Tetesi: Sheria ya uchaguzi kuwasilishwa Bungeni, Mgombea urais awe ameishi nchini mfululizo miaka miwili ili akidhi sifa ya Urais

Tetesi: Sheria ya uchaguzi kuwasilishwa Bungeni, Mgombea urais awe ameishi nchini mfululizo miaka miwili ili akidhi sifa ya Urais

Habari JF siasa.

Ukishangaa ya Musa utayaona ya Farao/ Firauni.
Sheria mpya ya uchaguzi itawasilishwa bungeni mapema November 2019 au February 2020. Lengo la sheria hii ni kuwabana wagombea urais waghaibu au diaspora ambao wanajipanga kuwania urais.

Sheria hii mpya ya uchaguzi itamtaka Mgombea Urais awe ameishi nchini Tanzania kwa miaka walau miwili mfululuzo hadi kufikia Mwezi August 2020 ili akidhi kigezo cha kupewa Fomu na NEC na hatimaye kugombea urais.

Chanzo changu nyeti serikalini kimeniambia mkakati huu umeiva na nitege sikio Bungeni November 2019 au February 2020.

Mimi nilimkatalia katakata lakini kasimama na msimamo wake.

Nilimuuliza je kama Mtaka urais kasafiri nje ya nchi siku moja au hata wiki mbili ndani ya hiyo miaka miwili itakuwaje?

Alijibu hili halina shida hata kidogo lakini ikiwa ni mwezi au miezi kadhaa basi hapo Mgombea atakosa sifa.

Yangu macho!!
Knitting laws with a focus in individuals amounts to UNYANI aka Apedomia( according to Mtikila)
 
Hii sheria inaweza kuwa nzuri kama itakuwa haina lengo ovu. Hata mimi sioni ni vizuri mtu aliyekuwa anaishi nje ya nchi kwa miaka miwili arudi kugombea. Ila tuwe na tahadhari, kusafiri kusiwe kikwazo na hata kukaa muda mrefu kwa ajili ya matibabu isiwe kikwazo. Na tusiishie kwenye urais tu bali kwangu mimi ubunge ndiyo muhimu zaidi. Tuweke sheria kuwa mbunge ni lazima awe mkazi wa kudumu wa jimbo lake na asiwe anaishi sehemu nyingine. Familia yake pia iwe inaishi kwenye jimbo analoliwakilisha.
Hiyo hatuitaki
 
Huyu jamaa anatamani aonane na mungu amulize kabisa ili ajue ataishi mpaka lini ili aungane na maswaiba zake wa afrika mashariki M7 kagame na Nkulunziza
Ama kweli viongozi wakutokea sehemu za pwani, wana ustaarabu kutushinda, na hawana uchu wa madaraka. Mwinyi, Mkapana Kikwete
 
Mr polepole kiti ulichonacho alikuwa nacho kingunge, Nape nk. Leo wananyoshewa bunduki na hata bungeni akisema hawamuelewi. So hata kwako ni swala la muda.

Walileta muswaada wa sheria kandamizi ya habari. Leo anadukuliwa yeye [emoji23][emoji1787].
Pambana na hali yako weweee...kila siku kujaji maamuz ya watu....
 
Usiombe iwe hivyo,ni moja ya sheria mbaya kabisa kama itawekwa.

Kuna wanasiasa hukimbizwa uhamishoni kwa visa na visasi.
Unaweza kuwa upo kama balozi huko nje.
Unaweza enda kwa masomo ama shughuli yeyote ile ya kukujenga.

Tulianza na utanzania wa namna fulana,leo ukaazi,kesho race,ukabila,udini,ukanda n.k Mungu aiepushe mipango hii.
Amen
 
Wana wasiwasi gani na Lisu hata kama akishinda watampora ushindi....
Hivi ni kweli hata wewe hujui kwamba kwa sheria iliyopo Tundu Lissu hana sifa ya kugombea Urais? kuna haja gani ya kumtungia sheria nyengine? yeye nani?
 
OoH Lord Give Mr Lissu Strength.

Bado Lissu anaogopwa kiasi hiki??

Hahahahahaaa.

Jamani anaumwa tu hakusafiri kula bata.
Afu ukute mtu ka wewe ndo think tank la wenye fikra ka zako, Lissu is already done, huwezi fukuzwa ubunge kwa kosa la kutemper na fomu za maadili ya viongozi wa umma afu utegemee sheria ikuruhusu kugombea ukuu wa nchi, labda ashinde kesi atayoifungua (kwa mujibu wake).
 
Hakuna mtu atakayekuwa na sifa hiyo kwa sababu hata kitendo cha Mh. Rais kwenda ziara nje ya nchi kinamnyima sifa hiyo. Hawezi kukaa nchini miaka 2 mfululizo.
Hehe..kweli Tanzania tunawatu wa ajabu, hivi kuna mtu timamu unaweza hata jibu huu upuuzi ambao hata TL mwenyewe huenda ndo kauandika ili apate public sympathy na kuteka fikra za watu!!??
 
Sina hakika na sheria kutokurudi nyuma.

Sheria mpya ya bodi ya mikopo inaelekeza wanufaika wote wa mikopo ya elimu ya juu kulipa 15% ya mishahara yao. Ikumbukwe kuwa kabla ya sheria hii marejesho yalikuwa 8% ya mshahara
 
Back
Top Bottom