Shingi 200 leo kidogo inivue utu

Shingi 200 leo kidogo inivue utu

Sometimes ni kuacha tu.. hiy 200 inaweza kukupa hasara zaidi.

Kuchaniwa shati
Kuharibu vifaa au kupoteza kbs
Kupoteza hela zaidi ya 200 na vitambulisho
Kuumia (reception)
Kuingia hasara kulipa fidia mali za watu
Kuwa moja ya Memes (utarekodiwa na kuzagaa mitandaoni)

Yaan implications ni nyingi..... dunia ya sasa kuwa mnyonge baridi.. yaan ujue kulipiza kisasi bila direct contact na aggressor..
Dah mzee, mda mwingine inabidi uoneshe uanaume wako
 
Nilishajifunza hawa makonda sio watu wa kufanya nao ligi hawako sawa vichwani.
Kuna bro alipanda na demu wake akaanza ligi na konda. Demu wake badala ya kumtuliza bro akaanza kumchochea na wote wakaamsakama konda. Mimi nilikaa karibu na demu nikamshauri amtulie bro asimchochee, demu akanigeukia na mimi akaanza kunipayukia. Yule konda akapandwa na jazba akamziba demu kibao cha mdomo. Bro akaingilia konda alikuwa fiti akawatia wote mikononi. Tingo naye akaingilia kati kumtetea konda.

Kifupi bro akachaniwa shati tumbo lote wazi. Nikamwambia dada kama ungemtuliza bro msingefika hapo
Amna man, wao nao wanaangalia kama ni mnyonge wanakuchukulia point tatu
 
Wataalam,
Leo nmepanda daladala hapa dar, Yani saivi tu kama nusu saa ilopita nilikuwa natoka job nmeachana na yule broo aliyeniunganisha na hyo kazi(nmemuachia 30k)....

, Sasa nauli nakoenda ni 800, mi konda nikampa buku ila hakunrudishia chenji.
Ile nashuka nkadai chenji akasema eti ameshanipa halafu anakaza kichizi.

Nikamwambia "acha uxenge we kima, em tapika hyo 200"
Kumbe jamaa naye anataka anioneshe umwamba. Yeye anadai ashanipa chenji...nikimcheki juu ana rasta halafu macho mekundu. Mimi apo nmechomekea shati jeupe viatu vinang'aa kiwi.

Kujisächi mfukoni sioni hyo 200.
Nkaona huyu boya anataka anizoee,
Nikamshika shati Nikamwambia "we kima huondoki apa mpaka uniachie iyo 200"

Akasema '' nshakupa, kwahyo unataka nkurudishie chenji mara mbili upate na faida? "

Nkwambia "boya we hunijui"

Nkamkamata shingo apo nikashuka chinj huku namvuta kwa nje ya gari. Mda huo abiria wanalalamika wanawahi na dereva anamwambia anipe halo ka 200 waondoke.

ila jamaa akawa anaona kama zarau kuaibishwa vile, kwahyo tukawa tunadindiana kama majogoo wawili pale stendi.

Afu jamaa akiona nmechomekea anachukulia mim mchumba.

Stendi Zima ikasimama watu wote wameacha shughuli zao wanashangaa Hilo tukio la bro mtanashati aliyechomekea anadindiana na konda mvuta bangi kisa 200.

Nikamwambia "Oya, leo umeyakanyaga kmmk, Yani huondoki apa. hao abiria waambie watafute gesti maana watalala hapa, huondoki apa bila kuachia iyo 200"

Dah! Jamaa alivoona nmekaza sana na Niko serious halafu yeye ndo anapata hasara ikabidi aiteme hyo 200 na kuniachia.

Funzo: Sio Kila aliyechomekea ni don, mtumishi, wakuja au boya. Kuna wengine sisi ni maninja ila tunajidisguise kwenye mavazi tu. Msituchukulie simpo.
Na Mimi niunganishe na kazi my dear
 
Back
Top Bottom