Shindano kwa wapishi wa JF

Shindano kwa wapishi wa JF

The Boss tunapo plan chakula tunazingatia makundi haya:
1;umri
2:aina ya kazi
3:wagonjwa katika stage tatu
4:vegetarian
5:mazingira
sasa tuzingatie kigezo kipi

Ahsante sana I was about to ask same question...
 
Last edited by a moderator:
Hiv huyu mnyamwezi alishatoa zawadi kwa aliyeshinda au alikuwa anatuumiza vichwa tu hapa?
Cc KOKUTONA na washiriki wenzangu wote
Bcc The Boss kwa ufafanuzi
 
Last edited by a moderator:
Hiv huyu mnyamwezi alishatoa zawadi kwa aliyeshinda au alikuwa anatuumiza vichwa tu hapa?
Cc KOKUTONA na washiriki wenzangu wote
Bcc The Boss kwa ufafanuzi

Amepotea mazima huyu bin adamu, hata sijui zawadi ataibuka nazo lini.......tulivojituma sasa kuweka menu za ukweee
 
Jumamosi:
Asubuhi: Uji wa lishe na vitumbua.

mchana. Kande za mahindi mabichi yaliyochanganywa na maharagwe mabichi kisha kuungwa na nazi. kisukumia maziwa ya mtindi.

Jioni: Rosti ya maboga yaliyochanganywa na nyama ya kuku ya kukaanga

N.B. Matunda na maji ni wakati wowote au saa moja baada ya mlo au kabla ya mlo.

JUMAPILI:

Asubuhi: Saa kumi na moja Maji ya kunywa ya moto with lemon/ asali. nusu lita.
Saa nne uji wa lishe na vinailon (aina ya viazi mbatata vya kukaanga)

Mchana: Ugali wa ndizi pamoja na rosti ya karanga iliyochanganywa na nyama ya ng'ombe.
ikisindikizwa na avocado, na juisi ya embe

Jioni: Maziwa fresh pamoja na mchemsho wa viazi mbatata.


Jumatatu: Asubuhi: Saa kumi na moja Maji ya kunywa ya moto with lemon/asali mdalasini
Saa Nne Uji lishe with mayai ya kukaanga yaliyochanganywa na vitunguu, green beans, celery,
karoti, kitunguu saumu na hoho.

Mchana: Michembe (wasukuma wanajua) with majani ya kunde ya kukausha pamoja na maziw mtindi.

Jioni. Samaki sato chukuchuku (mchemsho) pamoja na viazi mviringo mchemsho.



Jumanne: Asubuhi saa kumi na moja (maji ya kunywa ya moto kama kawa hapo juu)
Saa nee Supu ya mabogo iliyochanganywa na utumbo.

Mchana: Ugali wa ulezi na bamia.

Jioni. Chai ya maziwa na chips.

Nitaendelea.................

Nimependaje menyu yakooo jamanniii..nije nikupe visit lini asee
 
Nimependaje menyu yakooo jamanniii..nije nikupe visit lini asee
karibu wakati wowote. Hivi shindano liliisha jamani maana sikumaliza menu yangu kwa ajili ya kuwa occupied. sijui mshindi alikuwa nani.
 
karibu wakati wowote. Hivi shindano liliisha jamani maana sikumaliza menu yangu kwa ajili ya kuwa occupied. sijui mshindi alikuwa nani.

imalizie tu menu yako,deadline ni ni aprili mwisho wa mwezi
 
Mkuu The Boss menu hiyo ya week unamaana na Kipato cha hata Mtz anayeishi chini ya 1$ ?????
Maanaa naona kwa Mtz wa kawaida akila 1wk menu ya Kaunga na snowhite kwa wk 51 zilizobaki hawatakula tena
 
Last edited by a moderator:
Day 1;

A;chai rangi, magimbi ya kukaanga,roast maini na juisi fresh ya matunda
B;viazi vikuu vilivyoungwa na Karanga na njegere bila kusahau mbona za majani
C;futari ya mihogo,kunde ukishushia na chai ya maziwa na kipande cha chungwa

Day 2;

A;Maziwa fresh, omllete ,bagia za dengu na kipande cha tikiti maji
B;chips, mishikaki na salad(nyanya,vitunguu,karoti na tango) na glass ya red wine kupambana na cholestol
C;makande ,maziwa fresh na parachichi

Day 3;

A;uji wa ulezi uliochanganywa na maziwa mtindi ,siagi na Karanga
B;ndizi mshale za kupika na utumbo na juice ya ukwaju
C;fried coated potato with egg, salad (nyanya, kitunguu, carrot, pilipili na tango), kuku wa kukaanga na juice ya passion.
(dah! Siku heavy hii lazma iwe jumamosi)

Day 4;

A;chai rangi, sausage, maboga ya kuchemsha na kipande cha embe
B;firigisi za kusaga zilizochanganywa na mayai, ndizi za kuchoma, kachumbari na juice ya ubuyu
C;mchemsho wa mbogamboga na samaki, juice ya uyoga( hii juice weka mbali na watoto)

Day 5;

A;mihogo ya kuchemsha,chai ya maziwa na tango lenye mayonise
B;ndizi choma mbuzi choma, kachumbari na glass ya red wine
C;ndizi matoke zilizochanganywa na maharage, mboga za majani (hapa chinees itafaa) na chai ya maziwa

Day 6;

A;chai ya maziwa, vitumbua, yai la kuchemsha na juice ya parachichi
B;maboga ya nazi, maini roast na mboga za majani
C;futari ya viazi vitamu ilochanganywa na maharage na chai ya rangi

Day 7;

A;supu ya pweza, bagia za kunde na juice ya embe
B;salad ya matunda (embe,parachichi, ndizi, papai na tikiti) yenye asali baadae unashushia maziwa mtindi
C;kuku roast wa kusaga, na mkate wa mchele uliopakwa asali na juice ya uyoga.

Nb; kila mlo hapo utaseviwa na maji ya kunywa safi na salama

menu hii nimezingatia upishi wa asili na kisasa, na makundi yote ya chakula...bila kusahau vyakula maalum (aphrodisiac) kama vile juice ya uyoga, asali, supu ya pweza, parachichi na wine kumuweka mzee fit......
Juice ya uyoga plz
 
Back
Top Bottom