Shilingi Bilioni 3 Kudhamini Jezi za Timu ya Taifa

Sasa timu ya mchangani kama stars adidas wa kazi gani?
 
Nina uhakika Sheria Ngowi atashirikishwa katika mkataba huu ili kubalance mambo
 
Ila wabongo kwa ulalamishi hatujambo 😂😂😂😂

Hivi hao Adidas na nike na Puma wako wapi siku zote kuja kwenye hizi team ? Kwan team ya taifa imeanza leo? Au mnataka tukawapigie magoti ?
Halafu mwisho tuseme waTz hatunyanyuani? Wacha tenda ndogo kama hizi tuwape tu makampuni ya ndani ili pesa ibaki ndani,

Kwa sasa kilichobaki ni kuanzisha kiwanda kikubwa cha kuzalisha jersey hizo zote hapa Bongo
 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amelipongeza Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kuendelea kuwatumia wawekezaji wa ndani kutengeneza jezi za mpira wa miguu wa timu za Taifa.

Dkt. Ndumbaro ametoa pongezi hizo Septamba 11, 2023 Jijini Dar es Salaam mara baada ya kushuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Udhamini wa Jezi za Timu za mpira wa miguu za Taifa kati ya TFF na Sandaland Fashion Wear Ltd wa thamani ya Shilingi Bilioni 3 kwa muda wa miaka 5.

"Naipongeza Sandaland kwa kushinda zabuni hii, natoa rai kwenu kuongeza juhudi mfike nje ya mipaka ya Tanzania kwa kupata zabuni za kutengeneza jezi za klabu na timu za Taifa, naamini mtafanya hivyo" amesema Dkt. Ndumbaro.

Ameipongeza TFF kwa kusaini mkataba huo ambao utakua unawapa fedha, na kusisitiza kuwa uongozi wa Rais Walles Karia umefanikisha Tanzania kufuzu AFCON mara 2, timu ya Wanawake chini ya Miaka 17 na timu ya watu wenye ulemavu Tembo Warriors zimefika robo Fainali ya kombe la Dunia, huku Timu ya Wasichana ya Shule ya Sekondari ya Fountain Gate ya Dodoma, kuibuka mabingwa wa mashindano ya soka ya shule za Afrika ya CAF.

Kwa upande wake Rais Karia amesema Mkataba huo utahusisha Timu zote za Taifa za Mpira wa Miguu, ikiwa ni utekekezaji wa maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutaka wawekezaji wazawa kupewa nafasi zaidi nchini, ambapo amesema wataongeza wadhamini wengi katika maeneo mbalimbali kama ilivyo pia katika Ligi Kuu.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Sandaland Mhe. Yusuph Yenga amesema Kampuni hiyo ina uzoefu wa kutengeneza jezi hapa nchini ambapo tayari wana Mkataba timu ya Simba na kuahidi kuwa jezi hizo zitakuwa na ubora na viwango vya hali ya juu.
 

Attachments

  • IMG-20230911-WA0099.jpg
    27.1 KB · Views: 1
RRP Kitaa hizo Nyuzi zitakuwa Bei Gani ?

Tusije tukaweka bei ambayo sio rafiki watu kitaa wakaanza kujishonea zao; Watu kuzivaa Mtaani ni more Advantageous kuliko hata hizo Faranga...
 
Sasa timu ya mchangani kama stars adidas wa kazi gani?
Ni maono yako mkuu kuiona ya mchangani siwezi kukupinga ila kwangu mimi team yangu ya Taifa haiwezi kuwa ya mchangani.
 
Watanzania tuna changamoto ya kutothamini vya nyumbani, hta hao nike walianza km sandaland.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…