Shida zilipokubana uliwahi kuuza kitu gani kwa bei ya hasara ili ujinasue?

Shida zilipokubana uliwahi kuuza kitu gani kwa bei ya hasara ili ujinasue?

Shida zisikie Tu Mku Mwaka 2015 nilikuwa na Pikipiki nimempa jamaa afanye bodaboda nikapata tatizo kubwa sana wakuu. Nilipata kesi ambayo huenda leo ningekuwa natumikia kifungo jela ma la heshima yangu ingekuwa imeondoka na imani yangu kwa watu.

Nikapata bahati ya kuongea na mlalamikaji pamoja Na mwendesha mashitaka tuimalize kifamilia. wakawa wanahitaji hela kiasi fulani hivi kwa haraka nikawaomba wasubiri kidogo mshahara uingie wakatisha ukichelewa kesi kesho naanza kuita Mashahidi.

Nilitafuta mteja usiku ule ule Niliinunua 1.3M lakini niliuza laki tano fedha taslimu nikaenda kuuza na TV yangu kwa elfu arobaini pamoja na friji langu la laki sita kwa laki mbili tu mzee.

Mwaka jana nilipata changamoto ya kazi sehemu nilifua kinoma hadi nikaanza kutamani visungura maana ya bai sina, kodi ikawa mzigo home nilienda kuuza kiwanja changu nilinunua 4M nikauza kwa 2M ya kupew kwa awamu.

BINADAMU WAKIJUA UNA SHIDA WANAWEZA KUFANYA NEGOTIATION NA MKEO, WARUDISHE MAHARI WAMCHUKUE
Daaahh, pole sana mkuu
 
Niliweka bondi dell inspiron core i7 ya laki 9 nikachukua 50k
Hp elite book 7th generation niliuza laki🤣🤣
Simu nishauza sana zote kwa vei ya hasara
Samsung s7 edge niliuza 15k
Fridge la laki 9 niliuza laki 2
Funga kazi ka cresta nilinunua milioni 3 kwa pesa ya kubeti nikauza laki 8
Visa vingi vimesababishwa na kamari hasa spin and win nashukuru mungu hua sikosi mteja
Hakuna mtu hajawahi kuuza kitu akitingwa.

Hata Mimi nimewahi kuuza HP elite 150k Ili nipate nauli na hela ya kwenda kuanzia maisha Dar.

Ila Sasa nilifulia kurudisha taulo Mkoani ilikuwa Kwa Msaada wa msamalia mwema ambae tuliwahi soma nae sekondari Hadi Leo Huwa namtafuta sijampata 😆😆
 
Poleni sana wakuu,
Kwangu Mimi hayasimuliki.ila kubwa zaidi ni kitendo cha kuuza friji langu na TV kwa pamoja ili kujinusuru na njaa.

Jambo lililoniumiza hadi leo ni mtoto wangu kuniuliza kwanini nimeitoa TV ukutani nikawapa watu Sasa sisi tutaangalia nini?

Hii iliniumiza sana licha ya kwamba nilisolve na kuirudisha fasta lakini nilijikuta mwenye hatia,mengine ni mazito hayaelezeki ila muhimu tumuombe Mungu kwa Imani iliyo thabiti.
🤣🤣🤣🤣 Inahuzunisha ila acha nicheke hao watoto ndio wamenichekesha alooo!!
 
Daah aisee shida hz so poaa.

Kuna simu niliuza kwa bei ya hasara mix mteja kunambia hz cm ni mbovu ila ntanunua hvo hvo, cha ajabu anatumia mpaka leo na ni miaka kadhaa sasa na sifa kedekede.
😹😹😹 huyo ana dharau sana, nahisi ulitamani kumzaba kofi ila utafanyaje tena na una shida.!!
 
Nilichojifunza ukiwa na Shida kubwa, hakuna mtu wa nje wa kukusaidia, wewe mwenyewe na vitu uliyonayo ndio vina nafasi kubwa ya kukusaidia. Watu wengi unaowategemea watabaki kama watazamaji.
Nivizuri ukawa na vitu vinavyouzika kwa wepesi kwa ajili ya backup.

