeye na rafiki yangu na mpenzi wake.

Aisee baada ya kupata cheti hapo ndo matatizo yalipoanzia (siwezi kusema hapa mapungufu ya mwenzangu maana hata mimi pia na mapungufu) but ndoa ilikuwa chungu(nilichukua mkopo kufanya biashara but haikwenda vizuri ikafa so mke akawa na mshahara mkubwa zaid yangu).

Hali ilikuwa mbaya sana kwangu mpaka ikafika hatua nikaamua kuacha kazi na kila kitu nikamwachia na kuja Dar kuanza moja maisha. Kwa bahati nzuri Mungu akanijalia hapa mjini. Ingawa mwanzo hali ilikuwa ngumu zaidi ya ugumu wa kawaida kulala na kula ilikuwa mtihani kwelikweli but nikaanza kufanikiwa taratibu.

Mpaka sasa naweza sema nimepata vitu viwili vitatu(biashara/nyumba kadhaa na usafiri). Sasa huku nina binti nilianzisha nae mahusiano na amekuwa bora sana kwangu kwa ushauri na kunijali.

Yule mke aliyeko mkoani nimekuwa nikitunza mtoto kwa juhudi zote hivyo kwenye hilo hana malalamiko kabisa.

Juzijuzi ameanzisha maada ya talaka anataka kuwa huru na mimi nikaona ni jambo jema ili na me nimuoe huyu niliyenae.

Tatizo mahakama imeandika muda wa talaka ambao mimi sitakuwa nchini hivyo siwezi kwenda. Yule mke kashauri niandike barua ya kupokea wito wa mahakama na pia kuruhusu aendelee na process ya talaka iendelee huku nikikubali kutunza mtoto kwa maandishi na amedai mahakamni ndio wamemshauri hivyo(kwenye mabaraza ya usuluhishi alitoa pesa barua zake zikapita).

Swali langu ni je kisheria ni sahihi kesi inavyoenda bila uwepo wangu? Mahakama itatoa hukumu?

Swali la pili kwenye mali; kila kitu tulichopata wakati naishi nae nilipoondoka nilimuachia vyote. Hizi nilizonazo sijachuma nae bora hata huyu dada niliyenae aseme tumechuma wote ila yule hana hata 10 aliyochangia hapa. Swali ni je hizi mali zangu za sasa zitahesabika kwenye talaka?(nimejaribu kumdadis akadai hana shida nazo)

Naomba wataalam wa sheria wanipe ushauri.
 
Moja, ulikosea kumfanya ajue progress yako Dar, ila kwa ushauri mtafute advocate akulead katika hili hata kama haupo ukimpa power of attorney atawakilisha matakwa yako kwenye shauri, nimepitia pia magumu yako ila nimekua makini kuhusisha wanawake katika mali kutokana na uzoefu wa awali

Sent using Jamii Forums mobile app

Hajui kila kitu kama idadi ya nyumba au gar ila anajua nimefanikiwa maana anazisikia biashara zangu
 
Hajui kila kitu kama idadi ya nyumba au gar ila anajua nimefanikiwa maana anazisikia biashara zangu
Mkuu nipo idara husika, aina ya kesi yako ina changamoto kwa kweli.

Niseme tu kutokujua idadi sahihi ya mali ulizonazo sio kitu. Mahakama ikitaka kujua unachomiliki itajua tu.

Kisheria yule bado ni mkeo hata baada ya kumuachia kila kitu ukaja kuanza maisha mapya na kumiliki hizo mali ulizonazo bado kuna gawio linalomuhusu kisheria kutoka kwenye hizo mali ulizo nazo.

Ulifanya kosa kama kumpa talaka ilibidi umpe wakati ule ambao ulimuachia kila kitu.



Maswali ya kujiuliza?
Je, Wakati unamuachia kila kitu uliandikishana nae au ulifanya kumsusia?

Mahakama haiwezi kutambua vitu ulivyomuachia kama mgao wa mlichochuma mkiwa pamoja ikiwa ulimuachia kienyeji.

Inahitaji upate mtu wa kukutetea ila kisheria kesi yako inabidi ianzie mahakama ya mwanzo ambayo huwaga inatakiwa muhusika awepo si muwakilishi na hata wakili hatakiwi.
Endapo kesi ya ikaisha na huyo mwanamke akashinda utahitaji kukata rufaa kwenda Mahakama ya wilaya husika ambapo hapo una uwezo wa kumuajiei wakili atakaeisimamia hiyo kesi.

Ila mara vipengele vingi kwenye sheria ya ndoa vinam,beba mwanamke hasa ikiwa mna watoto mliozaa pamoja.
 
Mkuu nipo idara husika, aina ya kesi yako ina changamoto kwa kweli.

Niseme tu kutokujua idadi sahihi ya mali ulizonazo sio kitu. Mahakama ikitaka kujua unachomiliki itajua tu.

Kisheria yule bado ni mkeo hata baada ya kumuachia kila kitu ukaja kuanza maisha mapya na kumiliki hizo mali ulizonazo bado kuna gawio linalomuhusu kisheria kutoka kwenye hizo mali ulizo nazo.

Ulifanya kosa kama kumpa talaka ilibidi umpe wakati ule ambao ulimuachia kila kitu.



Maswali ya kujiuliza?
Je, Wakati unamuachia kila kitu uliandikishana nae au ulifanya kumsusia?

Mahakama haiwezi kutambua vitu ulivyomuachia kama mgao wa mlichochuma mkiwa pamoja ikiwa ulimuachia kienyeji.

Inahitaji upate mtu wa kukutetea ila kisheria kesi yako inabidi ianzie mahakama ya mwanzo ambayo huwaga inatakiwa muhusika awepo si muwakilishi na hata wakili hatakiwi.
Endapo kesi ya ikaisha na huyo mwanamke akashinda utahitaji kukata rufaa kwenda Mahakama ya wilaya husika ambapo hapo una uwezo wa kumuajiei wakili atakaeisimamia hiyo kesi.

Ila mara vipengele vingi kwenye sheria ya ndoa vinam,beba mwanamke hasa ikiwa mna watoto mliozaa pamoja.
Good comment

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali lako Je, Ni sahihi kisheria kesi kusikilizwa bila uwepo wa mlalamikiwa? Na je, hukumu pia inaweza kutolewa bila uwepo wa mlalamikiwa?

Jibu ni Ndio, Kesi inaweza kusikilizwa na kutolewa hukumu bila uwepo wako Ikiwa tu,

Mahakama itathibitishiwa kuwa ulipata wito wa kuitwa Mahakamani na hukufika.

Kama ulikuwa na Dharula ya muhimu ilibidi ufike mahakamani utoe ombi la dharula kimaandish na vithibitisho vya kuthibitisha kuwa utakuwa na dharula siku husika hivyo hutoweza kufika mahakamani utoe na pendekezo la lini utakuwa na muda wa kuweza kufika mahakamani.

Kumbuka mahakama ya mwanzo haipokei muwakilishi wala mawakili inahitaji muhusika uwepo.

Ni vyema kuzingatia na kuuheshimu wito wa mahakama ili usije ukampa ushindi kirahisi mlalamikaji.
 
Mgawanyo wa mali zilizopatikana katika ndoa utategemea na mchango wa wahusika katika kupatikana kwa mali hizo, mali ulizo chuma baada ya kutengana nae kienyeji hazitamuhusu, zitamuhusu kama tu ataweza kuithibitishia mahakama alichangia nini katika kupatikana kwa mali hizo(mchango unaweza kuwa wa mali na hata hali unakubalika)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom