Uchaguzi 2020 Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) limesikitishwa na kitendo uongozi wa CHADEMA kuwakemea na kuwafukuza watangazaji wake

Uchaguzi 2020 Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) limesikitishwa na kitendo uongozi wa CHADEMA kuwakemea na kuwafukuza watangazaji wake

Nawaza kwa mbali,
Ivi ndio CHADEMA wametinga IKULU KIMASIHARA TBC itaendelea kufanya kazi kama miaka yote?
Watageuka wapambe hata Zambia ilikuwa hivyo hivyo baada ya Michael Chilufya Sata kushinda vyombo vya habari vyote vilivyokuwa against yeye kesho yake viligeuka na kuanza kumpamba na kuponda chama tawala.
 
Mi sina chama lkn walichofanya CHADEMA ni upuuzi, walitakiwa kuwaacha waendelee na kazi yao. Kwa tendo lile ilikuwa ni hatari kwa usalama wa vyombo vyao na wakijua watangazaji pia. TCRA wana sheria na kanuni za maudhui, TBC hawataki kuingia mgogoro wa kulipishwa faini na TCRA.
 
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Limesikitishwa na kitendo uongozi wa CHADEMA kuwakemea na kuwafukuza watangazaji wake katika mkutano wao wa kuzindua Kampeni za Mgombea wao wa Urais katika viwanja vya Zakheim, Mbagala Jijini Dar es Salaam, jioni hii.

TBC1 na TBC Taifa kama chaneli za umma zilikuwa zinarusha matangazo ya moja kwa moja kwenye uzinduzi huo kwa mujibu wa sheria na miongozo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Hata hivyo, kwa mujibu wa mwongozo wa Tume wa mwaka 2020, (kifungu e na j), kanuni za maadili ya tasnia ya habari; vyombo vya utangazaji vya umma pia vinao wajibu wa kuhakikisha maudhui yanayorushwa hewani yanazingatia maadili ya taaluma na ya jamii.

Kitendo cha uongozi wa CHADEMA kutangaza kuwafukuza watangazaji wa TBC si cha kiungwana na kinahatarisha usalama wa watendaji hao na vifaa vyao.

Pamoja na kwamba TBC inapanga kutoa taarifa rasmi Polisi na kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kwa sasa inasitisha rasmi kurusha matangazo ya CHADEMA hadi hapo watendaji wake watakapohakikishiwa usalama.

TBC inapenda kutimiza wajibu wake wa kisheria na imekuwa tayari, siku zote, kufanya kazi na vyama vyote vya siasa bila ubaguzi.
tbc acha lawama , mnasema mnafuata maudhui ,ok sawa nakubali ila elewa nafikili hamkutakiwa kwenda maana kumbuka hiki ni kipindi cha kampeni watu watamwaga nyongo sana , sasa leo mlitia fora watu wakianza kumwaga nyongo mwajifanya kuweka uchambuzi , raha ya siasa ni wana siasa kumwaga nyongo ili mladi usiwe umbea au kumsingizia mtu , au kumtukana mtu, niwashauri achana na mikutano ya chadema basi ,mbona tangu mwanzo mlikua hamuonyeshi kipi leo kimewapeleka
?
 
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Limesikitishwa na kitendo uongozi wa CHADEMA kuwakemea na kuwafukuza watangazaji wake katika mkutano wao wa kuzindua Kampeni za Mgombea wao wa Urais katika viwanja vya Zakheim, Mbagala Jijini Dar es Salaam, jioni hii.

TBC1 na TBC Taifa kama chaneli za umma zilikuwa zinarusha matangazo ya moja kwa moja kwenye uzinduzi huo kwa mujibu wa sheria na miongozo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Hata hivyo, kwa mujibu wa mwongozo wa Tume wa mwaka 2020, (kifungu e na j), kanuni za maadili ya tasnia ya habari; vyombo vya utangazaji vya umma pia vinao wajibu wa kuhakikisha maudhui yanayorushwa hewani yanazingatia maadili ya taaluma na ya jamii.

Kitendo cha uongozi wa CHADEMA kutangaza kuwafukuza watangazaji wa TBC si cha kiungwana na kinahatarisha usalama wa watendaji hao na vifaa vyao.

Pamoja na kwamba TBC inapanga kutoa taarifa rasmi Polisi na kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kwa sasa inasitisha rasmi kurusha matangazo ya CHADEMA hadi hapo watendaji wake watakapohakikishiwa usalama.

TBC inapenda kutimiza wajibu wake wa kisheria na imekuwa tayari, siku zote, kufanya kazi na vyama vyote vya siasa bila ubaguzi.
Asiwalaumu Chadema, watazamaji ndiyo tulitaka wafukuzwe kwani hatukuwa Tayari kuwasikiliza wao badala wahusika wa mkutano. Kuhusu maudhui wasijifanye wao ni watabiri, wanawezaje kujua kitakachosemwa, sheria inahusu kilichoandaliwa na si anachokitamka mtu ghafla na hakukua na neno lolote baya.
 
Wakaendelee na vipindi vya kumsifu na kumuabudu mungu wa ccm na yesu wa ccm huko wanapoteza muda
IMG_20200828_204501.jpg
 
Mbowe alikosea pale ilikuwa wapewe dakika tano tu,kumi tano zilikuwa nyingi sana.
Hata hivyo iwe fundisho .....Kamanda wa anga alipaswa ndio apeperushe bendera kwa ujasiri ambao ameuonesha
 
Mheshimiwa Daktari Ayoub Ryoba,
Mengi ya kufurahisha na ya karaha yamefanywsa na TBC tumeyapokea kabla ya uongozi wsako na sasa kipindi cha uongozi wako.

Binafsi nilikupenda nilipokuwa nasoma makala zako na kukusikiliza katika radio na vipindi kadhaa vya runinga namna ulivyokuwa unachambua hoja kama mtu mwenye mawazo huru. Nilijivunia wewe, kama ambavyo nimeendelea kujivunia Jenerali Ulimweengu.

Lakini, kilichofanyika leo..kilichofanywa leo na wqafanyakazi wwalio chini yako (nashindwa kuamini kwamba ulikuwa huoni kilichokuwa kinafanywa). Umeyaona, ukanyamaza kimya. Umeona reaction ya wananchi, bado umenyamaza kimya. Dr Ayoub, utu uzima busara...kuomba radhi nao ni uungwana.

Kilichotokea leo kwenye uzinduzi wa kampeni za CHADEMA ni aibu kwa TBC, ni aibu kwa Taifa kutoka kwwa waale waliokuwa wakiangalia toka mataifa mengine..ni aibu kubwa kwsa tasnia ya habari...ni mfululizo wa aibu aibu.

Jambo walilolifanya leo TBC si mara ya kwsanza. Mwaka 2015 pale Jangwani wsalifanya hivyo na Mar. Marin Hassan aliponea chupu chupu kipigo kikuu, nakumbuka aliokolewa na red brigade..hata gari la TBC ilibidi lizingirwe na Polisi. Ndipo, viongozi wa UKAWA waalilazimika kuwaatuliza wsananchi. Leo tena, vijana wako wamepanga na kutimiza walichopanga. Kilichofanywa na TBC leo ndicho kilichofanywa na Global TV online. Inathibitisha ni mpamgo wa makusudi.

Najua unajua kuwa kuna kuwajibika kwsa makosa ya wale waliochini yako.

Nasubiri busara zako..
 
Back
Top Bottom