Namshukuru Mungu vyote nilivyoviuza baada ya msimu huo kupita vilirudi.
Ni rahisi mtu kukusaidia Ukiwa na mambo ambayo sio shida au starehe ila kwenye Changamoto Kila mtu anakukwepa na kukutenga,hapo anaeweza kukusaidia ni ndugu au Jamaa yako yeyote mwenye moyo tena Huwa ni wachache sana labda ubahatike mtaani uwe na washkaji wanaokufahamu vizuri napo ni Msaada wa mda,ishu ikiwa prolonged tafuta Msaada mwenyewe ujisaidie.

So ni muhimu sana kutunza hela ya akiba
 
Hakuna mtu hajawahi kuuza kitu akitingwa.

Hata Mimi nimewahi kuuza HP elite 150k Ili nipate nauli na hela ya kwenda kuanzia maisha Dar.

Ila Sasa nilifulia kurudisha taulo Mkoani ilikuwa Kwa Msaada wa msamalia mwema ambae tuliwahi soma nae sekondari Hadi Leo Huwa namtafuta sijampata 😆😆
mimi kuuza vitu imechangiwa sana na kamari
 
Shida zisikie Tu Mku Mwaka 2015 nilikuwa na Pikipiki nimempa jamaa afanye bodaboda nikapata tatizo kubwa sana wakuu. Nilipata kesi ambayo huenda leo ningekuwa natumikia kifungo jela ma la heshima yangu ingekuwa imeondoka na imani yangu kwa watu.

Nikapata bahati ya kuongea na mlalamikaji pamoja Na mwendesha mashitaka tuimalize kifamilia. wakawa wanahitaji hela kiasi fulani hivi kwa haraka nikawaomba wasubiri kidogo mshahara uingie wakatisha ukichelewa kesi kesho naanza kuita Mashahidi.

Nilitafuta mteja usiku ule ule Niliinunua 1.3M lakini niliuza laki tano fedha taslimu nikaenda kuuza na TV yangu kwa elfu arobaini pamoja na friji langu la laki sita kwa laki mbili tu mzee.

Mwaka jana nilipata changamoto ya kazi sehemu nilifua kinoma hadi nikaanza kutamani visungura maana ya bai sina, kodi ikawa mzigo home nilienda kuuza kiwanja changu nilinunua 4M nikauza kwa 2M ya kupew kwa awamu.

BINADAMU WAKIJUA UNA SHIDA WANAWEZA KUFANYA NEGOTIATION NA MKEO, WARUDISHE MAHARI WAMCHUKUE
Kesi ipi hiyo ya kukuvunjia heshima? Ulibaka?
 
nilishauza laptop kwa elfu 10 ,,,,,,,,,,,,ndiyo wee hesabu elfu moja moja yaaani buku 1,000 ziwe kumi ,,,ila ilikuwa mbovu ,,,,,,,,sema nilikuwa nahitahi nipate hela ya kutuma maombi ya chuo kikuu ardhi way back 2019 deadline ilikuwa ni kesho yake ...japo nilipata chuo ila ilinibidi tuuu maana nilikuwa sina msaada wowote ulee
Uliuza skrepa 🤣🤣🤣
 
Baada ya kufukuzwa kazi na ndani hakuna hata punje ya mchele watoto wameamka na mama yao hana cha kufanya ikinibidi kubeba kiatu changu aina ya cat ile original nikaanza kuzunguka kuhama nzima napiga uchinga kuanzia asubuhi hadi sa tisa mchana ndo napata mteja wa buku 20 nilikiuza huku machozi yananitoka lakin nilipata hela ya mchele na watoto wakala wali
🤣🤣🤣 tukiwaambia muwaachie wake zenu wafanye hata biashara ndogondogo za kujikimu hamtaki.!!
Ona sasa umekuwa chinga bila kutegemea 😹😹
 
Nilikunywa smart gin miaka miwili mpaka sukar ikashuka mwilini noma sana ........
Shida ni mwalimu anayetumia formula ngumu kukuelewesha topic usipo elewa ndo bai bai baba jeni maraaa kitanziiii shwaaaaaaaah....
😹😹😹😹
 
Niliwekaga tangazo home nauza nguo zangu na nikawatafuta wadada wale masista duu waliokuwa wanakuja kukodishaga nguo zangu waje tufanye biashara.!!
Mzee alivyorudi akalichana tangazo tulikula mikanda mimi pamoja na wateja wangu, aiseee wazee wa kichaga jau sana 🤣🤣🤣

Ila bila kujua ile ndio ilikuwa hatma yangu, ss hivi nimekuwa winga mzoefu.!! 😹
Noma sana
 
Back
Top Bottom